Wakili Mwabukusi: Wapinzani hawana afadhali yoyote na CCM, ni wabaya kuliko hata CCM

Wakili Mwabukusi: Wapinzani hawana afadhali yoyote na CCM, ni wabaya kuliko hata CCM

HAKUNA TOFAUTI KATI YA CCM NA WAPINZANI, NI WALEWALE" MWABUKUSI

Upinzani na CCM hawana tofauti, kitendo cha kutaka kuingia kwenye uchaguzi bila katiba mpya ni kwa sababu ya maslahi binafsi na sio maslahi ya Taifa, ndio maana kuna chawa wa chama tawala na huku upinzani nako kuna machawa huku kwetu kwenye upinzani

Hakuna mtu yuko tayari kumwambia kiongozi wake kwamba anayoyafanya hayako sawa, hatuna hata mgambo lakini nakuhakikishia sisi wapinzani ni wabaya kuliko hawa walioko madarakani, tunaogopana kuambiana ukweli, sisi na CCM hatuna tofauti kabisa.

Najiuliza kwanini wapinzani tunashindwa kuonyesha msimamo?

kwanini twende kushiriki uchaguzi bila katiba mpya?

Nilishasema kuna biashara ya Demokrasia inafanyika hapa nchini"

Chanzo : Jambo Tv
Mwabukusi anashindwa kuelewa kwamba haya yanatokea kwa sababu zile kamati za siri ziitwazo deep state zilibariki eti siasa ndio iwe kazi yenye malipo makubwa kuliko kazi nyingine!!! Ndio maana uchawa ni karata kubwa kwa ajili ya teuzi Ili wale mapesa!!

Akipatikana mtu kama Mimi nitakayeifanya siasa kuwa kazi ya kawaida isiyo. Na malipo makubwa kama ya ualimu tu vile nakuambia tutatatua tatizo kubwa sana,mapato ya siasa yaende kwenye ueledi Ili kuleta tija kwenye maendeleo ya watu wote!!!


Nitaendelea kulia na dola siku zote!!
 
Hapana. Lazima vyama vya upinzani viingie kwenye uchaguzi ili kupata nguvu ya kupambana na chama tawala. Mawazo na msimamo wa adv. Mwabukusi ni sahihi, lakini, si sahihi sana kwa wakati huu. Mapambano katika uwanja ya vita lazima kubadili mbinu za medani mara kwa mara kutokana na wakati na mazingira.
Nashauri vyama vya upinzani, ... Njoo vijijini kama Chadema walivyofanya huko kanda ya ziwa, Rukwa na kwingineko. Waelimisheni Watanzania juu ya hali yao na wanavyostahili kuwa. Wataelewa. Na baada ya hapo ingieni kwenye uchaguzi huku mkiimarisha usimamizi wa zoezi au mchakato mzima wa kura. Nendeni wilayani Nkasi mkajifunze Wananchi walifanyaje hadi Serikali na Chama tawala wakasalimu amri mwaka 2020 hata mwanamke, tena binti mdogo tuu Aidah Kenani akamgaragaza kwa aibu aliyekuwa mbunge machachari na maarufu Ally Kessy Mohamed. Inawezekana.
Kimsingi, Wananchi walikwishaichoka CCM na Serikali yake. Wanataka mabadiliko. Lakini, ni nani atakayewaongoza kuleta mabadiliko hayo? Ni Chama gani? Hawa hawa wachumia-tumbo Chadema, ACT, TLP, and the like?!
Anyway, vyama vya upinzani hamjachelewa bado, ingieni vijijini, "mwageni sumu" kwa Wananchi; wataelewa na kukisubiri CCM kwenye sanduku la kura.
Mwabheja sana!

Shida uchaguzi kwa katiba hii na sheria zilizopo ni Bure tu. Serikali ndio inaamua nani akae wapi na asikae wapi.
 
Ndio!!
CCM ni chama cha kihistoria tena historia iliyotukuka...

Na hata Chadema mnayo Historia inawayowatambulisha vizuri sana katika Jamii,
Mathalani kuwa na Mwenyekiti wa chama wa Maisha.

Lakini pia mna historia ya kutukana mno na mihemko kwa sana tu,

Mna historia ya sususia mambo mbalimbali kama vile chaguzi, baadhi ya mitandao ya simu na kadhalika, vitu ambavyo havijawahi kuwasaidia chochote Zaidi ya kuwaharibu na kudidimiza Zaidi.

Na kwasasa Chadema imevamiwa mathalani na mtu kama wewe, kutwa uchwao kulalamamika na kulaumu mara dipi weldi, mara tume ya uchaguzi, mara katiba mpya vitu ambavyo viko kwenye mipango na rada za serikli na itashughulika navyo kwa wakati wake kadiri itakavyona inafaa.

