Wake wa Marais wetu na Mambo yao

jamni mmesoma mtanzania leo? aliyemsaidia ana mkapa kudhulumu wafanyakazi wa serikali nyumba hizi, ni mramba wakati akiwa mkuu wa mkoa wa mbeya.
 
Shukran Mwikimbi
 
Last edited:
jamni mmesoma mtanzania leo? aliyemsaidia ana mkapa kudhulumu wafanyakazi wa serikali nyumba hizi, ni mramba wakati akiwa mkuu wa mkoa wa mbeya.

MRAMBA ni kiboko nafikiri anatakiwa kuwekwa katika historia ya nchi yetu.
 

huyo mwanasheria ni CHENGE nini
 


nao wanaosafirisha watu kubeba unga wana mkosa yao pia ambayo hayahalalishi wizi wa mrs
 
Ufisadi haukutosha kuwapa fedha za kutosha? ni mpaka tena wawanyonye waalimu jamani? Mgodi wa kiwira mbona uanwapa pesa nyingi ? ulafi huu ndio utawaangamiza kabisa .

Hivi ule mfuko wa EOTF ni wa kwake binafsi ama nao kaupora tuu?


Mpaka kieleweke, kama ulikuwa hujui ngoja nikupe ukweli. Mfuko wa EOTF ni mali halali ya mama Anna Mkapa. Hata kama ilianzishwa ikulu na ikapata wafadhili wa ndani na nje kwa msaada wa serikali na bunge lenu la wabunge makanjanja lakini Anna aliianzisha kwa mtaji wake mwenyewe. Kumbuka mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe. Anna aliweka nguvu zake mwenyewe kuipata EOTF.

EOTF ni mali halali ya Anna Mkapa kama ilivyo WAMA ambayo ni mali halali ya mama Salma Kikwete. Nyie mlie tu, hapa hanyang'anywi mtu. Jiandaeni kushuhudia mama Salma Kikwete akiondoka na WAMA yake.
 

Kama mifuko hii ni MALI yao; kwa nini wanasubiri waume zao waingie IKULU yetu ndipo waianzishe?
 

Mkuu,
Kwanza kabisa nitumie fursa hii kukukaribisha hapa kijiweni.Karibu tufanye mageuzi ya kweli kwenye taifa hili lililopoteza dira.wewe una wajibu mkubwa kabisa katika kuwa wakala wa mabadiliko ya kweli.


Btn: mbona hii taasisi alikua anafanya nayo kazi as if ni public institution? Nguvu za kumtetea hapa sijui unazioa wapi mkuu? Labda kuna jipya ambalo hatulijui? Basi hebu rudi basi kwa hisani yako utueleweshe.
 
Kama mifuko hii ni MALI yao; kwa nini wanasubiri waume zao waingie IKULU yetu ndipo waianzishe?


Ikulu ndiko mitaji inakopatikana kwa urahisi. Mbona watu wengi wamepata mitaji kupitia mashirika ya umma lakini hamuwasakami kama mama???? Mama kawatumikia miaka kumi bila mshahara. Sasa kumbe mlitegemea yeye aishije??? Mlitegemea mama akale polisi???
 

Kwani KAACHIKA? Ikulu yenye mitaji ni hii ya Watanzania? Mwalimu asitusikie huko alikotangulia.
 
MRAMBa na mkuu wa wilaya wa wakati huo mbeya, walimlazimisha aliyekuwa municipal director wilson kabwe kutoa letter of offer kwa mama ana mkapa na baadaye kumlikisha eneo lenye nyumba za serikali.

waliouziwa nyumba hizo ni pamoja na mhandisi wa sekretariat ya mkoa. hadi leo wamekwama kupata hati hali wakiwa wamelipa
 
Date::7/23/2008
Walimu wajutia kilichowapeleka kukopa Bayport
Na Tausi Mbowe
Mwananchi

BAADHI ya walimu wamejitokeza hadharani na kudai Kampuni ya Bayport Financial Services, ambayo mke wa Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Anna ana hisa imekuwa ikikata zaidi ya mara tatu mkopo waliyochukua.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Mwalimu wa Shule ya Msingi Hekima zamani Buguruni B, Scolastica Kaduma, alisema kampuni hiyo imekuwa ikiwanyonya bila huruma kutokana na kulipa kiwango kikubwa cha deni halisi ikilinganisha na benki nyingine ambako baadhi yao wamechukua mkopo.

