Wake wa Marais wetu na Mambo yao

Wake wa Marais wetu na Mambo yao

Mwandishi Wetu
Daily News; Thursday,July 17, 2008 @19:01


Kampuni ya Huduma za Fedha ya Bayport iliyolalamikiwa bungeni majuzi kuwa inawatoza walimu riba kubwa baada ya kuwakopesha, imesema mke wa Rais mstaafu Benjamin Mkapa, Anna, ni mmoja wa wakurugenzi wake, lakini hana hisa binafsi anazomiliki kwenye kampuni hiyo.

Mtendaji Mkuu wa Bayport, Etienne Coetzer, alisema katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyosambazwa Dar es Salaam leo kuwa Anna Mkapa anawakilisha taasisi ya Fursa Sawa kwa Wote (EOTF) ambayo inamiliki asilimia moja ya hisa za kampuni hiyo.

Kampuni hiyo pia imesema Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Ibrahim Kaduma ni mmoja wa wakurugenzi kupitia kampuni ya Uwekezaji ya Taifa (NICOL) ambayo nayo inamiliki sehemu ya hisa katika Bayport. Haikuelezwa kiasi cha hisa zinazomilikiwa na NICOL.

“Mama Mkapa na Kaduma wameteuliwa na taasisi hizo mbili kuziwakilisha kwenye bodi ya wakurugenzi ya Bayport,” ilifafanua taarifa hiyo. Bayport imetoa ufafanuzi huo baada ya Mbunge wa Mbozi Mashariki Godfrey Zambi (CCM) kutoa tuhuma nzito bungeni na kukaririwa na magazeti kadhaa leo, kwamba watu hao wawili kuwa wanamiliki kampuni ya Bayport ambayo alidai inawaibia walimu kwa kuwatoza riba ya juu.

Mbunge huyo alifafanua kuwa kampuni hiyo imekuwa inawakopesha walimu lakini inawatoza riba kubwa inayofikia asilimia kati ya 167 na 200. Alitoa mfano kuwa mwalimu anayekopa Sh milioni moja amejikuta analipa Sh milioni 3, jambo alilodai ni wizi kwa watumishi hao wenye kipato kidogo.

Wakati Zambi anawasilisha hoja yake bungeni, hakuwasilisha nyaraka zozote zinazothibitisha kuwa Anna Mkapa na Kaduma ni wamiliki wa Bayport. Lakini hata hivyo Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Jumanne Maghembe alimwahidi kuwa atafuatilia malalamiko hayo ya walimu.

Taarifa ya leo ya Bayport imewataja wanahisa wengine mbali na EOTF na NICOL kuwa ni Africa Yetu na Bayport Management Ltd. Kaduma ambaye ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe ni mwanahisa katika kampuni ya NICOL na Anna Mkapa ni Mwenyekiti wa EOTF.

Kuhusu riba, kampuni hiyo ilisema inatoza riba inayotokana na gharama halisi za mkopo. “Bayport inatoza riba yenye ushindani katika sekta ya masoko na siyo kwamba sisi riba yetu ni ya juu.” Hata hivyo haikutaja kiasi cha riba inayotozwa. Coetzer alisema kampuni imeshtushwa na habari za Mbunge huyo alizozitoa, wakati Bunge limekaa kama kamati ya matumizi na akihitaji ufafanuzi kutoka kwa waziri sababu ya kampuni hiyo kutoza riba kubwa kiasi hicho.

Tujadilini sasa ama nayo hii ni Spin ama sisi tunakurupuka ama tunafuata upepo?
 
DAILY NEWS Reporter
Daily News; Friday,July 18, 2008 @00:02

Former first lady mama Anna Mkapa does not hold shares in Bayport Financial Services as has been alleged by an MP for Mbozi East, Godfrey Zambi. Some local newspapers quoted the MP as alleging that Mama Mkapa and Mr Ibrahim Kaduma, the Chancellor of Mzumbe University, own the firm that lends money to teachers at exorbitant interest rates.

Bayport Financial Services CEO Etiene Coetzer issued a press statement saying that the duo do not hold any shares in the financial institution but are just board members. Mr Coetzer however said EOTF, which is headed by Mama Mkapa, holds one per cent of the allocated shares and NICOL, which is apparently run by Mr. Kaduma, is a shareholder.

