KERO Wakazi wa Goba njia ya Tegeta A kwenda Madawa na Kulangwa tuna changamoto kubwa ya Barabara

KERO Wakazi wa Goba njia ya Tegeta A kwenda Madawa na Kulangwa tuna changamoto kubwa ya Barabara

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Ms Billionaire

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2020
Posts
2,452
Reaction score
4,955
Nawasalimu kwa Jina la Jamhuri. Kazi iendelee.

Mama Samia, wakazi na wapiga kura wako wa Goba njia ya Tegeta A kwenda kutokea Madawa na njia Tegeta A kuelekea Kulangwa kupitia makanisa ya Katoliki Tegeta A, na Anglikana Tegeta A tuna changamoto kubwa sana ya barabara haitaki kutatuliwa kwa miaka mingi sasa.

Ile njia ni mbovu sana na wakazi wa maeneo hayo waliwahi kumfuata Mwenyekiti wa Serikali za Mtaa Kumwomba awasadie kupambania kibali cha kurekebisha barabara walichojibiwa na serikali ya mtaa ni hivi: “HIYO SIYO KAZI YENU”

Ikaja kugundulika kwamba ile njia inamwingizia faida kubwa mwenyekiti ya serikali ya mtaa wa Goba Tegeta A kwasababu ana mradi wake wa Bajaji. So anajua akikubali barabara itengenezwe itafanya madaladala yapite kule na yeye atapoteza mradi wake wa Bajaji.

Wakazi wa Tegeta A na Kulangwa tunahitaji karavati kwenye makazi yetu. Mbunge na diwani wamenyamaza labda tukikuomba wewe mama utawakumbusha wajibu wao.

Tunateseka na hiki kipindi cha mvua school bus zinapita na watoto wetu ni hatari sana sehemu zingine karavati zimebomoka kabisa mfano hii njia karibu na kituo cha afya cha Mtakatifu Yohanne Goba Kulangwa njia ni mbovu sana na viongozi wa serikali za mtaa hawataki kutengeneza hiyo njia kwa sababu wanajua watakosa mapato ya miradi yao ya bajaji na pikipiki.

Mama samia tunaomba msaada wa njia hizo kuerekebishwa tuwekewe Karavati tukiwafuata viongozi wa serikali za mtaa hawatoi ushirikiano kwasababu hawataki kupoteza mapato yao ya Bajaji na bodaboda.

Nimeambatanisha ramani ya Goba Kulangwa inayopakana na Tegeta A ambayo inaenda kutokea St. Yohane Health Center kwenda kwenye makazi.

Viongozi, hapo nlipoweka alama nyekundu kuna mto unapita, Karavati limebomoka upande na school bus za watoto wetu zinapita hapo kila siku na watoto. Tunaogopa watoto wasije kusombwa na maji tunaomba serikali kuu itusaidie kama serikali tunazoishi nazo mtaani hazina msaada. TUNAOMBA KARAVATI ENEO HILO. Na tunaomba hizo njia zirekebishwe kwasababu zimechimbika sana kwasababu ya mvua.

Cc Mbunge wa Ubungo, Diwani wa Goba kulangwa, serikali ya mtaa Goba kulangwa na Tegeta A.

Nawasilisha.

cc309ef9-7a1b-4e14-a529-651420da9b3e.jpeg
 
Tunapoelekea viongozi wengi kata, mitaa na watendaji mbali mbali katika wilaya na mikoa watapigika, wanaurasimu wa ajabu ajabu mno Mimi niwaombe Waheshimiwa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya msaidieni Mheshiwa Raisi wetu kwa dhati muwe basi na amsha amsha hata kama za Mheshiwa Makonda na wengine wasiozidi kumi simamieni haki kwa yoyote. Waonyeni watendaji wenu mara kwa mara juu ya rushwa na uonevu mwingi.
 