Nje ya hapo no consultation, no mobilization and engagements na wanachama uchaguzi unafika unashindwa then unakuja tena kulalamika unadai kuibiwa 😜

My friend,
Piolitics is science
Ukija kichwa kichwa unaliwa kichwa vizuri tu na kulaumu mpaka siku ya Mwisho....
Historia ya ccm huko siku za nyuma ilikuwa ina maana kwa kiwango fulani, ila baada ya kujazana mafisadi, kwa sasa inaongooza kutokana na kujaa makondoo hapa nchini. Haina sifa nyingine zaidi ya kuwa chama Cha majizi.

Cdm hawana muda wa kushiriki upuuzi ili ionekane ina sifa ya kutosusia. Na Isitoshe kususia na njia sahihi ya kisiasa popote pale duniani. Hata sisi kama nchi tumewahi kususia baadhi ya nchi. Mfano tuliwasusia Africa kusini wakati wa apartheid, lakini hatukuzuia SA kuwa matajiri na uchumi mkubwa.

Huko cdm Mimi ni shabiki wa kutupwa na Wala sijavamia. Sina popote ninapowasifia au kuwaunga mkono majizi ya ccm. Sasa unaposema nalalamika sijui unaanisha Nini. Tume ya uchaguzi na katiba mpya sio ombi ni lazima maana vimedaiwa kwa more than 30yrs, hivyo enough is enough. Hatuna muda wa kuendelea kushiriki upuuzi uitwao uchaguzi wakati tunaona kabisa hilo zoezi haliheshimiwi. Uchaguzi tunashindwa ama ni uhayawani huwa unaendelea? Hakuna ccm ya kuendelea kushinda kama mtakavyo.

Siasa ni science, ila sio kwa hizi siasa za kipuuzi mnazoendesha ccm. Labda kama hilo neno science unalitumia kama fashion.
 
Ndio!!
CCM ni chama cha kihistoria tena historia iliyotukuka...

Na hata Chadema mnayo Historia inawayowatambulisha vizuri sana katika Jamii,
Mathalani kuwa na Mwenyekiti wa chama wa Maisha.

Lakini pia mna historia ya kutukana mno na mihemko kwa sana tu,

Mna historia ya sususia mambo mbalimbali kama vile chaguzi, baadhi ya mitandao ya simu na kadhalika, vitu ambavyo havijawahi kuwasaidia chochote Zaidi ya kuwaharibu na kudidimiza Zaidi.

Na kwasasa Chadema imevamiwa mathalani na mtu kama wewe, kutwa uchwao kulalamamika na kulaumu mara dipi weldi, mara tume ya uchaguzi, mara katiba mpya vitu ambavyo viko kwenye mipango na rada za serikli na itashughulika navyo kwa wakati wake kadiri itakavyona inafaa.

Nje ya hapo no consultation, no mobilization and engagements na wanachama uchaguzi unafika unashindwa then unakuja tena kulalamika unadai kuibiwa 😜

My friend,
Politics is science
Ukija kichwa kichwa unaliwa kichwa vizuri tu na kulaumu mpaka siku ya Mwisho....

Hayo ungesema kukiwa na Time huru na mabadiliko ya katiba. Sio kwenye nchi hii ambayo Mkuu wa mkoa anampigia kampeni mbunge wa CCM.
 
Swala la uchaguzi nitaamuliwa na vikao halali vya chama na wanachama, chadema sio chama cha mchezo msifikili ikitokea wakasusa uchaguzi kwamba patakalika, haijalishi ni vyama vya mfukoni vingapi vinaweza shiriki, hilo ccm wakae wakilijua na wasilete hujua na jambo hili ,

Unapozungumzia siasa za tz ndani na nje ya nchi unazungumzia ccm vs Chadema , so hacha ccm wajichanganye ndo watakapo lifikisha taifa pale wanapataka
 
uchaguzi chadema itashiriki ,na itashindwa kihalali
Hakuna ccm ya kushinda kihalali nchi hii. Na siku ccm itakubali ushindani wa halali ndio itakuwa mwisho wake. Cdm kama chama kushiriki huo ni uamuzi wao, lakini sisi wapiga kura tulio wengi hatutakuwa na muda tena wa kushiriki huo upuuzi usioheshimiwa.
 
Kashaanza kuchanganyikiwa...anaanza kuona joto la sirikali...uwakili ukienda na mishe za kusaka ugali zitaathirika pakubwa!

Alidhani zile rhetorics za DPW zingetosha kuitisha sirikali...truth being revealed before him kwamba sirikali ni lidude likuubwa ambalo kushindana nalo inabidi uende kwa steps za tahadhari!

Ukweli kabisa. Yeye anaona wengine hawafanyi chochote.
 
Sidhani kama yupo anayejielewa atautilia shaka msimamo wa Adv. Mwabukusi, na ni ngumu sana kwa mtu mwenye msimamo wa aina ile, aliyeiweka mpaka nafsi yake rehani, kuchanganywa kundi moja na wapinzani maslahi wanaoutafuta utajiri kupitia siasa, hiyo ni sawa na kuchanganya maji na mafuta.

