Wakatoliki (TEC) wameanza, huenda wakafuata waprotestant (CCT), wapentekoste(PCT) na wasabato. Rais Samia nakushauri achana na DP world!

Hutkaa uamini huyo Bibi atakavyofika nungwi akiwa peku...
Thubutuuuu hujui nguvu ya raisi ndugu yangu tupo wengi tunaomsupport hakuna wa kumtisha hayo maneno maneno ya nyie walafi tumeshawazoea msipokuwa na maslahi binafsi lazima mponde
 

Mashehe nao watakuwa wanajipanga sasa!
 
Thubutuuuu hujui nguvu ya raisi ndugu yangu tupo wengi tunaomsupport hakuna wa kumtisha hayo maneno maneno ya nyie walafi tumeshawazoea msipokuwa na maslahi binafsi lazima mponde
Huna unalojua Rais ndebwedo huyo...
 
Huna unalojua Rais ndebwedo huyo...
Wewe baada ya kuhangaikia kula yako unahangaika na dp world na raisi watu wengine bwana huwezi kubadilisha chochote, na mungu atamlinda na wanafki wenye chuki kama wewe na hao wenzio walafi
 
 
Ujumbe umefika.
 
Serikali inaendeshwa kwa utaratibu wake hizo taasisi za Kikristo umezitaja kwa mahaba yako taja na Waislam harafu tuone mpambano.
 
Hata Baraza la mashehe nao wanaweza kukaa na kutoa tamko lao la kuupinga mkataba, lakini hata kama Baraza la mashehe wataupinga mkataba, haimaanishi kwamba waumini wao wote Wanaoupinga mkataba. Lakini pia mkataba huu umeshasainiwa na umeshapitishwa na Bunge, hivi sasa NI too late. Ushauri wangu Kwa serikali msikubali kuyumbishwa, Kwa sababu mkataba huu ukianza baada ya miaka 15 hao wote wanaopinga, kama watakuwa hai, naamini watakufa Kwa Aibu. GDP per capital ya Tanzania mwaka 1960 na 1970 ilikuwa 165, miaka hivyohivyo ya Nchi ya Thailand ilikuwa 166, Leo hii GDP per capital yetu NI 1400 ya Nchi ya Thailand NI zaidi ya 7000. Ukiangalia rasilimali Tanzania tuna rasilimali nyingi kuwazidi Thailand. Tujiulize Kwa nini uchumi wetu haukui ? Jibu lake NI Kwa mambo kama haya, kuupinga VITU hata visivyostshili kupingwa. Mama piga kazi, tunajua unaipenda na unaipigania Nchi yako, endless kumtanguliza Mungu mbele. Hauna Shaka watakukumbuka Sana utakapo maliza kipindi chako cha uongozi alichokupangia Mungu.
 
Wewe baada ya kuhangaikia kula yako unahangaika na dp world na raisi watu wengine bwana huwezi kubadilisha chochote, na mungu atamlinda na wanafki wenye chuki kama wewe na hao wenzio walafi
Takataka wewe, kula yangu ndio inayomlisha Rais.... Nyie vilaza wa CCM hamna mmalojua Nchi hii.
 
