Wakili Mwabukusi, Emmanuel Masonga na Mdude Nyagali wakamatwa na Polisi Mikumi wakiwa safarini kuelekea Dar es Salaam

Wakili Mwabukusi, Emmanuel Masonga na Mdude Nyagali wakamatwa na Polisi Mikumi wakiwa safarini kuelekea Dar es Salaam

tangulia wewe watakukuta polisi ukiwa unarusha mawe
Mimi ni muhehe kiongozi wa wahehe wote jamii forum sisi tunayorekodi ya kutosa maganga dunia nzima inajua. Msiwe na wasiwasi juu ya hilo nakungoja wewe tuu twende
 
Yaani hata wafanye, lazima wajibu tu hizi hoja.....

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
hizo ni porojo na vioja mpelekee mamako atakujibu huo uvundo wako
 
Haisikitishi, hii inasisimua, wanadhani Adv. Mwabukusi ndie pekee kupinga utoaji bure bandari zetu milele kwa mwarabu, wanajidanganya. Usiogope.
Hakuna cha Mwabukusi wala nzi yeyote kukatiza Mikumi, shenzi zenu. Eti Bandari imeuzwa, wekeni risiti ya EFD hapa tuone imeuzwa kiasi gani!!

Yaani tupitwe na Beira, Mombasa na Lobito sababu ya hawa wajinga wawili Mwabukusi na Mdude!! Pumbavu sana
 
Mimi ni Muislam sahahau kabisa huo ujinga wa kuwacha dini.

Unataka niwe kama wewe usiye na dini?
Bibi leo umeshauriwa vizuri maana dini yako angalau ingekufanya smart kama kikwete tungeona inakusaidia.
 
Mamlaka isifanye mambo kimihemko, madhara yatajayotokea Kwa Mwabukusi yatachochea chuki dhidi ya Samia, hii iliopo itakua maradufu.
huyo nyau hana lolote la kusababisha, serikali imewashughulikia watu wakubwa maarufu km Aboud Jumbe aliyekuwa rais wa Zanzibar, huyo nyau anatafuta umaarufu kwa bei rahisi agombee ubunge kule kwao, sisimizi tu huyo
 
Ndugu Watanzania,

Taarifa zilizotufikia hivi punde ni kuwa wakili msomi Boniface Kanjunjule Mwabukusi amekamatwa na Jeshi la Polisi kule Mikumi, Morogoro akiwa pamoja na Katibu wa Kanda wa CHADEMA, Emmanuel Masonga na Mdude Nyagali.

Inadaiwa kuwa walikuwa safarini kuelekea Dar es Salaam. Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika, watu waliojitambulisha kuwa ni Askari ndio wamewakamata pasipo kutaja kosa lao na wapi wanapelekwa zaidi ya kuambiwa ni Maelekezo kutoka Juu. Pia, vifaa vyao vya mawasiliano (Simu za mkononi) vimechukuliwa.
This is a police state mimi sishangai. Kinachonishangaza ni reaction ya watu. Kwa sababu watu wanadhani haliwaathiri wao jwa sababu hawahudiki moja kwa moja. How wrong. Mnakumbuka 1990 wanafunzi wa UDSM walipinga suala zima la mikopo ya wanafunzi. Chuo kilifungwa na wanafunzi wa primary na secondary schools wakaandamana kuwalaani UDSM. Ujinga wao hawakufikiria kwamba nao wanapitia huko huko. Waliokuja kuathirika zaudi ni wao na mpaka leo watu wanapata shida na mikopo hiyo. The same is happening now. Believe me tutapata maumivu makubwa sana. In fact tumeshaanza. Tunatakiwa kulipa 1.5trn na kesi bado xinaendelea.
 
Back
Top Bottom