“It is through EOTF and NICOL equity participation in Bayport Financial Services that Mama Mkapa and Mr Kaduma have been nominated by the two institutions to represent them, respectively in the Board of Directors,” Mr Coetzer said in the statement. He also defended interest rates they charge of the loaned money, saying they were not the most expensive. Mr Zambi charged in the Parliament that the firm was reaping off poor teachers by charging them exorbitant interests on the loans advanced.
 
Zambi Ni Mbunge Mpya Ila Sasa Ameingia Ktk Vita Ambayo Nadhani Haifahamu Kabisa. Kuna Siku Nilikaa Naye , Nadhani Aliamini Kuwa Angelikuwa Ni Mmoja Wa Wateule Wa Mkuu Maana Alikuwa Analalama Na Kuponda.

Ninamuonea Huruma Kwani Hizi Hoja Anazokomaa Nazo Wakati Hajishughulishi Na Kusaka Ushahidi Wa Kutosha Kabla Kwenda Ktk Public Zinawafanya Adui Zake Huko Mbozi Wajindae Kumng'oa 2010 Kwa Msaada Wa Haohao Anaowakomalia Kwa Kubahatisha Ktk Hoja.
 
wabunge wetu jamani wengine hawana utafiti. bayport BOT wamewaruhusu wachaji riba KUBWA kwani mazingira ya ukopaji bongo bado hayajawekwa kumsaidia mwananchi.

nachojua mama mkapa kupitia eotf ana hisa hapo ila hapangi riba.
vipi benki yetu CRDB tunayoimiliki kwa asilimia zaidi ya 70 wako vipi kwa riba na huduma za mikopo kwa ujumla.
naomba TUJADILI..
 
Sidhani kama kuna mtu anayewashikia bastola hawa walimu ili wasaini fomu za kuchukua hiyo mikopo, tujenge utamaduni wa kuheshimu mikataba tunayoingia. Cha msingi ni hawa walimu kuelewa kwa undani terms and conditions za mkopo kabla hawajasaini. Katika kipindi hiki cha ushindani mkali wa biashara ni vyema tukaacha market forces zifanye kazi.
 
wabunge wetu jamani wengine hawana utafiti. bayport BOT wamewaruhusu wachaji riba KUBWA kwani mazingira ya ukopaji bongo bado hayajawekwa kumsaidia mwananchi.

nachojua mama mkapa kupitia eotf ana hisa hapo ila hapangi riba.
vipi benki yetu CRDB tunayoimiliki kwa asilimia zaidi ya 70 wako vipi kwa riba na huduma za mikopo kwa ujumla.
naomba TUJADILI..


Nyauba,

Hii thread haina uhusiano na CRDB. Halafu swala la anna na kaduma bado halieleweki. Tunahitaji kuchimba zaidi ili tuje na data kwa vile mbunge hajatoa vielelezo na wamiliki hawawezi kusema maneno ya kuwakaanga wenyewe.
 
Vielelezo vipo, na huenda vikatolewa bungeni wakati wowote kama wahusika watakua hai. Si lazima Zambi ndiye awasilishe, maana walimu wamechachamaa sana
 
Haya ninyi msiotaka kuwaacha wastaafu wetu wapumzike salama. kwa taarifa yenu Mr& Mrs Clean kwa sasa ni wajasiriamali. Je Mna wivu nao??? nanyi kuweni wajasiriamali.
 
Vielelezo vipo, na huenda vikatolewa bungeni wakati wowote kama wahusika watakua hai. Si lazima Zambi ndiye awasilishe, maana walimu wamechachamaa sana


Hao walimu
wawakilishe vielelezo ambavyo vinaonyesha amabavyo waliposaini riba ilikua tofauti na jinsi walivyokatwa malipo.Hapo ita make sense.
 
Kampuni inayohusishwa na Mama Mkapa yabanwa

na Tamali Vullu, Dodoma
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MBUNGE wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi, amezidi kuibana kampuni ya mikopo inayohusishwa na Mama Anna Mkapa, mke wa Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa.

Katika hatua nyingine, mbunge huyo jana alionyesha vielelezo kuhusu kile anachokieleza kuwa ni utapeli unaodaiwa kufanywa kupitia kampuni ya Bayport Financial Services.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Zambi alisema alipoibua suala hilo bungeni, haikuwa nia yake kutuhumu tu, bali kueleza ukweli aliotumwa na watu wake.