1. Tegeta A ipo Jimbo la Kibamba na siyo Jimbo la Ubungo kwa hiyo Mbunge wa Ubungo hahusiki na eneo hilo.

2. Mimi ni dereva bajaji na ninamiliki bajaji. Katika udereva wangu nimegundua kwamba bajaji inahitaji njia nzuri kuliko vyomvo vingine vya moto ambavyo pia nimewahi kuviendesha. Kwa hiyo hoja kwamba Mwenyekiti wa Mtaa hataki kutengeneza barabara kwa sababu ya bajaji zake ni hoja dhaifu sana.

3. Nimewahi kuishi Tegeta A na nimefanya kazi kadhaa za CCM na Serikali huko: Mwenyekiti wa sasa ninamjua vizuri na namna anavyojitahidi kuleta maendeleo huko Tegeta A. Kwa hiyo ukiniambia anahujumu miradi mimi ninakataa.

4. Wakazi na wenyeji wa Tegeta A na mabingwa wa Majungu kwa viongozi wao. Hata Diwani wa hapo Mh. Ester anapigwa majungu eti kwamba kwa kuwa yeye ni wa Kinzudi basi maendeleo anapeleka kwake. Mara anaambiwa anataka kuanzisha kata nyingine ya Kinzudi kwa hiyo anawabagua Tegeta A.

5. Pamoja na hayo, Manispaa ya Ubungo imepokea pesa za Mradi wa DMDP kwa ajili ya miundombinu ya barabara kwa hiyo bila shaka zitafika huko.
 
Siku zikipiga mvua kubwa wakazi wa Goba katikati ya tegeta A na kulangwa hatuna mawasiliano wakati kuna njia nyingi sana na zote zinahitaji caravat, mfano hiyo njia niliyopost ramani, njia nyingine ni kutokea hapa deez pub kuingia kuelekea makanisa ya catholic tegeta A kote kunahitajika caravat sasa viongozi wetu mkikaa kimya ni kama vile mnaafikiana na tabia za wenyeviti wa serikali.
 
Kuhalisia hiyo siyo kazi yenu, ni kazi ya serikali iliyopo madarakani. Sababu nyie ni walipa kodi na ni haki yenu kurekekebishiwa hiyo njia, kitu ambacho ni wajibu wa serikali. Na haiwezekani mlipe kodi na hapohapo kazi ya serikali mfanye nyinyi wananchi, huo ni ujinga na upumbavu. Kama ni hivyo then pesa zenu za kodi zinaenda wapi? Zinafanyiwa nini?

Kama serikali haitekelezi wajibu wake basi ni haki wananchi kutokulipa kodi, lakini si unajua jinsi gani serikali ilivyo katili kwa wakiuka wajibu wasiolipa kodi? Sasa na nyinyi kuweni makatili kwa serikali inayogoma au kuzembea kutekeleza wajibu wake na kuwanyima haki zenu. Au watazoea na tatizo litajirudia milele.

Badala ya kwenda kwa huyo kiongozi awape kibali mfanye kazi isiyowahusu kisheria. Mlitakiwa muende kumdai haki yenu hiyo barabara irekebishwe haraka iwezekanavyo sababu inaumiza harakati za wananchi kiuchumi na mbaya zaidi kuhatarisha maisha yenu. Wananchi amkeni na muache heshima na ustaarabu wa uoga.

Kisheria huyo kiongozi hana makosa yoyote kuwajibu hivyo na hamtomfanya chochote wala hao viongozi wakubwa vilevile, sababu wazi ujinga na makosa ni yenu. Hata hiyo serikali inajua hilo na inakaa kimya ili wachache wale kodi na jasho lenu kizembe kwa uzembe wenu wananchi.

Mwananchi asiyejua wajibu na hazi zake mwenyewe ni mtumwa wa serikali ndani ya nchi huru.
 
Viongozi hawasimamii watumishi ipasavyo mikoani na wilayani,italeta majanga, na watumishi wakiona bosi wao au msaidizi, hakoromi wanajua Serikali inahalalisha uovu wao.

