Wakili Msomi Peter Kibatala amhakikishia kumpigania Mwanachadema aliyekamatwa Kisutu, aahidi kumtoa selo

Wakili Msomi Peter Kibatala amhakikishia kumpigania Mwanachadema aliyekamatwa Kisutu, aahidi kumtoa selo

Out of topic issue ni freembowe katiba kaandamane wewe na mama yako
Huna hoja mpaka unaleta kisirani chako kwangu, kukusaidia tuu ni kwamba wanasema watu waandamane ni viongozi wako wa chadema 😂😂😂 Bila shaka ulimaanisha viongozi wako wa chadema wakaandamane na mama zao.
 
Brazil linapofika swala la kitaifa ni marufuku kwenye maandamano kupeperusha bendera ya chama. Mnaweka vyama pembeni na kubeba bendera ya Taifa. Siasa hizi za kistaarabu bado hazijaanza kufanya kazi Tanzania.
Iko siku tutafika
Nalog off
Ni kweli mkuu, inafika wakati unajiuliza hii katiba mpya ni ya chadema au nchi.!
 
Kibatala, kama uko humu, ubarikiwe sana na Mungu akujalie, akuzidishie wema na alinyanyue jina lako juu zaidi. Mtu safi, mchukia mikwaruzo na mpenda haki... ya nini kukamata watu kisha bango? Naombeni hata nyie polisi walinda haki, uhuru na mali za watu, badilikeni basi, dunia inasonga kwa kasi sana, ya nini kuwa katika mawazo mgando na kuwaonea watu? Mabango yamekuwapo enzi na enzi hata wakoloni hawakuwakamata wafuasi wa Kifimbo kwa kuonesha hisia zao kwa njia ya ,mabango.. acheni kuonea watu, ipo siku watu wataanza kujitoa muhanga, msije sema hamkuliona hilo... Chululu chululu sio ndondondo... haba na haba hujaza kibaba, shauri yenu... nyie endeleeni tu kuwaonea wenye nchi na wenye haki... haya ya uonevu, yana mwisho wake. Nyie endeleeni tu kuwa kama mamba anayekimbilia mtoni wakati mvua inanyesha...
 
Kumbe kwa Mujibu wa Sheria za Tanzania, kuonyesha bango si kosa na wala halijawahi kuwa kosa, Polisi wengi wanaowakamata walioshika mabango yenye ujumbe usio na matusi ama udhalilishaji wanafanya hivyo ili kuwafurahisha waliowatuma ili wapandishwe vyeo ama waongezwe Marupurupu tu.

Msikilize Peter Kibatala akifafanua huku polisi waliotumikishwa wakijiinamia kwa aibu

View attachment 1881136
We mama mbona hukwenda kuonyesha bango? Umebaki JF ukibonyeza keyboard tu?
 
Kumbe kwa Mujibu wa Sheria za Tanzania, kuonyesha bango si kosa na wala halijawahi kuwa kosa, Polisi wengi wanaowakamata walioshika mabango yenye ujumbe usio na matusi ama udhalilishaji wanafanya hivyo ili kuwafurahisha waliowatuma ili wapandishwe vyeo ama waongezwe Marupurupu tu.

Msikilize Peter Kibatala akifafanua huku polisi waliotumikishwa wakijiinamia kwa aibu

View attachment 1881136
jamaa mropokaji mahakamani utafikiri sio mwanasheria, na shreia hajui. ila chadema huwa wanamuona msomi balaa. the only msomi ninayemheshimu kwenye tasnia hiyo ni Tundu Lisu, ila huyo dogo chadema mmepotea sana, labda kama ni kisiasa. anawaaminisha watu watatoka, mbona huwa wanafungwa mikononi mwake?
 
Kwa nini watawala wa kiafrika wanapuuza sana sheria,kwani sheria zipo hapo ili iweje sasa ama zimetungwa kwaajili ya akina mbwa
 
Kumbe kwa Mujibu wa Sheria za Tanzania, kuonyesha bango si kosa na wala halijawahi kuwa kosa, Polisi wengi wanaowakamata walioshika mabango yenye ujumbe usio na matusi ama udhalilishaji wanafanya hivyo ili kuwafurahisha waliowatuma ili wapandishwe vyeo ama waongezwe Marupurupu tu.

Msikilize Peter Kibatala akifafanua huku polisi waliotumikishwa wakijiinamia kwa aibu.

View attachment 1881136
Lesson No.2.
Kwa siku hii hii ya leo. pekee!

Mwishowe elimu itaenea kila sehemu.
 
Wapenda amani kote nchini na wazalendo wa nchi popote pale walipo kamwe tusikubali hawa wahuni wachache wanao jifanya wanadai haki kwa kuvunja sheria watuharibie Amani ya nchi yetu.
tuchukue hatua za kuwafichua na kuwa ripoti popote pale walipo.
sio wafuasi wote wa chadema wanafurahia uhuni huu bali wapo wahuni wachache wenye chembe chembe za Ugaidi/uhalifu/ujanbazi/wizi ndio wanafanya vitendo hivi vya kihuni ili wapate sababu.
 
Familia ya Mbowe, Mnyika, Mrema, Kibatala wote wanao uhakika wa kula vizuri na kusoma lkn wewe ambaye maisha yako ni ya kubangaiza unaishia gerezani unaacha familia yako inateseka. jiongeze, achana na upuuzi tafuta maisha yako uwe na uhakika.
 
Ni kweli mabango hayakuwa na matusi lakini je mliandika kitu gani.? Chadema jikiteni katika kutoa elimu kwa wananchi kuhusu faida ya katiba mpya.

Mimi nitakuwa tayari kuandamana ikiwa nitaona hiki kichwa cha habari kinasema 'WANANCHI WA TZ WAMEANDAMANA KUDAI KATIBA MPYA' ila nikiendelea kuona kichwa cha habari kinasema 'WANA CHADEMA WAANDAMANA KUDAI KATIBA MPYA' basi kamwe sitokuwa pamoja nanyi, bila kusahau nataka niwaone hao viongozi wanaohitaji katiba mpya wakiwa mstari wa mbele katika maandamano.
Utajuaje waandishi wa habari wataandika nini kuhusu maandamano yanayoendelea? Bora usiandamane. You won't be missed.

Amandla...
 
Brazil linapofika swala la kitaifa ni marufuku kwenye maandamano kupeperusha bendera ya chama. Mnaweka vyama pembeni na kubeba bendera ya Taifa. Siasa hizi za kistaarabu bado hazijaanza kufanya kazi Tanzania.
Iko siku tutafika
Nalog off
Brazil ya wapi hiyo? Buguruni?

Amandla...
 
Back
Top Bottom