“Wabunge wanaposema mambo bungeni wanakuwa wametumwa na wananchi. Mimi haikuwa nia yangu kumshutumu mtu yeyote bungeni, bali kueleza ukweli kuhusu utapeli unaofanywa na kampuni hiyo,” alisema.

Alisema katika kamati ya matumizi, mbunge anapewa muda mfupi, hivyo alishindwa kutoa vielelezo hivyo ingawa alikuwa navyo.

Zambi alisema baada ya kuibua suala hilo na kueleza kuwa riba hiyo ni asilimia 200, waathirika hao (walimu) walimpigia simu na kumweleza kuwa riba ya asilimia 200 aliyotaja ni ndogo.

Aidha, alisema kampuni hiyo ilipokwenda kwa walimu hao kujinadi, iliwadanganya kuwa itawalipia madeni mengine waliyo nayo, ili waweze kuchukua mikopo katika kampuni hiyo.

Hata hivyo, mbunge huyo aliilaumu Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa kushindwa kudhibiti viwango vya riba na kusababisha wananchi kuendelea kuumia.

Pia alisema Mama Mkapa anahusishwa na kampuni hiyo kupitia Taasisi ya Fursa Sawa kwa Wote (EOTF), ambayo ina hisa katika kampuni hiyo na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Ibrahim Kaduma, kupitia Kampuni ya Uwekezaji ya Taifa (NICOL). Kaduma ni mmoja wa wakurugenzi.

Mbunge huyo alionyesha vielelezo mbalimbali kuhusiana na suala hilo ikiwamo barua ya Shule ya Sekondari Mbeya kwenda kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, ikitaka kusitisha makato ya mkopo wa fedha kutoka kampuni ya Bayport.

Katika barua hiyo ya Mei 8, mwaka huu, shule hiyo imeeleza kuwa hali hiyo inatokana na udanganyifu na utapeli uliofanywa na taasisi hiyo ya fedha.

“…Tunaomba kusitisha makato mpaka tutakapokubaliana na kampuni hiyo kwa sababu imebadili mkataba kutoka miezi 12 mpaka miezi 36.

“Tulikopa fedha ya kulipa ndani ya miezi 12, lakini Bayport wameongeza miezi 24 ambayo ni mikopo hewa. Marejesho yalianza kukatwa kabla ya nakala ya mkataba kurejeshwa kwa waliokopa baada kupitishwa na mkuu wa kituo cha kazi pamoja mwajiri,” alieleza sehemu ya barua hiyo.

Pamoja na barua hiyo, walimu hao waliambatanisha majina 16 ya walioathirika na suala hilo na viwango vya makato.

Walimu hao ni Idde Mwanjute aliyekopa sh 1,115,000. Alitakiwa kulipa sh 3,536,159; Mdewa Fungo alikopa sh 800,000 (kulipa sh 2,680,625); Yustus Mwalyambi alikopa sh 250,000 (kulipa sh 837,159); Eliza Mpesya alikopa 535,000 (kulipa 1,792,686); Nelusigwe Kajuni alikopa 600,000 (kulipa 2,010,489).

Wengine ni Thabita Mhagama aliyekopa sh 1,780,000 (kulipa sh 5,964,451); Antonia Kileo aliyekopa sh 405,000 (kulipa sh 1,357,080); Hastings Alamu aliyekopa sh 1,085,000 (kulipa 3,635,634); Sicknesye Sanga aliyekopa 310,000 (kulipa sh 1,038,752); na Reuben Kaminyoge sh 690,000 (kulipa sh 2,312,062).

Wako wengi. Elisala Mina alikopa sh 525,00 (kulipa sh 1,759,178); Lucy Liwungo alikopa sh 1,000,000 (kulipa sh 3,350,815); Redempta Mlingi alikopa sh 710,00 (kulipa sh 2,379,078); Elizabeth Mhilwa alikopa sh 1,000,000 (kulipa sh3,350,815); Benedicta Kagoro alikopa sh 1,000,000 (kulipa sh 3,350,815).

Vielelezo vingine ni barua kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kwenda kwa wakurugenzi watendaji wa Halmashauri na Mkurugenzi wa Jiji wa Mkoa wa Mbeya, kuonyesha kukubali kuanzishwa kwa kampuni ya Bayport Finacial Services na Platinum Credit Limited.

Katika barua hiyo ya Januari 16, mwaka huu, iliyosainiwa kwa niaba yake na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya, Ndewa, J.L, imewaomba viongozi hao kuzikubalia kampuni hizo kufanya huduma hiyo katika ofisi zao.

