Wakenya wanataka fainali ya AFCON 2027 ifanyike kwao

Wakenya wanataka fainali ya AFCON 2027 ifanyike kwao

Sawa tuu,ufunguzi ukifanyika Tzn hakuna shida pia japo sidhani kama CAF watapeleka fainali Kenya Kwa sababu Tzn Ina mashabiki wengi.
Mji ambao unaandaa fainali haungaliwi Kwa wingi wa mashabiki wa nchi husika Bali ni miundombinu na hotel za kutosha na usalama.
Nchi ya marekani haina washibiki wa Mpira lkn bado washabiki walijaa.
Nairobi Wana hotel za maana kushinda DAR na Hali ya hewa ni tamu Sana kushinda hapa DAR
 
Hauoni kama ni sehemu ya kujitangaza ulimwenguni? Wakenya sio wajinga Hadi wapiganie fainali ipigwe Nairobi kwasababu wanajua nchi Yao itaweka history na kuongeza thamani ya utalii..
Zile nguvu zilizotumika kwenye royal tour zingeenda huku
Ukifanya cost benefit analysis ya kujitangaza kuna namna nzuri zaidi za kujitangaza.

Kuhost michezo kunaleta prestige ya nchi zaidi ya kusaidia uchumi.

Hili ni jambo ambalo nchi zilizopiga hatua kiuchumi zinafanya na kujipongeza na kujitangaza kuwa na sisi tumo.

Qatar ku host World Cup ilikuwa sawa. They could afford that.

Huku Africa Tanzania watu wana njaa, umeshindwa kuwapa hata sukari, nyama ni anasa, umeme wa uhakika hakuna, unataka ku host big tournament? Ujitangaze? Utangaze nini?

Unataka umeme ukatike katikati ya michezo uitangazie dunia kwenu hakuna umeme?
 
Hakuna lolote. Labda kama u host kwa kujibana na kutia aibu.

Fuatilia mashindano ya Olympic wanavyopata hasara almost everytime.

Kabla ya kuhesabu gharama za ujenzi, Ivory Coast wametumia zaidi ya dola za Kimarekani bilioni moja kuandaa AFCON 2023.

Je, nchi yenye matatizo mengi kama Tanzania ni sawa itumie hela zote hizo ku host michezo?
Hivi B1kea Mama Kizimkazi ni issue

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
Tatizo ni wabahili sana, hawanunui tiketi za kuingia uwanjani.
Wanasababisha hasara kubwa
Ruto anajihangaisha Bure. Wakenya wengi hawapendi mpira wa ndani tofauti na Tz uwanja unaweza kukosa mashariki. Anyway it's good move for Kenya. Congratulations to them.
 
Punguza ujuaji wa kijinga Caf Wana fans base kubwa zaidi Tz kuliko Kenya.... CAF hawawezi kupeleka fainal eneo ambalo hamna hamasa ya boli. E.Afrija ni Tz tu ndipo hiyo fainal itapigwa...
 
Kwa kiwango cha soka cha sasa kilichopo Tanzania, Ukubwa wa ligi ya Tz, pamoja na Vibe za ushabiki wa soka sambamba na swaga za kimpira, hakuna namna fainali hizo zinaweza kukwepa kubebwa na Tanzania zaidi kuliko nchi nyingine yoyote katika ukanda huu wa Afrika mashariki.
 
Hata kama mashindano hayo yakasemwa yanafanyika kesho, miundo mbinu ya viwanja bora, utayari wa mashabiki uko Tz kwa 100%.
 
Kimsingi mechi ya fainali inapaswa ichezwe tanzania kwa kuwa tanzania latest ndio imeshiriki fainali hizo huko ivory coast.
 
Hata kama mashindano hayo yakasemwa yanafanyika kesho, miundo mbinu ya viwanja bora, utayari wa mashabiki uko Tz kwa 100%.
Viwanja vyenyewe ndio akina Sheikh Amri Abeid, Kirumba, Mkwakwani na Jamuhuri, Morogoro hivyo ndivyo viwanja mnavyosema. Mmekosa kazi nyie.
 
Wakenya wanataka fainali ya AFCON 2027 ifanyikiwe kwao. Rais Ruto ameliagiza Jeshi pamoja na Wizara ya Michezo wajenge uwanja wenye hadhi ya Kimataifa unaobeba watu 60,000 jijini Nairobi tena Ukamilike ndani ya Miaka 2 tu. Tanzania inabidi tuchangamke, fainali ichezewe kwa Mkapa.

Sisi wabongo tukiwa bado kwenye usingizi wa pono wa siasa michezoni pamoja na UJINGA wa akina Haji manara na akina Baba levo wenzetu wakenya wameshatoka usingizini Toka SAA 11 alfajiri. Wakenya wanajua dunia nzima itasimama kuangalia fainali pale Nairobi...

Wizara yetu ya michezo imejipanga vipi na haya mashindano ya AFCON 2027 au bado tunawasubiri wahamasishaji wa soka akina mwijaku?View attachment 2925194
Wasilazimishe mambo.Hoja ya mashindano kuletwa Tanzania,Kenya na Uganda ni kwa hamasa na mvuto uliopo Tanzania. Wawe na shukrani yenye subira.
 
Back
Top Bottom