Hali ni mbaya tunapaza sauti Serikali isikie hatushindwi kuchukua hatua na kujisalimisha ila tunaheshimu sana mamlaka basi mmalaka ziimarishe imani kwetu
 
1. Tegeta A ipo Jimbo la Kibamba na siyo Jimbo la Ubungo kwa hiyo Mbunge wa Ubungo hahusiki na eneo hilo.

2. Mimi ni dereva bajaji na ninamiliki bajaji. Katika udereva wangu nimegundua kwamba bajaji inahitaji njia nzuri kuliko vyomvo vingine vya moto ambavyo pia nimewahi kuviendesha. Kwa hiyo hoja kwamba Mwenyekiti wa Mtaa hataki kutengeneza barabara kwa sababu ya bajaji zake ni hoja dhaifu sana.

3. Nimewahi kuishi Tegeta A na nimefanya kazi kadhaa za CCM na Serikali huko: Mwenyekiti wa sasa ninamjua vizuri na namna anavyojitahidi kuleta maendeleo huko Tegeta A. Kwa hiyo ukiniambia anahujumu miradi mimi ninakataa.

4. Wakazi na wenyeji wa Tegeta A na mabingwa wa Majungu kwa viongozi wao. Hata Diwani wa hapo Mh. Ester anapigwa majungu eti kwamba kwa kuwa yeye ni wa Kinzudi basi maendeleo anapeleka kwake. Mara anaambiwa anataka kuanzisha kata nyingine ya Kinzudi kwa hiyo anawabagua Tegeta A.

5. Pamoja na hayo, Manispaa ya Ubungo imepokea pesa za Mradi wa DMDP kwa ajili ya miundombinu ya barabara kwa hiyo bila shaka zitafika huko.
1. Imeambatanishwa picha ya postcode ikionesha Tegeta A na Goba kulangwa. Kibamba inaingiliana vipi na Goba kulangwa?

2. Una taarifa kwamba ile njia inayoenda kutokea shule ya msingi tegeta A kipindi cha mvua za kawaida watu huwa wanapaki magari mbali wanavuka na boda boda? Na mvua zikizidi ndo hapapitiki kabisa?

3: unasema umewahi kuishi Tegeta A, lini? Mwaka gani? Na ulikaa eneo ambalo ni lazima uvuke caravat kwenda kwako?

4: umejibu hoja za kutetea ugali wako lakini hujajibu hoja za kuhusu caravat pale. Hizo hujuma za diwani zinahusika nini na kutengeneza barabara?

5: umesema tegeta A haipo ubungo ipo kibamba, hizo pesa za halmashauri ya ubungo zinaendaje kata za kibamba? Mbona unajichanganya Kiongozi fanyeni kazi acha janja janja. Nenda kaongee na wakazi wa mitaa watakueleza kinaga ubaga huu sio mda wa kuwa chawa wa viongozi. Fanyeni kututengenezea barabara muone kama tutaongelea hizo bajaji zenu. Nani afanye figisu juu ya viongozi kila mtu ana maisha yake hamna mwenye tamaa na hivyo vyeo vyenu. Wajibikeni.

IMG_6178.png
IMG_6179.png
 
Inaonekana hujui unachokiandika ama umetumiwa taarifa na wewe ukakurupuka kuileta hapa.

1. Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo/Wilaya ya Ubungo ina majimbo mawili ya uchaguzi ambayo ni Jimbo la Kibamba ambalo mbunge wake ni Issa Mtemvu, na Jimbo la Ubungo ambalo mbunge ni Kitila Mkumbo.

2. Jimbo la Kibamba lina kata 6 ambazo ni Kibamba, Mbezi, Msigani, Saranga, Kimara, Goba.

3. Ndani ya Kata ya Goba ndipo unapatikana Mtaa wa Tegeta A.

4. Kwa hiyo ni hivi Mtaa wa Tegeta A unapatikana ndani ya Jimbo la Kibamba, Tarafa ya Kibamba, Wilaya ya Ubungo, Dar es Salaam.

