Wakinamama wanaolea watoto bila baba (single mothers): Sababu, athari kwa mtoto, changamoto na mitazamo ya jamii

Wakinamama wanaolea watoto bila baba (single mothers): Sababu, athari kwa mtoto, changamoto na mitazamo ya jamii

mi nashauri oa, mwenyewe niko njiani kufanya hivyo hivi karibuni na nilishaleta thread humu ya kuzungumzia hilo (zaidi ilizungumzia kiwango cha mahali). wewe una wasiwasi na mama mwenye mtoto mmoja ambaye baba kakimbia, kuna jamaa yangu flani ye ameoa mwenye watoto wawili tayari tena wa baba tofauti na kila baba anahudumia mtoto wake na ndoa yao ina amani na furaha kama nini.....wana mtoto mmoja sasa!!
Na hayo mahitaji mwanamke anaenda kuyafuatilia mwenyewe au sio?
 
pokrei, Kuachana si suluhisho kwamba hawatakumbushia big no!! Nyie wanawake huwa mnatumia hisia kwenye mambo yanayohitaji mantiki
 
@Mgg3, Kwenye mawasiliano mbona simple haihitaji kuwa vizuri kichwani kwa mwanamke ni hivi kama huyo mwanamke alikubali kutoka na jamaa means alimpensaga na kumwamini ndo maana akaaamua kuzaa naye(japo jamaa ali deviate) ila udhaifu ule ule wa mara ya kwanza ndo jamaa atautumia kupasha kiporo moto.
 
Maskini ya mungu ntamtupa wapi huyu mwanamke anavyoniheshimu namna hii,nakojolea pazuri ndugu yangu we acha
Kama anataka kuolewa kwanini asiwe ma heshima? Au haujaona kuwa ni drama hizo?
 
Umeongea kwa uchungu sana na masikitiko mkuu,lakini wengine tumezoea kash kash,vurugu kwenye maiaha kwaiyo sioni hatari kwa hili wazo langu..
Swala la kuadhibu mtoto kwa kipigo sio jema.
Baba wa mtoto hana time na mtoto na mtoto hamjui baba yake,japo najua itafika kipindi itakua ni muhimu mtoto kumtambua baba yake wa kibiolojia.
Pole sana ndugu yangu na hizi ndio changamoto za maisha upende boga na ua lake.

Kama hapashi kipolo usimuache huyo single mama nakusihi sana mkuu
It's a matter of time kabla hajamkumbuka baba wa mtoto wake ukute jamaa alikuwa haoni kinyaaa daadeki utakuja na uzi hapa
 
tangu lini mechi ikaanza wakati timu moja tayari ina goli?....unahs kutakuwa na maelewano hapo? sheremaya
 
Uchunguzi wangu ni yakinifu,
Labda apo uliposema baba wa mtoto akianza tena kutaka mawasiliano,
Hicho kitu kinachounganisha mimi nikimzalisha hakiwezi kuunganisha..
Mkuu inavyoonekana majibu unayo na unedhamiria kuoa we oa tu ili baadaye uje ulete mrejesho kwa ulichofanyiwa ila kikubwa ni kuwa hiyo connection iliyoongelewa si kwa sababu amezaa na jaamaa hapana bali cnnection iliyopo ndiyo iliyosababisha akazaa na jamaaa na kamwe haiwezi vunjika kwa kuwa upendo alio nao kwa huyo x wake ni mkubwa kushindwa atakao kuwa nao kwako ila nakushauri sana jiandae kisaikolojia sanaa usije kuanza kuumwa na magonjwa ya presha na msongo wa mawazo.
 
Maskini ya mungu ntamtupa wapi huyu mwanamke anavyoniheshimu namna hii,nakojolea pazuri ndugu yangu we acha
Anakuheshimu sababu ana shda sasa subiri huyo mwanae akue..shda ziishe...afu aje akuoneshe tabia halisi sasa....mbna utashangaaa

sku zote watu hujishusha ili kupata huduma fulan
 
Yaani omba mungu usiwe na uzao wa kike maana lazima mungu akulaani kwa huu waraka wako.kizazi chako Cha kike kitapata tabu sana
Maana lazima mungu anilaani!! Mbona wewe umejitwalia hayo mamlaka, halafu hizo ni sifa za shetani. Mungu Mwenyezi muumba mbingu na na nchi akubariki wewe na uzao wako, Amen.
 
Ah wapi! Kwa kosa gani? Ametahadharisha kwa jambo la kweli kabisa, tena mbona atabarikiwa sana. Na uzao wake wa kike utaepushwa na laana ya single motherhood. Na hata watoto wake wa kiume wataepushwa na kukingwa kabisa dhidi ya single mothers.
Wewe mwenyewe nina uhakika hutaki mwanao wa kiume akuletee single mother ati ndio mkweo! Na kama una binti nina uhakika hutaki awe single mother. Ni laana hiyo kitu.
Amen. Umenena vema mkuu, asante sana
 
Niweke nukta kwenye mtazamo wako binafsi?? Hapa tunaangalia uhalisia tu kama single fathers wanaweza kuoa wanawake wanaoanza ndoa inashindikanaje kwa single mothers kuolewa na wanaume wanaoanza ndoa??

Mwanamume humfundisha mkewe kuenenda kwa jinsi atakavyo na sio vice versa. Kuchukua single mother mwenye mafunzo na uzoefu kutoka vyanzo tofauti ni kujitakia matatizo.
 
Hatutetei ila tunaongea uhalisia tunaouona kwenye jamii hatuwezi kukaa tunasikiliza maneno ya watu tu humu wakati matendo ni tofauti
Kumbe tuwaache watoto wa kike wazalishwe hovyo basi, maana limekuwa jambo jema machoni pa wanawake. Pia wanaume wanaoa zaidi wanawake waliozalishwa hovyo na ndoa kudumu. Basi sawa
 
Na sisi tulioishi na Single mom zaidi ya 10yrs tunacomments wapi hapa?
 
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]sasa swala siyo mimi kupenda ila swala ni uhalisia kwamba wapo wanaoolewa
Wasingekuwepo wanaoolewa tungejulia wapi matatizo yao? Kwani tukisema vijana wajiepushe na ushoga masna yake hakuna wanaofanya hayo? Jaribu kuelewa concept, usitetee uharibifu kwa sababu tu kwenye jamii wapo. Simamia kweli daima, usisombwe ni upepo wa mazoea, angalia msingi wa jambo naw utakuwa salama na kizazi chako, Mwenyezi Mungu akubariki
 
Humu tupo wengi sana tukiacha ushabiki wa mitandaoni,Mimi hapa nawakaribisha wenzangu.

Ukweli jamani sisi tuliooa Single mom tunapata raha sana yaani Haiadithiwi na ndoa zetu zinadumu sana mimi huu mwaka wa 9 sasa.

Nasikitika hao wanaotukandia sie kila siku unasikia wameua au wameuawa na wake zao(Someni Alama za nyakati).

NAKUPENDA SANA SINGLE MOM WANGU!!
 
Back
Top Bottom