Unayo haki ya mawazo huru mkuu cassava. JPM hakuwa fascist. Alikuta taifa la wapigaji na akaamua alichangamshe.
Hakuna fascist anayeweza kujenga SGR kama ilivyojengwa na kuelekea kumalizika.
Hakuna dikteta anayeweza kupambana mpaka bwawa la Mwalimu Nyerere limekamilika na kwenda kuongeza umeme kwenye gridi ya taifa.
Hakuna dikteta mwenye uwezo wa kufufua shirika la ndege na linapaa katika ushindani wa kidunia kwa kasi, hayupo mbabe wa aina hiyo.
Tunadhani ni dikteta kwa sababu wengi wetu tulizoea kubembelezana katika kila hatua ya uongozi wa nchi, tumezoea mno kupiga domo na kudhani wenzetu na wao wanaendekeza ujinga huu wa demokrasia zinazopitiliza kama sisi.
Muungano wetu sio fumbo la imani, mkuu usiikejeli imani katoliki hata kama wewe sio mkatoliki.
Muungono wetu umejikita kwenye utu wa mtu na hauwezi kukwepa mantiki ya muungano wakati wowote ule wa maisha yako. Usiwasikilize hawa wapumbavu wanaozungumzia Utanganyika katika afrika mashariki ambayo Sudan ya kusini inataka kuwa sehemu yake pia.
Usiwasikilize hawa wapumbavu wanaojiita watanganyika wakati Congo anaingia kwa kasi kuwa sehemu ya jumuiya ya afrika mashariki na kati.