Wako wapi mabodigadi na wapambe wa Makonda? Sasa anatembea peke yake vijijini. Je, ni laana ya Warioba? Vijana tuna la kujifunza

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Makonda, almaarufu Bashite, aliongoza Mkoa wa Dar es salaam kwa mkono wa chuma uliojaa damu, ni yeye na sabaya tu waliotembea na mabodigadi wenye silaha za moto, Makonda alithubutu kwenda clouds fm akiwa na askari wanaodaiwa kuwa wa jumba jeupe(makirikiri).

Sasa anaonekana mpweke, wale aliowa harass Sasa wameshika mpini, Jiji aliloliona la kwake, na wakazi wake kama wapangaji, amelikimbia kama Ghadafi alivyoikimbia Tripoli, au Saddam alivyoikimbia Bhaghdad.

Wale walinzi mahiri, makirikiri, hawako nae tena, Polisi na usalama hawako naye tena, ni mpweke huko maporini akipanda milima na kukatiza njia za waenda kwa miguu, pengine anapishana na watu aliowadhuru ila yeye ameshawasahau!

Ni Makonda aliyewaonya viongozi wakuu wa dola kwamba ana nguvu kuliko wanavyodhani!

Wakati ukuta



Cc: Lemutuz
 
Sasa anaonekana mpweke, wale aliowa harass Sasa wameshika mpini, Jiji aliloliona la kwake, na wakazi wake kama wapangaji, amelikimbia kama Ghadafi alivyoikimbia Tripoli, au Saddam alivyoikimbia Bhaghdad
 
Sina mengi ila nauliza kwanini nakala ya uzi wako umempelekea Le Mutuz ?
 
LAANA ya WARIOBA hii hapaaa

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
bashite mjanja kweli kweli, anacho tafuta apo ni ‘huruma’ ya jamii ili asiburuzwe mahakani kwa yale alio wafanyia ‘wabaya’ wake, yaani kwa sasa anapost ‘strategic pictures’ ili kupata huruma na msamaha kutoka ktk jamii na watu aliowafanyia uovu wa kutisha……….na tayari wadanganyika wengi tuu wameisha ingia mkenge wa kumhurumia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…