Wako wapi hawa wasanii?

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2012
Posts
21,113
Reaction score
65,124
Wasalaam,
Hivi hawa dada zetu wasanii wamepotelea wapi?
Nlikuwa nawakubali sana.
1. Enika
2. Dataz
3. Rah P
4. Paulin Zongo
5. Grace Matata

Na pia ningependa kujua hawa wasanii wa kiume wametokomea wapi?

6. Mike T (Mnyalu)
7. Stan Boy (East Coast Team)
8. Rado
9. Steve RnB
10. Chindo Man

Mbona kimya sana na vipaji wanavyo?
Naomba tujuzane.
 
4,5,6,8 na 10 pia ni dada zako? Unatisha mkuu.
 
mnyalu yupo na biashara ya nguo
 
Ndio matatizo ya kuanza kufikiria title kabla ya context.


Ndio matatizo ya kuanza kufikiria title kabla ya context.

Muungwana mimi mbona siyo Mungu!!
Nakosea pia, naamini hata wewe umeshawahi kosea.
πŸ™‚πŸ™‚πŸ™‚πŸ™‚πŸ™‚
Basi nisaidie nijue wako wapi hawa jamaaa.
 
Ila Dataz alikuwa hatari, sijui yu wapi huyu mdada?

Daaa huyu sister tulishawahi kaa naye sehemu moja miaka ya nyuma, ghafla kapotea tu.
Na kwenye gemu nako haonekani wakati uwezo anao
 
Jamani, Mjumbe kauliza swali pamoja na swali la nyongeza. Sasa swali huwa ndio linabeba title na swali la nyongeza huwa linaingia kwenye Any other Business (A.O.B)...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…