Umeandika vizuri sana ndugu yangu. Kwa utambulisho wako, bila shaka wewe ni ndugu yetu kutoka Zenji na ni wa Imani ya kiislamu. Umeupendeza moyo wangu kwa kujipambanua na kukaa mbali na hisia na itikadi za kidini kuhusu sakata linaloendelea la mkataba wa bandari. Nimekuwa nikishangaa na kusikitishwa baadhi ya ndugu zetu waislamu wanaupigania mkataba na wanaonekana kuwashutumu wakosoaji na kumuunga mkono Rais Samia na Serikali yake ktk suala ambalo lina dalili za wazi za rushwa na ufisadi mkubwa wa kimataifa.
Madhehebu ya kikristo hususan Kanisa Katoliki linaongozwa na wasomi wengi wabobezi ktk fani mbalimbali. Ni makanisa yamejaa wasomi na ni viongozi na watumishi ktk taasisi mbalimbali za Serikali (GOs) na zile zisizo za Serikali (NGOs). Wanajua kila kitu kinachofanyika ndani ya Nchi hii. Wanazo taarifa sahihi kabisa kuhusu kila kitu kilichofanyika na kinachofanyika kuhusiana na Mkataba huu wa Bandari. TEC wanapotoa Tamko, wanajua.
Mwanamapinduzi na mzalendo Askofu Mwamakula ktk ule mkutano wa Temeke alitufumbua akili kwa kutujulisha na kuitahadharisha Serikali kuwa hawakurupuki, wanajua kila kitu kinachoendelea Serikalini kwani wana washirika ktk makanisa yao walio ktk System wanavujisha taarifa ya kila kitu kinachoendelea.
TEC inajua na taarifa zoote wanazo juu ya kwa nini ndugu zetu Waislamu wanaunga mkono Rais Samia na mkataba wake huu. Wanajua kuna elementi za udini zinazolenga kueneza imani ya uislamu Tanzania.
Kanisa Katoliki ni Kanisa kubwa hapa Tanzania na duniani kwa jumla. Askofu mkuu wa Rumi (Papa) ndiye Kiongozi mkubwa na maarufu wa kidini kuliko wote duniani. Kwa Mfumo wa Kanisa Katoliki, sauti au Tamko la Baraza la Maaskofu wa Kikatoliki (TEC) huwa ni Tamko la Vatican, yaani, ni Tamko la "Baba Mtakatifu Papa. TEC haifanyi kitu ila kwa kibali cha Papa; hivyo, Papa ametamka, Mkataba wa Bandari kati ya Tanzania na UAE una kasoro; hivyo, ufutwe, au, ufanyiwe marekebisho kwa kuwashirikisha kikamilifu Watanzania wote.
Askofu mkuu wa Kanisa la Rumi, Papa, ana ushawishi mkubwa sana wa maamuzi ya kisiasa na kiuchumi ktk Nchi nyingi duniani. Anaheshimika sana. Hata Waarabu wanamheshimu sana kama anavyowaheshimu wao. UAE wanalijua hilo pia na watalichukuwa kwa tahadhari kubwa Tamko la TEC kwani wanajua madhara yake wakikiuka.
Mwisho, Watanzania kamwe hawapingi uwekezaji, bali, wanapinga namna Serikali inavyoingia mikataba ya uwekezaji. Mikataba inakuwa imegubikwa na rushwa na ufisadi, hivyo, Kufanya uwekezaji usiwe wenye manufaa kwa Tanzania.
Nawashauri ndugu zangu Waislamu, Nchi hii ni yetu sote; Imani za dini ni kutuongoza kwa Mungu. Lakini imani za dini zetu zinadai haki na siyo kutetea uovu. Mbona masheikh mnakemea maovu misikitini kwa waumini wenu, mumekwama nini ktk hili? Nashangaa!
Msomi Sheikh Alhad Musa na hekima zako, mbona sijakusikia? Sheikh Mkuu Zubeir, mbona kimya mnawaacha wahuni waganga wa jadi na washirikina akina, ati 'sheikh' mwaipopo ndiyo wanaisemea Bakwata! Kunani? Mbona ninyi ni wanachama wa Baraza la amani la Taifa, hamjawasiliana na wenzenu wa TEC kupeana taarifa sahihi juu ya mchezo mchafu unaofanywa na Serikali kuhusiana na Mkataba huu mbovu wa Bandari? Uislamu hauwezi kuenezwa kwa namna hiyo. Kuunga mkono uovu?!
Ndugu zetu Waislamu kumbukeni, uislamu wa Tanzania uko tofauti kabisa na Nchi nyingi nyingine duniani. Ninyi ni ndugu wa Watanzania wote maana unakuta ktk familia moja kuna Wakristo na Waislamu na wanaishi pamoja kwa amani. Wapo wanandoa waliooana, mke ni mkristo, mume ni mwislamu na wanaishi kwa upendo na amani. Ndugu zetu Waislamu acheni kudanganywa na hawa akina nape, ni wachumiatumbo, wanaingiza udini ktk suala hili ili wapate mradi wao; akina nchemba. Akina mkumbo. Akina wasira. Akina kasheku. Akina lusinde. Akina chalamila, n.k. Hawa ni wajasiriasiasa tu. Ni hatari.
 
Watu, ukitia ndani cct, tec, pct, bakwata na wasabato wana uhuru wa kusema lolote, lakini serikali haipangiwi na watu baki cha kufanya. Muda ukifika, DP world watapewa bandari zote za Tanganyika ili waziendeshe. Ambaye haitaki DP world ahamie Burundi
 
Takataka wewe, kula yangu ndio inayomlisha Rais.... Nyie vilaza wa CCM hamna mmalojua Nchi hii.
Hiyo kura yako moja ya chuki na matusi bora ukae nayo tu, enemy of progress wewe
 
Hiyo kura yako moja ya chuki na matusi bora ukae nayo tu, enemy of progress wewe
Wewe ni mjinga mmoja tu, hakuna mahali nimesema "kura" nimesema kula uwe mtambuzi wa maandishi takataka wewe hujui hata kuandika.
 
Wewe ni mjinga mmoja tu, hakuna mahali nimesema "kura" nimesema kula uwe mtambuzi wa maandishi takataka wewe hujui hata kuandika.
Huna unachojua sasa kula yako inamhusu nini raisi wetu embu toa umbumbumbu wako hapa , ujuaji mwingi utakuta hata mkataba wenyewe hujausoma boya wewe kufuata mkumbo tu
 
Jambo Hili la DP World linafunzo kubwa sana kwa mtanzania aliye makini.Kwa namna yoyote ambavyo litaisha tayari limeshaacha dosari na maswali mengi kwa watanzania.
 
Serikali inaongozwa na watu, usizipuuze taasisi za kidini, mjinga pekee atazipuuza
 
Ok...binafsi nimekuelewa...ila katika kuachana na mkataba huu unashauri process iweje kwa maana serikali ichukue mkakati upi...
 
Kilichotokea ni kuwa tayari nchi imeshapasuka mapande mapande...Kuna mpasuko wa Tanganyika vs Zanzibar...Kuna mpasuko wa kidini....Kuna mpasuko ndani ya CCM....Kuna mpasuko was walalahoi dhidi ya elites....kwa hakika kazi ipo....
Binafsi nimeona awamu zote...ya Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli na Sasa Samia...ila kwa haya ya Sasa dah mmmmhhh yanatia hofu kwa kweli...
 
Huijui Dunia inavyoendeshwa wewe endelea kula maharage yako ulale.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…