Wakenya ni watu wenye roho nzuri sana

Wakenya ni watu wenye roho nzuri sana

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Ingawa wakati mwingine Watanzania na Wakenya hushambuliana kwenye mitandao ya kijamii, haimaanishi kuwa ni maadui. Utani wao ni kama ugomvi wa watoto wanaofuatana kuzaliwa.

Linapokuja suala la shida au changamoto, uhalisia wa mahusiano yao hujithihirisha. Husaidiana.

Ingawa Watanzania na Wakenya ni ndugu wanaopendana, Wakenya wanaonekana wana roho nzuri sana. Takwimu zinaonesha kuwa Kenya imeshaifanyia Tanzania mambo mengi mazuri kuliko iliyofanyiwa na Tanzania.

1. Wakati wa vita vya Kagera, Kenya iliipatia Tanzania ushirikiano uliowezesha JWTZ kuteka ndege ya Libya ikiwa na wanajeshi wa Libya waliokuwa wanaenda kumsaidia Idd Amin.

2. Kagera ilipokumbwa na tetemeko la ardhi, Kenya ilituma msaada wa kuwasaidia wahanga.

3. Baada ya Tundu Lissu kupigiwa risasi, alienda kutibiwa Nairobi nchini Kenya. Sijui kama angepata huduma bora kama hiyo kama angepelekwa Kigali nchini Rwanda.

4. Baada ya Godbless Lema kuamua kukimbia nchini kwa madai kuwa maisha yake yalikuwa hatarini, ni Kenya ndiyo ilimsaidia kutorokea huko alikokimbilia. Inasemekana Serikali ya Tanzania ilitaka Lema arudishwe nchini lakini Kenya ikagoma. Vipi kama angepitia Uganda, Museveni angekubali?

5. Baada ya mwimbaji wa nyimbo za Injili, Rose Muhando kuugua, alienda kupata matibabu nchini Kenya. Hakutumia fedha zake binafsi. Alihudumiwa kwa fedha na rasilimali za Wakenya. Sijui ingekuwaje kama angeipata hiyo changamoto akiwa nchini Burundi. Ndiyo maana baada ya kupona, alitunga wimbo kuishukuru Kenya kwa kumsaidia.

6. Serikali ya Kenya ilipokamata dhahabu iliyosadikika ilitoroshwa kutoka Tanzania, Rais Uhuru Kenyatta aliamuru zirejeshwe Tanzania. Hakujali kuwa Tanzania ilishawahi kuchoma vifaranga vilivyotoka Kenya. Zilirejeshwa kwa kutumia ndege ya Jeshi la Kenya, nafikiri.

7. Baada ya Wamasai wa Loliondo kuparurana na Jeshi la Polisi, majeruhi wa Kimasai walienda kutibiwa nchini Kenya. Walikuwa na amani zaidi kwenda kutibiwa nchi jirani, Kenya, kuliko nchini kwao.

Kwa mifano hiyo michache na mingi inayofanana nayo, ni halali Watanzania wakisema "Mungu ibariki Kenya".
 
Ushirikiano wa kenya na Tanzania haujawahi kuwa wa mashaka hata kidogo
Tanzania imekuwa na viongozi wengi sana wenye asili ya Kenya bila hofu akiwepo prof Sarungi
Tuko vizuri Kenya kuisaidia zaidi tz ni kwa sababu ndie big brother lazima atoe zaidi
 
Ingawa wakati mwingine Watanzania na Wakenya hushambuliana kwenye mitandao ya kijamii, haimaanishi kuwa ni maadui. Utani wao ni kama ugomvi wa watoto wanaofuatana kuzaliwa.

Linapokuja suala la shida au changamoto, uhalisia wa mahusiano yao hujithihirisha. Husaidiana.

Ingawa Watanzania na Wakenya ni ndugu wanaopendana, Wakenya wanaonekana wana roho nzuri sana. Takwimu zinaonesha kuwa Kenya imeshaifanyia Tanzania mambo mengi mazuri kuliko iliyofanyiwa na Tanzania.

1. Wakati wa vita vya Kagera, Kenya iliipatia Tanzania ushirikiano uliowezesha JWTZ kuteka ndege ya Libya ikiwa na wanajeshi wa Libya waliokuwa wanaenda kumsaidia Idd Amin.

2. Kagera ilipokumbwa na tetemeko la ardhi, Kenya ilituma msaada wa kuwasaidia wahanga.

3. Baada ya Tundu Lissu kupigiwa risasi, alienda kutibiwa Nairobi nchini Kenya. Sijui kama angepata huduma bora kama hiyo kama angepelekwa Kigali nchini Rwanda.

