Umepotosha kwa kiasi kikubwa, unaonekana hujasoma hata ule waraka wa Vatican, ulichofanya ni kuokoteza maneno kwa wengine na kuja kuanzisha huu uzi wako hapa, hujafanya uchunguzi wowote, sasa hiyo aibu aione nani?
- Kama hutaki mashoga wavumiliwe na kutambuliwa ndani ya Kanisa Katoliki, unataka wezi, waongo kama wewe, na wazinzi, wao pekee ndio waendelee kuvumiliwa? Kanisa Katoliki haliishi kwenye misingi ya kinafiki.
- Kwanini hutaki mashoga wapewe sakramenti kama waumini wengine? au wale wanaopewa ni watakatifu? hayupo yeyote miongoni mwao mwenye dhambi? Hapa unaonesha ulivyojaa ubinafsi, Papa yuko above your thinking capacity.
- Wapi umeona kwenye ule waraka wa Vatican pameandikwa Kanisa Katoliki litabariki mashoga? tuwekee hapa tupaone, kisha nami nitakuwekea pale palipoandikwa Kanisa Katoliki litabariki mali za mashoga, sio mashoga kama ulivyopotosha hapa.
Hii ni sawa na kubariki mali za wengine wasiojulikana tabia na matendo yao, hakuna yeyote anayejulikana kama ni mzinzi sababu hufanyia sirini, mwizi hufanyia sirini, kujaribu kuwatenga mashoga kama vile wao pekee ndio wenye dhambi ni unafiki na ubinafsi, Papa hataki huu unafiki.
Papa anajua miongoni mwetu hayupo aliyekamilika, Kanisa Katoliki pia linajua hivyo, tukianza kutazamana usoni na kutengana mwisho wa siku huko kanisani atabaki nani? injili atahubiriwa nani? hujui hata Yesu Kristu alikuja duniani ili kuwahubiria wenye dhambi wapate kuokoka?
Mna upeo mdogo sana kifikra, na thinking yenu ni ya kijima sana wakati Kanisa Katoliki lilishatoka huko.
Sent from my SM-G900H using
JamiiForums mobile app