5. Kama nilivyosema: Tegeta A mna majungu sana. Sasa embu angalia; wewe hata mbunge wako humjui, hujui upo jimbo gani wala hujishughulishi kujua.

6. Maana yake hata kiasi cha pesa kilichotengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo huko hujui, na badala hata ya kuuliza unaleta taarifa humu ambayo hata wewe mwenyewe huielewi.

7. Ningekutajia kazi nilizofanya huko Tegeta A na mwaka ila kwa kuwa ninyi huko ni mabingwa wa kuzuriana sikwambii. Wala sina maslahi yeyote na mtu yeyote humo kwenu.

8. Barabara za huko zina changamoto kama maeneo mengine ya nchi.

9. Wilaya ya Ubungo inaongoza kwa kuwa na wahamiaji wengi sana kutoka maeneo mengine ya nchi, kwa hiyo hili linafanya huduma za huko kuzidiwa kwa kiasi kikubwa.

10. Hata hivyo, Halmashauri inajitahidi sana kuboresha huduma. Mfano Shule ya Msingi Tegeta A ni shule ya kwanza ya Msingi Tanzania kuwa na darasa maalum la masomo Digitali.

11. Ninapafahamu vizuri sana Tegeta A.
 
Inaonekana hujui unachokiandika ama umetumiwa taarifa na wewe ukakurupuka kuileta hapa.

1. Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo/Wilaya ya Ubungo ina majimbo mawili ya uchaguzi ambayo ni Jimbo la Kibamba ambalo mbunge wake ni Issa Mtemvu, na Jimbo la Ubungo ambalo mbunge ni Kitila Mkumbo.

2. Jimbo la Kibamba lina kata 6 ambazo ni Kibamba, Mbezi, Msigani, Saranga, Kimara, Goba.

3. Ndani ya Kata ya Goba ndipo unapatikana Mtaa wa Tegeta A.

4. Kwa hiyo ni hivi Mtaa wa Tegeta A unapatikana ndani ya Jimbo la Kibamba, Tarafa ya Kibamba, Wilaya ya Ubungo, Dar es Salaam.

5. Kama nilivyosema: Tegeta A mna majungu sana. Sasa embu angali; wewe hata mbunge wako humjui, hujui upo jimbo gani wala hujishughulishi kujua.

6. Maana yake hata kiasi cha pesa kilichotengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo huko hujui, na badala hata ya kuuliza unaleta taarifa humu ambayo hata wewe mwenyewe huielewi.

7. Ningekutajia kazi nilizofanya huko Tegeta A na mwaka ila kwa kuwa ninyi huko ni mabingwa wa kuzuriana sikwambii. Wala sina maslahi yeyote na mtu yeyote humo kwenu.

8. Barabara za huko zina changamoto kama maeneo mengine ya nchi.

9. Wilaya ya Ubungo inaongoza kwa kuwa na wahamiaji wengi sana kutoka maeneo mengine ya nchi, kwa hiyo hili linafanya huduma za huko kuzidiwa kwa kiasi kikubwa.

10. Hata hivyo, Halmashauri inajitahidi sana kuboresha huduma. Mfano Shule ya Msingi Tegeta A ni shule ya kwanza ya Msingi Tanzania kuwa na darasa maalum la masomo Digitali.

11. Ninapafahamu vizuri sana Tegeta A.
Kwa taarifa hizi za ndani unazotoa wewe ni mtendaji wa ndani kabisa wa huku najua taarifa umeipata. Hayo maelezo ya wilaya ipi iko wapi kaa na watendaji wenzio bandikeni tangazo kwahiyo nikusikilize wewe au postcode?

