Mgagaa na Upwa
JF-Expert Member
- Sep 30, 2013
- 13,481
- 28,116
Chaguzi za serikali za mitaa ni mwaka huu oktobaKaa kikao na watendaji wako mtutengenezee caravat lasivyo tusiwaone kwenye uchaguzi wa 2025 tutawafyekelea mbali. Sisi ndo wenye Goba tunaishi huku miaka zaidi ya 20 mje mtusumbue leo? Tumewavumilia tumechoka. Hizo route za barabara nilizozitaja zirekebishwe kusiwe na hayo makorongo.
Tutabanana nao mwaka huu hadi kieleweke. Huyu wangu anajifanya mjuaji akae kwa kutulia uchaguzi wao wa serikali za mitaa mwaka huu lazima kichafuke na mwakani mbunge lazima ajipange. Watanyooshana wenyewe.Wapo hivyo hao shwain,watu mkiwa front ya kudai maendeleo ya mtaa wenu wanadai mna majungu,wote wapo hivyo,au watadai unataka kugombea nafasi zao chaguzi zijazo,huyo pimbi nilipoona aergument zake nikajua ndio walewale,mimi kwangu mtendaji alikuja kabisa kuuliza idhini ya kuvuta maji ya kutokea kibamba nimeipata wapi wakati kuna mradi wa mtaa wetu unaendelea kule hali ya hewa na utakamilika may 2023,hiyo ilikua 2022,nikamuambia akawaulize dawasa na fasta aondoke nyumnani la sivyo tutagawana nyumba za serikali,leo may 2024 huo mradi wao wa hali ya hewa huko sijui bado autoi maji hata chembe na kitu kizuri yale maji waliyokua hawayataki 50% ya watu wa king'azi wamevuta including m/kiti wa mtaa na mtendaji wake bila aibu na wenyewe wamevuta majumbani kwao
Mkuu mimi nakuelewa asilimia 💯 na ni wabishi sana hata ukiwafuata maofisini utazungushwa hawana msaada wowote na ukija kama hivi jamii forum kuliongelea wana panic balaa unamuona wakwangu kaja kujitetea huku anakazana kuniambia maswala ya mbunge sijui wa kibamba sijui ubungo takataka tu wanaacha kuwa rensponsible wanatupiana mipira.
Hawa dawa yao tunayo labda Watupigie wao kura. Wasipofuata matakwa yetu kwenye suala la maendeleo watamponza hadi Mama. Tumechoka
Sasa kama humjui mbunge wako, huyo mbunge unayetaka kunuwajibisha ni yupi?Tutabanana nao mwaka huu hadi kieleweke. Huyu wangu anajifanya mjuaji akae kwa kutulia uchaguzi wao wa serikali za mitaa mwaka huu lazima kichafuke na mwakani mbunge lazima ajipange. Watanyooshana wenyewe.
Andika yaliyo ya kweli na siyo majungu yako hayo.
Mwenyekiti wa Tegeta A ni kiongozi mzuri sana.
Pamoja na changamoto za kimiundombinu huko Tegeta A, lakini yule jamaa ni msikivu sana na anapambana.
Ninakumbuka zamani Tegeta A haikuwa na Kituo cha Polisi lakini sasa hivi kipo.
Pia usalama wa raia ulikuwa mdogo lakini sasa hivi kuna afadhali kubwa.
Angalau hizi changamoto zingeletwa na mtu anayeijua Tegeta A basi.
Sasa mleta taatifa mwenyewe ni Guantanamoh 😂😂
Wewe andika yote ila message sent and delivered. Tukutane october 2024 na waambie hao wenzio. Huto tuvyeo twenu hatusumbui mtu. Mi sina mda wa kukaa eti nigombanie uenyekiti wa serikali ya mtaa? Seriously? Muwe wajibikaji. Kumjua mbunge kunanisaidia nini kama hatatui matatizo ya eneo langu: MWENYEKITI WA SERIKALI YA MTAA WA GOBA TUMEKUJUA JIKESEHE UNAVYOJIKESHA ILA CARAVAT MTAWEKA NA MSIPOWEKA TUTAPELEKA USHAHIDI WA MRADI WENU WA BAJAJI KWA MAMA SAMIASasa kama humjui mbunge wako, huyo mbunge unayetaka kunuwajibisha ni yupi?