4. Baada ya Godbless Lema kuamua kukimbia nchini kwa madai kuwa maisha yake yalikuwa hatarini, ni Kenya ndiyo ilimsaidia kutorokea huko alikokimbilia. Inasemekana Serikali ya Tanzania ilitaka Lema arudishwe nchini lakini Kenya ikagoma. Vipi kama angepitia Uganda, Museveni angekubali?

5. Baada ya mwimbaji wa nyimbo za Injili, Rose Muhando kuugua, alienda kupata matibabu nchini Kenya. Hakutumia fedha zake binafsi. Alihudumiwa kwa fedha na rasilimali za Wakenya. Sijui ingekuwaje kama angeipata hiyo changamoto akiwa nchini Burundi. Ndiyo maana baada ya kupona, alitunga wimbo kuishukuru Kenya kwa kumsaidia.

6. Serikali ya Kenya ilipokamata dhahabu iliyosadikika ilitoroshwa kutoka Tanzania, Rais Uhuru Kenyatta aliamuru zirejeshwe Tanzania. Hakujali kuwa Tanzania ilishawahi kuchoma vifaranga vilivyotoka Kenya. Zilirejeshwa kwa kutumia ndege ya Jeshi la Kenya, nafikiri.

7. Baada ya Wamasai wa Loliondo kuparurana na Jeshi la Polisi, majeruhi wa Kimasai walienda kutibiwa nchini Kenya. Walikuwa na amani zaidi kwenda kutibiwa nchi jirani, Kenya, kuliko nchini kwao.

Kwa mifano hiyo michache na mingi inayofanana nayo, ni halali Watanzania wakisema "Mungu ibariki Kenya".
Unazungumzia wakenya wa enzi za Jomo kenyatta,siku hizi wamekuwa watu wa hovyo,ukiishi nao ndio utajua vizuri
 
#3,5,7 zote ni za matibabu
Ni kuelimishe tu kuwa hapakuwa na roho nzuri, walienda kwa sababu Kenya ndiko kwenye huduma nzuri zaidi za Hospitali ukanda wa Africa mashariki na WOTE HAO WALILIPIA, ingekuwa roho nzuri wangetibiwa Bure!
4; Lema kusaidiwa sio suala la kenya; ni usaidizi wa kawaida wa kimataifa (mkimbizi wa Siasa, kimataifa hupewa usaidizi)
Kimsingi Tanzania ndio inabeba wakenya wengi tu kwa janja janja ya kujiita Wajuluo au Wamasai; ngoja nisiende huko nisikokuwa na ujuzi nako....

Nyongeza:
1. Kama ungekuwa unafuatilia mambo ya ukanda huu, ungejua jinsi Kenya walivyo mnyanyasa MIGUNA MIGUNA - (Lema hafiki hata robo)
2. Unamsahau baba (Odinga) alivyo nyanyasika; kupigwa mabomu hata kwenye gari lake, ni Mungu tu amemuweka hai hadi leo
3. Unasahau uchaguzi wao, yule aliyekataa kutoa password ya seva ...akakutwa ameuawa kabisa....
4. Na mengine meeeengi

Kama huna data, ungetulia tu.....
 
Ingawa wakati mwingine Watanzania na Wakenya hushambuliana kwenye mitandao ya kijamii, haimaanishi kuwa ni maadui. Utani wao ni kama ugomvi wa watoto wanaofuatana kuzaliwa.

Linapokuja suala la shida au changamoto, uhalisia wa mahusiano yao hujithihirisha. Husaidiana.

Ingawa Watanzania na Wakenya ni ndugu wanaopendana, Wakenya wanaonekana wana roho nzuri sana. Takwimu zinaonesha kuwa Kenya imeshaifanyia Tanzania mambo mengi mazuri kuliko iliyofanyiwa na Tanzania.

1. Wakati wa vita vya Kagera, Kenya iliipatia Tanzania ushirikiano uliowezesha JWTZ kuteka ndege ya Libya ikiwa na wanajeshi wa Libya waliokuwa wanaenda kumsaidia Idd Amin.

2. Kagera ilipokumbwa na tetemeko la ardhi, Kenya ilituma msaada wa kuwasaidia wahanga.

3. Baada ya Tundu Lissu kupigiwa risasi, alienda kutibiwa Nairobi nchini Kenya. Sijui kama angepata huduma bora kama hiyo kama angepelekwa Kigali nchini Rwanda.

4. Baada ya Godbless Lema kuamua kukimbia nchini kwa madai kuwa maisha yake yalikuwa hatarini, ni Kenya ndiyo ilimsaidia kutorokea huko alikokimbilia. Inasemekana Serikali ya Tanzania ilitaka Lema arudishwe nchini lakini Kenya ikagoma. Vipi kama angepitia Uganda, Museveni angekubali?