Mimi nijue fungu lililotoka hizo taarifa napata wapi? Kama wewe hukai goba unapata wapi taarifa? Tufanye mimi ni mwanachi wa kawaida kabisa mkereketwa nimeleta malalamiko nasema CARAVAT ZIWEKWE lasivyo wote mtafyekwa. Hatutaki janja janja. Tunataka barabara zitengenezwe
 
Kwa taarifa hizi za ndani unazotoa wewe ni mtendaji wa ndani kabisa wa huku najua taarifa umeipata. Hayo maelezo ya wilaya ipi iko wapi kaa na watendaji wenzio bandikeni tangazo kwahiyo nikusikilize wewe au postcode?

Mimi nijue fungu lililotoka hizo taarifa napata wapi? Kama wewe hukai goba unapata wapi taarifa? Tufanye mimi ni mwanachi wa kawaida kabisa mkereketwa nimeleta malalamiko nasema CARAVAT ZIWEKWE lasivyo wote mtafyekwa. Hatutaki janja janja. Tunataka barabara zitengenezwe


Huna uwezo wa kunifyeka kwa sababu ninawajua ujinga wenu huko Tegata A.

Na hiii taarifa umeileta hapa kwa sababu umetumwa kuja kuchafua watu kisiasa.

Bahati mbaya sana na wewe huelewi chochote.

Anyway, nimekusamehe!
 
Inaonekana hujui unachokiandika ama umetumiwa taarifa na wewe ukakurupuka kuileta hapa.

1. Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo/Wilaya ya Ubungo ina majimbo mawili ya uchaguzi ambayo ni Jimbo la Kibamba ambalo mbunge wake ni Issa Mtemvu, na Jimbo la Ubungo ambalo mbunge ni Kitila Mkumbo.

2. Jimbo la Kibamba lina kata 6 ambazo ni Kibamba, Mbezi, Msigani, Saranga, Kimara, Goba.

3. Ndani ya Kata ya Goba ndipo unapatikana Mtaa wa Tegeta A.

4. Kwa hiyo ni hivi Mtaa wa Tegeta A unapatikana ndani ya Jimbo la Kibamba, Tarafa ya Kibamba, Wilaya ya Ubungo, Dar es Salaam.

5. Kama nilivyosema: Tegeta A mna majungu sana. Sasa embu angalia; wewe hata mbunge wako humjui, hujui upo jimbo gani wala hujishughulishi kujua.

6. Maana yake hata kiasi cha pesa kilichotengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo huko hujui, na badala hata ya kuuliza unaleta taarifa humu ambayo hata wewe mwenyewe huielewi.

7. Ningekutajia kazi nilizofanya huko Tegeta A na mwaka ila kwa kuwa ninyi huko ni mabingwa wa kuzuriana sikwambii. Wala sina maslahi yeyote na mtu yeyote humo kwenu.

8. Barabara za huko zina changamoto kama maeneo mengine ya nchi.

9. Wilaya ya Ubungo inaongoza kwa kuwa na wahamiaji wengi sana kutoka maeneo mengine ya nchi, kwa hiyo hili linafanya huduma za huko kuzidiwa kwa kiasi kikubwa.

10. Hata hivyo, Halmashauri inajitahidi sana kuboresha huduma. Mfano Shule ya Msingi Tegeta A ni shule ya kwanza ya Msingi Tanzania kuwa na darasa maalum la masomo Digitali.

11. Ninapafahamu vizuri sana Tegeta A
Wewe umekazana kunirekebisha mbunge wangu sijui kata ngapi mbona unanikwepeshea mada. Jengeni barabara achaneni na miradi ya kijinga hiyo mnatutesa wananchi kwani mnashindwa kuweka bajaji na kutengeneza barabara ili wote tuwe salama?

Mimi nilikupa ushahidi mdogo tu kule juu. Naurudia tena hapa kwenye picha.
Kwamba mimi nimejaribu kujielewesha kwa postcode na inaonekana kabisa kwamba nipo jimbo gani.

Na mimi na deal na mwenyekiti wa serikali ya mtaa husika wewe hayo mengine ni ya kwako. Ni kama umepanic hivi. Anyways ujumbe umefika na barabara mtatengeneza tu. Tuko nje ya mda Mama samia njoo u deal na watu wako
IMG_6181.png
IMG_6179.png
IMG_6178.png
 
Huna uwezo wa kunifyeka kwa sababu ninawajua ujinga wenu huko Tegata A.