Bila shaka hata mwenyekiti wa Mtaa humjui. Unatia aibu!
Wewe andika yote ila message sent and delivered. Tukutane october 2024 na waambie hao wenzio. Huto tuvyeo twenu hatusumbui mtu. Mi sina mda wa kukaa eti nigombanie uenyekiti wa serikali ya mtaa? Seriously? Muwe wajibikaji. Kumjua mbunge kunanisaidia nini kama hatatui matatizo ya eneo langu: MWENYEKITI WA SERIKALI YA MTAA WA GOBA TUMEKUJUA JIKESEHE UNAVYOJIKESHA ILA CARAVAT MTAWEKA NA MSIPOWEKA TUTAPELEKA USHAHIDI WA MRADI WENU WA BAJAJI KWA MAMA SAMIA
😂😂😂😂WASWAHILI WANASEMA “UMEGUSA KWENYE MSHONO” au “UMEGONGELEA PALE PALE KWENYE MFUPA” unataka kuwapoteza watu maboya wanione mimi
Mbabaishaji😂 nimeweka hadi ramani waende wakaangalie hilo caravat. Wakawaulize na wakazi wa pale wawaambie majibu wanayopewa ofisini. Tutajua muongo nani acha panyeshe tujue panapo vuja.
Umekomalia kusema nimetumwa kukuchafua kisiasa. Mwenyekiti wa serikali ya mtaa? Seriously? Of all the positions nikahangaike na takataka? Mnajionaga nani? Au ni zile
Ela za sungusungu ndo zinazowazuzua. Hivyo viti vyenu hakuna anaevitaka except for inferior human beings. Niko very busy aisee kukaa nahangaika na nafasi yako.
Eti mradi wa bajaji😂 yani tushindwe kupita barabarani kisa bajaji zako! Tengeneza barabara ongeza bajaji hata mia utapata wateja wengi tu ila msitupotezee muda wa kutengeneza zile barabara ni haki yetu!
Hali hiyo una bajaji unapumulia utosi ungekua na mabasi si tungehama hata hiyo
Goba yenyewe.
Tujikite kwenye hoja. CARAVAT GOBA KULANGWA/TEGETA A. I am out
Mitano tena kwa Mama
Kwani ni nani kakataa?Chaguzi za serikali za mitaa ni mwaka huu oktoba
Halafu wewe😂Pole sana,unakopeleka malalamiko hawana habari na wewe,mama anaupiga mwingi mitano tena
Bora umueleze mkuu. Hawa watu hawajui majukumu ya viongozi. Kila kiongozi anawafanya sehemu yake na akishamaliza inakuwa basi ni kusubiri.Mnawaonea tu.. wenyeviti hao hawana mishahara wanategemea hela za ninyi mnpoaenda kuandikiwa barua zenu .. wakati ndiye wafu muhimu kwenye mtaa
Wewe ndiye mjinga kwa sababu hujui unabishana na nani, na hujui unabishania nini; una upeo finyu kiasi kwamba hujui hata Wilaya yako ni ipi!Msijitetee bila sababu za msingi. Nyinyi mna uwezo wa kutoa vibali watu wajitengenezee barabara kwa juhudi zao lakini mnawakwamisha ili miradi yenu isife. Huo ni ujinga
Matatizo hayo ya barabara kwenye eneo hilo analolalamika mdau ni kweli yapo?Wewe ndiye mjinga kwa sababu hujui unabishana na nani, na hujui unabishania nini; una upeo finyu kiasi kwamba hujui hata Wilaya yako ni ipi!