5. Baada ya mwimbaji wa nyimbo za Injili, Rose Muhando kuugua, alienda kupata matibabu nchini Kenya. Hakutumia fedha zake binafsi. Alihudumiwa kwa fedha na rasilimali za Wakenya. Sijui ingekuwaje kama angeipata hiyo changamoto akiwa nchini Burundi. Ndiyo maana baada ya kupona, alitunga wimbo kuishukuru Kenya kwa kumsaidia.

6. Serikali ya Kenya ilipokamata dhahabu iliyosadikika ilitoroshwa kutoka Tanzania, Rais Uhuru Kenyatta aliamuru zirejeshwe Tanzania. Hakujali kuwa Tanzania ilishawahi kuchoma vifaranga vilivyotoka Kenya. Zilirejeshwa kwa kutumia ndege ya Jeshi la Kenya, nafikiri.

7. Baada ya Wamasai wa Loliondo kuparurana na Jeshi la Polisi, majeruhi wa Kimasai walienda kutibiwa nchini Kenya. Walikuwa na amani zaidi kwenda kutibiwa nchi jirani, Kenya, kuliko nchini kwao.

Kwa mifano hiyo michache na mingi inayofanana nayo, ni halali Watanzania wakisema "Mungu ibariki Kenya".
Ni kweli mkuu Wakenya ni watu wenye moyo radhi wasio na hila nyingi kama wabongo, Tanzania na Kenya ni ndugu wa damu kabisa.
 
Ushirikiano wa kenya na Tanzania haujawahi kuwa wa mashaka hata kidogo
Tanzania imekuwa na viongozi wengi sana wenye asili ya Kenya bila hofu akiwepo prof Sarungi
Tuko vizuri Kenya kuisaidia zaidi tz ni kwa sababu ndie big brother lazima atoe zaidi
Na aliyekuwa Waziri wa Elimu, Joseph Mungai inasemekana naye alikuwa Mkenya.
 
Wakenya ukiachana na ukabila wao wanapendana sana, Huwa wanafanya Harambee za kuchangishana watoto wakosome Ng'ambo, hii kwa Tanzania haiwezekani ndugu pekee hawako tiyali kumchangia ndugu yao akasome hata hapa ndani ya nchi achilia mvakia nje
Hiyo ilikuwa zamani siku hizi hakuna nimeishi kenya wana maisha mgumu sana,
 
Hawajui WaKenya
Wanasomeshana kwa ukabila
Katika East Africa wenye Roho za utu ni WaTanzania ndio maana tunaitwa wajinga na majirani. WaKenya hawana utu ni wakatili wanawake kwa wanaume. Hujaona matukio wewe ingia YouTube channel zao utajiambia nawapenda WaTanzania amini hili Mkuu!
 
Hawajui WaKenya
Wanasomeshana kwa ukabila
Katika East Africa wenye Roho za utu ni WaTanzania ndio maana tunaitwa wajinga na majirani. WaKenya hawana utu ni wakatili wanawake kwa wanaume. Hujaona matukio wewe ingia YouTube channel zao utajiambia nawapenda WaTanzania amini hili Mkuu!
hivi kwa mfano tungekua roho mbaya, unadhani tungekua bado tunaishi na ndugu zako walioko humu kutwa kucha kazi yao ni kuombaomba kweli? wanajua wanapata kitu ndio kwa maana hawaishi kumiminika humu mamia kwa mamia takriban miji yote ya Kenya ukienda utawakuta
 
Hawajui WaKenya
Wanasomeshana kwa ukabila
Katika East Africa wenye Roho za utu ni WaTanzania ndio maana tunaitwa wajinga na majirani. WaKenya hawana utu ni wakatili wanawake kwa wanaume. Hujaona matukio wewe ingia YouTube channel zao utajiambia nawapenda WaTanzania amini hili Mkuu!
Nawapenda Watanzania kwa sababu mimi nami ni Mtanzania!

Kuwepo watu wachache wakatili hakuwezi kuwaondolea Wakenya sifa nilizowahusisha nazo. Isitoshe, hata hapa Tanzania kuna watu wachache wakatili!

Kwani hukusikia mwanaume aliyemwua mtoto wake mwenye ualbino mkoani Kagera?

Hukusikia mwanaume aliyehukumiwa kunyongwa hadi kufa mkoani Geita kwa kosa la kumwua mtoto wake mchanga kisa hajafanana naye sura?

Hukusikia mwanamke aliyemwua mume wake hivi karibuni mkoani Kilimanjaro kwa sababu ya wivu wa mapenzi?

Matukio kama haya yatahalalisha kuwaita Watanzania makatili?

Kuyasema mema ya jirani yako ni ukomavu! Wakenya Wana roho nzuri! Wapewe maua yao!!!
 
Back
Top Bottom