Na hiii taarifa umeileta hapa kwa sababu umetumwa kuja kuchafua watu kisiasa.

Bahati mbaya sana na wewe huelewi chochote.

Anyway, nimekusamehe!
Nitumwe na nani sasa? Yani mimi niache kuhangaikia familia yangu ipate chakula nikahangaike na mwenyekiti wa serikali ya mtaa? Sina mpango wa kugombea hata ujumbe wa nyumba kumi takataka tu. Mnakalia majungu na dhuluma nani anataka kazi za kurogana. Em tengenezeni barabara. Tunataka caravat njia inayotokea deez pub kuja catholic tegeta A, na njia inayotokea skymart supermakert kupita st yohanne health center. Wekeni caravat na ile njia inyooke ova.
 
1. Tegeta A ipo Jimbo la Kibamba na siyo Jimbo la Ubungo kwa hiyo Mbunge wa Ubungo hahusiki na eneo hilo.

2. Mimi ni dereva bajaji na ninamiliki bajaji. Katika udereva wangu nimegundua kwamba bajaji inahitaji njia nzuri kuliko vyomvo vingine vya moto ambavyo pia nimewahi kuviendesha. Kwa hiyo hoja kwamba Mwenyekiti wa Mtaa hataki kutengeneza barabara kwa sababu ya bajaji zake ni hoja dhaifu sana.

3. Nimewahi kuishi Tegeta A na nimefanya kazi kadhaa za CCM na Serikali huko: Mwenyekiti wa sasa ninamjua vizuri na namna anavyojitahidi kuleta maendeleo huko Tegeta A. Kwa hiyo ukiniambia anahujumu miradi mimi ninakataa.

4. Wakazi na wenyeji wa Tegeta A na mabingwa wa Majungu kwa viongozi wao. Hata Diwani wa hapo Mh. Ester anapigwa majungu eti kwamba kwa kuwa yeye ni wa Kinzudi basi maendeleo anapeleka kwake. Mara anaambiwa anataka kuanzisha kata nyingine ya Kinzudi kwa hiyo anawabagua Tegeta A.

5. Pamoja na hayo, Manispaa ya Ubungo imepokea pesa za Mradi wa DMDP kwa ajili ya miundombinu ya barabara kwa hiyo bila shaka zitafika huko.
Wenyekiti wengi wa serikali za mitaa hasa jimbo la kibamba wapo hivyo,hawataki kusikia kabisa swala la maendeleo ya mitaa yao,mimi natokea mtaa wa king'azi malamba mawili,mwenyekiti na mtendaji wake wapo hivyo,tena wananchi mkisema mjichangishe wenyewe wanakua wakali,issue ya maji walikua wanakwamisha maksudi ila wananchi wakapambana wenyewe at least shida ya maji kwa 40 imepungua king'azi,sasa hivi ni barabara,king'azi ina sehemu za machimbo ya mawe na mtoa kibali wa kuchimba mawe pale ni m/kiti wa mtaa wa king'azi,utakuta m/kiti wa mtaa wa kwembe,kifuru na maeneo mengine anawapa vibali wakachimbe mawe pale lakini mtaani kwake hataki kutoa mawe,ccm ni janga
 
Wewe umekazana kunirekebisha mbunge wangu sijui kata ngapi mbona unanikwepeshea mada. Jengeni barabara achaneni na miradi ya kijinga hiyo mnatutesa wananchi kwani mnashindwa kuweka bajaji na kutengeneza barabara ili wote tuwe salama?

Mimi nilikupa ushahidi mdogo tu kule juu. Naurudia tena hapa kwenye picha.
Kwamba mimi nimejaribu kujielewesha kwa postcode na inaonekana kabisa kwamba nipo jimbo gani.