Huyu ameamua kusema kweli liwalo na liwe, kwani ameshaona dalili huko tuendako, ni wapinzani ndio wataanza kucheza ngoma za CCM na sio vice versa, CCM wameshajua hawa wakitaka kitu chelewa kuwapa mwishowe watageukana wenyewe, kwa sababu hawana misimamo ya pamoja.

Hiki ndicho Adv. Mwabukusi amekiona na kukilaani, na wala sio vinginevyo, ambacho kwangu ni ukweli mtupu.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app

Tusiteme big G kwa karanga za kuonjeshwa. Nadhani hujui motive ya Mwabukusi. Mwabukusi anatumia nguvu nyingi kuishambulia upinzani kuliko CCM. Kwanza kadai wapinzani wanafanya biashara ya demokrasia nk. Sasa kwa kauli Kama hiyo huyo yupo upinzani kwa lengo gani. Hapo kaipa CCM milage kubwa Sana.

Mimi simuamini Tena. Kuna kauli mtu akizisema unajua huyu sio mpinzani ana mission yake tofauti. Mtu unaushambulia upinzani kuliko hata Makonda na chongolo. Muangali Mwabukusi kwa jicho la mbali utaujua ukweli.
 
Nchi za Africa Magharibi nyingi zipo kwny mikono ya Wanajeshi na Raia wanapigania zirudi kwa Raia japp hapo awali waliona bora Mapinduzi ya kijeshi yatokee

Sent from my SM-G9500 using JamiiForums mobile app
Tunataka hayo mapinduzi ya kijeshi, kisha tukirudi kiraia tuanze Moja, hakutakuwa na chama chochote kupendelewa. Hapo Kila mmoja atashinda kwa sera na sio huu uhuni unaoendelea sasa.
 
Unamlaumu nani?. CHADEMA kiliwafukuza wakaenda mahakama kuu, na spika kuwalinda ingawa sio wanachama. Sasa Kama watu wanalindwa na serikali unalaumuje upinzani?.
Huwezi kujua,mchezo wa siasa ulivyo, hivi unajua uwepo wao pale bungeni, ndio nafuu ya serikali yako kkt kuomba misaada huko nje? Hivi unajua uwepo wao pale una baraka zote ambazo wewe ,hoya hoya huwezi kuzijua kamwe? Baki kuwa hoya hoya huku watu wakikuonesha majumba yao na wakila bata
 
Punguza unafiki hakuna upinzani ndio kitu gani?. Mnataka upinzani ufanyeje?. 2020 mmejaza wabunge wa CCM bungeni na madiwani karibia wote wa CCM , halafu unaleta kauli za kinafiki hakuna upinzani.

Ingekuwa nusu ya wabunge wanatoka upinzani halafu wakapitisha mkataba wa DP world au mafao ya wenzi wa viongozi wakuu, huku mama mjamzito akifa kwa kukosa lakini na nusu? basi hata Mimi ningesema hakuna upinzani.

Ila mmejaza CCM kwenye vyombo vya maamuzi lakini lawama kwa upinzani. Mnataka upinzani wafanyeje?. Waanze harakati Kama za akina Prince Johnson wa Liberia enzi hizo?
Hakuna mpinzani ,narudia tena hakuna mpinzani tanzania ,kama hujui jua sasa, labda mpinzani we wewe na dhiki zako
 
Nasema hivi hakuna sifa yoyote ya kuungana wapinzani ili kupewa nafasi za hisani. Kama ushindani wa sera ndio ungekuwa unatoka mshindi hapa kwetu, Leo hii ccm isingekuwa madarakani, na hata kama ingekuwa isingekuwa na uwezo kufanya maamuzi itakavyo. Hilo neno sera mnalitumia kama fashion, lakini ccm haiko madarakani kutokana na sera, Bali sababu za kihistoria, na hasa hasa katiba mbovu ya chama kimoja.

Hizi chaguzi za kihayawani unazoziona, ni ili kuhakikisha ccm inaendelea kukaa madarakani huku kizazi kikiwa kimeichoka. Huo usanii kuwa mko madarakani kwa ajili ya sera, kawaambieni wale wajinga mnaowasomba kwenye malori. Zama za ccm kuendelea kukaa madarakani zilishapita na kizazi chake. Hivyo hizo chaguzi mnazolazimisha kukaa madarakani, fanyeni/shirikini na wenye huo mda mchafu. Na ukitaka kuamini hiki si kizazi Cha ccm, subiri uone idadi ndogo ya wapiga kira watakaojitokeza, kama ishara kuwa hamkubaliki na kizazi hiki tena.
Wapiga kura kidogo sio tu wanaonesha raia hawaiungi mkono CCM bali hata upinzani pia hauungwi mkono, mana kama wangeupenda upinzani basi wangejitokeza kwa wingi sanaaaaaaa kwenda kuwapa kura
 
Back
Top Bottom