Pia mbunge huyo alionyesha barua kutoka Ofisi ya Rais (Ikulu) ya Julai 11, 2006, iliyoeleza kuikubalia kampuni kutoa huduma hiyo kwa wafanyakazi wake, lakini ilikataa kuidhamini kampuni hiyo.

Kielelezo kingine ni muhtasari wa kikao cha walimu waathirika wa Bayport na mwakilishi wa kampuni hiyo aliyetajwa kwa jina moja la Gama, kilichofanyika Aprili 3, mwaka huu.

Katika kikao hicho, Gama alikiri kupata malalamiko ya walimu hao na kueleza kwamba mawakala waliotumwa walikuwa wamewapotosha wateja.

Pia Gama alikaririwa akisema kuwa kampuni hipo ipo tayari kumsikiliza mteja atakayeamua kurejesha mkopo na kuongeza kwamba kampuni hiyi ipo tayari kumuongezea mteja fedha kwa mkataba wa awali au kupunguza makato.

Katika kikao hicho, walimu hao na mwakilishi huyo wa Bayport walikubaliana kampuni hiyo itapokea na kusikiliza malalamiko ya kila muathirika (mwalimu), ili kufikia ufumbuzi.

Pia walikubaliana kufikia Aprili 12, mwaka huu, nakala za fomu za mikataba ziwe zimewasilishwa Ofisi ya Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Wilaya ya Mbozi, na kwamba walimu waliotaka kurudisha fedha, ili kufuta mkataba wakubaliwe bila kikwazo.

Kampuni hiyo juzi ilitoa taarifa kwa vyombo vya habari na kueleza kuwa Anna Mkapa hana hisa binafsi anazomiliki kwenye kampuni hiyo.

Kampuni hiyo ilieleza Anna Mkapa na Kaduma wameteuliwa na taasisi hizo kuziwakilisha kwenye Bodi ya Wakurugenzi ya Bayport.

Bayport iliwataja wanahisa wengine kuwa ni Afrika Yetu na Bayport Management Ltd.

Kuhusu riba, kampuni hiyo imeeleza kuwa inatoza riba inayotokana na gharama halisi za mkopo na kuongeza kuwa riba hiyo ni ya ushindani katika sekta ya masoko, lakini haikutaja kiasi cha riba.

Jumanne wiki hii, Zambi aliibua tuhuma hizo bungeni na kusema watu hao wanamiliki kampuni hiyo ambayo imekuwa ikiwatapeli walimu na watumishi wengine wa halmashauri za wilaya, kwa kuwakopesha kwa riba kubwa.

Akijibu hilo, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Jumanne Maghembe, aliahidi kulifuatilia suala hilo.
 
mh kila anapogusa huyu mama lazima aibue kilio..zama za unyonyaji zimerudi kwa style yake ukope laki tatu ulipe milioni.
 
Haya ninyi msiotaka kuwaacha wastaafu wetu wapumzike salama. kwa taarifa yenu Mr& Mrs Clean kwa sasa ni wajasiriamali. Je Mna wivu nao??? nanyi kuweni wajasiriamali.

Wao walie tu. Mama lao Anna ni mjasiriamali kama kawaida ya asili yetu. Sijui wangefurahi kama angetoka ikulu na umasikini wake alioingia nao!???? Loh..mwacheni mama yetu apumzike na ale pensioni yake safi baada ya kazi ngumu aliyoifanya ikulu. Au munamuonea wivu kumiliki hiyo EOTF?.
 
Lakini tujiulize hawa watumishi mbona hawaishi kukopakopa, je hizi fedha wanafanyia nini hasa wanapopewa? nikiwango gani hicho kinachokopwa na watumishi wengi zaidi? kwa kutizama hizi data za mbunge wengi hukopa kati ya 250,000/= hadi 3,500,000/=.

Kwa mtizamo wangu hizi fedha hutumika kulipa ada za shule za watoto wao, kumalizia nyumba za kuishi, na kuanzishia miradi midogo kama maduka ya nguo na biashara ya taxi.

Kwa mtizamo wangu mashirika kama nssf badala ya kujiingiza kwenye biashara kubwa kama ujenzi wa madaraja wangeanzisha "law cost housing scheme" na "school fees beneficiary schemes"

hebu tujiulize ilikuwaje mwingereza akaanzisha mradi wa "magomeni kota" lengo lilikuwa nini? halafu sivibaya tukaiga na tukaborasha mawazo hayo!