Na mimi na deal na mwenyekiti wa serikali ya mtaa husika wewe hayo mengine ni ya kwako. Ni kama umepanic hivi. Anyways ujumbe umefika na barabara mtatengeneza tu. Tuko nje ya mda Mama samia njoo u deal na watu wako View attachment 2989319View attachment 2989320View attachment 2989321
Sasa kwenye hili gazeti lako umeelewa nini?
 
Wenyekiti wengi wa serikali za mitaa hasa jimbo la kibamba wapo hivyo,hawataki kusikia kabisa swala la maendeleo ya mitaa yao,mimi natokea mtaa wa king'azi malamba mawili,mwenyekiti na mtendaji wake wapo hivyo,tena wananchi mkisema mjichangishe wenyewe wanakua wakali,issue ya maji walikua wanakwamisha maksudi ila wananchi wakapambana wenyewe at least shida ya maji kwa 40 imepungua king'azi,sasa hivi ni barabara,king'azi ina sehemu za machimbo ya mawe na mtoa kibali wa kuchimba mawe pale ni m/kiti wa mtaa wa king'azi,utakuta m/kiti wa mtaa wa kwembe,kifuru na maeneo mengine anawapa vibali wakachimbe mawe pale lakini mtaani kwake hataki kutoa mawe,ccm ni janga
Mkuu mimi nakuelewa asilimia 💯 na ni wabishi sana hata ukiwafuata maofisini utazungushwa hawana msaada wowote na ukija kama hivi jamii forum kuliongelea wana panic balaa unamuona wakwangu kaja kujitetea huku anakazana kuniambia maswala ya mbunge sijui wa kibamba sijui ubungo takataka tu wanaacha kuwa rensponsible wanatupiana mipira.

Hawa dawa yao tunayo labda Watupigie wao kura. Wasipofuata matakwa yetu kwenye suala la maendeleo watamponza hadi Mama. Tumechoka
 
Sasa kwenye hili gazeti lako umeelewa nini?
Kaa kikao na watendaji wako mtutengenezee caravat lasivyo tusiwaone kwenye uchaguzi wa 2025 tutawafyekelea mbali. Sisi ndo wenye Goba tunaishi huku miaka zaidi ya 20 mje mtusumbue leo? Tumewavumilia tumechoka. Hizo route za barabara nilizozitaja zirekebishwe kusiwe na hayo makorongo.
 
Mkuu mimi nakuelewa asilimia 💯 na ni wabishi sana hata ukiwafuata maofisini utazungushwa hawana msaada wowote na ukija kama hivi jamii forum kuliongelea wana panic balaa unamuona wakwangu kaja kujitetea huku anakazana kuniambia maswala ya mbunge sijui wa kibamba sijui ubungo takataka tu wanaacha kuwa rensponsible wanatupiana mipira.

Hawa dawa yao tunayo labda Watupigie wao kura. Wasipofuata matakwa yetu kwenye suala la maendeleo watamponza hadi Mama. Tumechoka
Wapo hivyo hao shwain,watu mkiwa front ya kudai maendeleo ya mtaa wenu wanadai mna majungu,wote wapo hivyo,au watadai unataka kugombea nafasi zao chaguzi zijazo,huyo pimbi nilipoona aergument zake nikajua ndio walewale,mimi kwangu mtendaji alikuja kabisa kuuliza idhini ya kuvuta maji ya kutokea kibamba nimeipata wapi wakati kuna mradi wa mtaa wetu unaendelea kule hali ya hewa na utakamilika may 2023,hiyo ilikua 2022,nikamuambia akawaulize dawasa na fasta aondoke nyumnani la sivyo tutagawana nyumba za serikali,leo may 2024 huo mradi wao wa hali ya hewa huko sijui bado autoi maji hata chembe na kitu kizuri yale maji waliyokua hawayataki 50% ya watu wa king'azi wamevuta including m/kiti wa mtaa na mtendaji wake bila aibu na wenyewe wamevuta majumbani kwao
 
Back
Top Bottom