Matatizo yapo ila namna anavyoyaeleza siyo sahihi.Matatizo hayo ya barabara kwenye eneo hilo analolalamika mdau ni kweli yapo?
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimekuelewa mkuu, asubuhi njema.Matatizo yapo ila namna anavyoyaeleza siyo sahihi.
Kwanza hajui eneo husika lipo Wilaya gani.
Anasema sababu ya ubovu wa barabara ni mradi wa babaji wa viongozi ambao wanataka barabara iwe mbovu ili daladala zisipite na bajaji zipate abiria.
Pia anadai mimi ni kiongozi wa huko.
Mimi kama mwenyeji wa huko, pia ni mtaalamu na biashara ya bajaji ninapingana na anayoyaeleza kwa maana kwamba si kweli kwamba bajaji inahitaji barabara mbovu.
Pia mimi siyo kiongozi wa huko na wala sina maslahi yeyote kwenye siasa za Tegeta A, japo ninapajua vizuri.
Nimemjaza na yeye kajaa!
Sasa Mbezi Msumi kuna issue kama hiyo hiyo. 👍Nawasalimu kwa Jina la Jamhuri. Kazi iendelee.
Mama Samia, wakazi na wapiga kura wako wa GOBA Njia ya Tegeta A kuelekea madawa na njia ya Tegeta A kuelekea kulangwa kupitia makanisa ya Katoliki Tegeta A, na Anglikana Tegeta A tuna changamoto kubwa sana ya barabara haitaki kutatuliwa kwa miaka mingi sasa.
Ile njia ni mbovu sana na wakazi wa maeneo hayo waliwahi kumfuata MWENYEKITI WA SERIKALI YA MTAA Kumwomba awasadie kupambania kibali cha kurekebisha barabara walichojibiwa na serikali ya mtaa ni hivi: “HIYO SIYO KAZI YENU”
Ikaja kugundulika kwamba ile njia inamwingizia faida kubwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa GOBA TEGETA A kwasababu ana mradi wake wa Bajaji. So anajua akikubali barabara itengenezwe itafanya madaladala yapite kule na yeye atapoteza mradi wake wa Bajaji.
Wakazi wa Tegeta A na kulangwa tunahitaji caravat kwenye makazi yetu. Mbunge na diwani wamenyamaza labda tukikuomba wewe mama utawakumbusha wajibu wao.
Tunateseka na hiki kipindi cha mvua school bus zinapita na watoto wetu ni hatari sana sehemu zingine caravat zimebomoka kabisa mfano hii njia karibu na kituo cha afya cha mtakatifu Yohanne goba kulangwa njia ni mbovu sana na viongozi wa serikali za mtaa hawataki kutengeneza hiyo njia kwa sababu wanajua watakosa mapato ya miradi yao ya bajaji na pikipiki.
Mama samia tunaomba msaada wa njia hizo kurekebishwa tuwekewe caravat tukiwafuata viongozi wa serikali za mtaa hawatoi ushirikiano kwasababu hawataki kupoteza mapato yao ya Bajaji na bodaboda.
Nimeambatanisha ramani ya Goba Kulangwa inayopakana na Tegeta A ambayo inaenda kutokea st yohane health center kwenda kwenye makazi.
Viongozi, hapo nlipoweka alama nyekundu kuna mto unapita, caravat limebomoka upande na njia ni mbovu hata mkienda sasa hivi mtaona na school bus za watoto wetu zinapita hapo kila siku na watoto. Tunaogopa watoto wasije kusombwa na maji tunaomba serikali kuu itusaidie kama serikali tunazoishi nazo mtaani hazina msaada. TUNAOMBA CARAVAT ENEO HILO. Na tunaomba hizo njia zirekebishwe kwasababu zimechimbika sana kwasababu ya mvua.
View attachment 2989251
Cc Mbunge wa Ubungo, Diwani wa Goba kulangwa, serikali ya mtaa goba kulangwa na tegeta A.
Nawasilisha