Kaduma alitoa mfano wake kwamba Aprili mwaka jana alikopa Sh470,000 kutoka Bayport, lakini anaendelea kukatwa Sh43,747.75 kila mwezi kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa na bado anadaiwa Sh1.1 milioni.

"Mpaka sasa nimeshalipa zaidi ya Sh437,000 katika kipindi cha mwaka mmoja, lakini bado karatasi yangu ya malipo inaonyesha nina deni la Sh1,049,922," alisema huku akionyesha karatasi hiyo.

Kwa mujibu wa hesabu ambazo Mwananchi ilifanya, zinaonyesha walimu hao wanalipa riba ya asilimi 6.53 kwa mwezi sawa na asilimi 78.36 kwa mwaka.

Hesabu hiyo inafanya walimu hao kulipia zaidi ya mara tatu ya kiwango halisi cha mkopo.

Kwa mujibu wa mchanganuo ambao Mwananchi imefanya, inaonyesha katika mkopo huo mwalimu huyo analipa Sh13,055.55 kama makato ya kila mwezi sanjaro na riba ya Sh30,691.20 kwa mwezi na kufikia Sh43,746.75.

Wakati zikiibuliwa tuhuma hizo dhidi ya Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na mkewe Anna, bado kuna tuhuma lukuki ambazo hazijatolewa maelezo zinazowahusu kwamba walijihusisha na biashara wakiwa Ikulu.
 
Wana ndugu hili jambo nafikiri inatukumbusha ule uzama wa ufalme hivi sasa kila sehemu ya zanzibar utokosa jina la karume mwishoni...sasa naona na hawa walio uongozini wameamua kula kivyao....pale forodhan tulipokuwa tukiingia na kutafuta samaki wa pweza ukiwa na mkeo...leo hii kumefungwa wanaakarabati na habari za uhakika ni kwamba mke wa RAIS wa ZANZIBAR mama shadya karume katunukiwa kipande ile...kwa hiyo wale ndeugu zzetu waliotoka bara kuja zanzibar kuuza pweza ni wakati wa kurudi kwao mbagala kuangalia kama wnaweza pata mafao ya nyumba zao walizokimbia.....sioni mantiki ya kugawa hizi nchi kwa kisingizio cha me wa rais...jamani mama mkapa bado kidogo atuache UC*** WA MNYAMA KILA SEHEMU YAKE MPAKA MAJUZI KAJIFANYA KUMUUZIA MTU LILE HOTEL LAKE KUBADILI NA JINA KUMBE FIX...MAMA SALMA NAE ALTHOUGH AJATOKA RASMI NATUMAINI NNDANI YA MIAKA 5 NA WAMA YAKE LAZIMA WAMTAMBUE...HAYA WA MADHABAHUNI ALI MADHABAHUNI
 
Jamani wake za marais mtatumaliza watoto wetu watokaje???????????
 
We Mr.Impossible vp?
Hujuwi kuwa sehemu ile ni ya marehemu Ba Mkwe?
 
....pale forodhan tulipokuwa tukiingia ...leo hii kumefungwa... ni kwamba mke wa RAIS wa ZANZIBAR mama shadya karume katunukiwa kipande ile...kwa hiyo wale ndeugu zzetu waliotoka bara kuja zanzibar kuuza pweza ni wakati wa kurudi kwao...
Duh! Hivi wauza pweza na ngisi pale forodhani ni wabara... eh!?
 
Viongozi wetu wanapaswa kujua kwamba wakipata public offices siyo sehemu za ku -accumulate wealth na kujipendelea.
Huyu Mama Shadya na kupewa hiyo Forodhani amepewa kwa sababu zipi hasa?kama siyo sababu za kimaendeleo wala kuwanuafaisha watu wa sehemu husika basi it does not justify hicho kitendo chao cha kifisadi!
 
Huo ni ufisadi ,huo ni ufisadi, huo ni ufisadi.
 
Mr.Impossible ule ukarabati pale forodhani unagaramiwa na nani? Mama Shadya au SMZ?
 
hasara loo mtu mzima kuvamia mambo ya udaku na kuanza kulaumu kwanza fuatilia upashwe na ndio unene sio upayukwe utadhani umepandwa na kibuki

pole mradi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…