Pia ningewashauri viongozi wastaafu wasitumike kama "deal makers" kufanya hivyo kutapunguza heshma zao katika jamii! itakuwaje kama gen.mboma ataanza ku-supply nyama jeshini, kila mtu atasema sio bure kuna jambo!
 
Ufisadi haukutosha kuwapa fedha za kutosha? ni mpaka tena wawanyonye waalimu jamani? Mgodi wa kiwira mbona uanwapa pesa nyingi ? ulafi huu ndio utawaangamiza kabisa .

Hivi ule mfuko wa EOTF ni wa kwake binafsi ama nao kaupora tuu?
 
nasubiri kuona majibu ya bayport kama wanalo la kujibu!
 

Katika kikao hicho, Gama alikiri kupata malalamiko ya walimu hao na kueleza kwamba mawakala waliotumwa walikuwa wamewapotosha wateja.

Kama hii ni kweli this is fraud and deception, sasa sijui polisi wanafanya kazi gani kama hadi sasa hao mawakala hawajakamatwa.
 
Huu ni mfano bora sana kuonyesha jinsi NJAA inavyoweza kuondoa UTU wa mtu hasa maskini mkopaji..NJAA inaweza kabisa kumfanya mtu auze organs zake acha mbali utu na ndio maana nasema hadi hapo wananchi watakapoweza kujenga fikra za Umaskini jeuri kichwani mwao ndipo tunaweza kupiga hatua ktk vita hivi against UFISADI..

Katika hili Mama Mkapa hana kosa kabisa!.. Haya ni makubaliano yaliyofanywa kati ya wahusika na ikiwa mhusika umeambiwa mapema kwa kauli ama kimaandishi kwamba Ukikopa millioni 1 unatakiwa kurudisha millioni 3 ktk muda wa miezi kadhaa, Ukakubali na kuweka sahihi kukubali masharti hayo magumu basi hakuna sheria ya kumfunga mtoa mkopo.
Kilichotokea hapa ni sawa kabisa na mikopo ambayo nchi yetu imejiingiza na WB ambapo haiwezekani kabisa kulipwa kwa biashara zetu. Tumejifunga wenyewe ktk mikopo hiyo hivyo kuilalamikia BVenki kuu ya Dunia ama IMF ni ujuha wetu wenyewe na hakuna mahakama inayoweza kutusaidia sisi isipokuwa wadhamini wa mikopo hiyo ambao hutufunga tena ktk mikataba mingine mizito ili kupata misamaha ya kodi.. Hata tunaposamehewa huwa tayari tumekwisha lipa RIBA inayozidi kiwango cha awali cha Mkopo kwa hiyo msifikirie kwamba Tanzania inaposamehewa madeni ina maana hatukulipa kitu chochote.. tumelipa sana tena zaidi ya fedha za mkopo lakini kiwango hicho huhesabika kama RIBA tu...Deni huwa limesimama pale pale!..

Ni makubaliano na ndio maana sisi Waislaam tunalaani RIBA...Ni Ukiukaji kama huu na tamaaa za Utajiri kama hizi toka pande mbili unaotengua RIBA na kuwa Haramu...
Hawa walimu ujinga wao wenyewe hasa kutokana na ile dhana kwamba akikopa millioni anaweza kuizalisha within miaka miwili akizitumia fedha hizo kufungua shule ya jioni....
Kifupi mtrindo huu unaondoa kabisa thamani ya Elimu mashuleni mwetu ni Utaratibu unaoponza Ufundishaji wa watoto wetu kwa sababu walimu wanakuwa wakitazama zaidi maslahi yao nje ya ajira waliyopewa na serikali...Hii inatokea hata ktk Hospital na Zahanati zetu ni mfumo mbaya kabisa wa ufanisi ktk utoaji huduma...
 
Kwani kwenda kukopa hao watu walifungwa pingu na kuvutwa ili wakachukue hiyo mikopo?..............aagghh kulia lia kwingine bwana........this is disgusting!!........yaani wewe Mbunge unakuja kupiga kelele after the fact........shame on you.

........Nilitegemea wewe kama Mbunge..........kuwa ungewaonya wanajimbo lako kuwa waangalifu na mikataba ya kinyonyaji
 
Back
Top Bottom