Wako wapi wale waliokuwa wanatetea umeme wa maji utakuwa bei rahisi?

Wako wapi wale waliokuwa wanatetea umeme wa maji utakuwa bei rahisi?

Mradi utaisha kwa 100%, alafu utaingizwa gridi ya taifa utaenda kureplace baadhi ya uzalishaji ikiwemo mafuta na gesi, hapo ndio hili swali linapaswa kuja. Sasa hivi bado mapema
Ccm ni ile ile ooh ni ile ile
 
Haya malalamiko ni kwa sababu Watanzania hawajazoea kulipa gharama halisi za umeme.
Ningekubaliana na wewe kama kampuni kama IPTL ilichokuwa inalipwa kilikuwa kinaendana na uhalisi wa inachozalisha.

Tanzania is a different country linapokuja suala la ulaji.
 
Ufike mahala tukubaliane au ukubali .....msingi wa hoja upo wazi kwa nini bei haishuki hata baada ya bwawa kuànza uzalishaji......mi nikiongeza pia mbali ya kuànza uzalishaji pia kuna baadhi ya gharama zimepungua kutokana Na kuachana Na vyanzo vingine nilivyokuwa vinasababisha ukubwa wa uzalishaji Na umekiri kuwa ni kweli hivyo vyanzo vimepungua hususani Iptl na wenzake pia umeme wa kutumia jenereta

Iptl kuwa aliacha kuzalisha kabla ya bwawa,sawa ila pia tambua kuwa amepunguza mzigo kwetu Na kwa maana yako ni kuwa kama angekuwepo gharama zingekuwa juu zaidi ya sasa

Umeme wa majenereta,mkoa ninaotoka ni mmoja wapo wa mkoa tulioachana Na matumizi ya jenereta Na kwa hiyo huko kuachana Na matumizi ya jenereta kwa kiasi kidogo ilitakiwa ilete nafuu kwetu watumiaji hata kwa kiasi hicho kidogo Na sio kuongezea mzigo kwetu


Imejengeka miongoni mwetu kuwa Mtu binafsi akiuza kwa kukomoa kwa kuweka faida kubwa kuliko gharama zake za uzalishaji tunamuona beberu ila kwa serikali kutuuzia kwa mtindo huo huo tunatakiwa tuone ni sawa sawia
Kuna sehemu unakosea, nimekujibu mradi haujakamilika kwa 100% hivyo huwezi sema mbona Bei haijapungua. Ilipaswa mradi uishe megawatt zote ziingie grid ya taifa iende kureplace hizo aina nyingine za uzalishaji ndio hapo sasa tutaanza luhojj

Vyanzo vingine vimepungua mfano umetolea iptl, nikamuuliza unajua mbadala wake gharama zipoje? Mfano tu umeme wa mafuta uzalishaji uliongezeka nakufikia megawatt 80.

Unasema umeme wa majenereta umepungua, unaposema umeme wa majenereta unamaanisha nn? Maana mm nitakuambia haujapungua bali umeongezeka. Twende kwa takwimu sasa
 
Yawezekana kama chuma cha pua Magufuli angekuepo angetimiza ahadi yake ya umeme kupungua bei kwa maana ya bei ya unit, usisahau ni kipindi chake alishusha gharama za maunganisho ya umeme kutoka laki 3 na 20 hadi elfu 27 kwa maeneo ya mjini lakini yule bibi chaudele akaja kufanya anavyo jua yeye
 
Wakati ujenzi wa bwawa la Mwalimu Nyerere unaanza, watetezi wake walikuwa wanatoa mishipa ya shingo kuwa bwawa hilo likianza kazi umeme utashuka bei. Nikawa nasema miaka yote tumekuwa tukitumia umeme wa maji, lakini hatukuwahi kuwa na sifa ya umeme wa bei rahisi, maana sababu ya umeme kuwa ghali hapa nchini haiendani na gharama za uzalishaji, bali sababu nyingine kabisa.

Watetezi wakawa wanasema gharama kubwa haiwezi kupungua kwa kutumia umeme wa mafuta. Wakajiapiza umeme wa maji ukianza automatically bei itashuka.

Wakati umefika na kile nilichosema kinaonekana. Bwawa limeanza kazi, umeme unazidi kupanda bei, na kibaya zaidi bado sio wa uhakika maana mgao bado upo, hata kama sio kwa kiwango kikubwa. Kwenye hili la bei wote ni mashahidi kwa walioanza kununua umeme hivi karibuni. Na hapo bado.

Paskali Mayalla Choicevariables, Lucas Mwashamba
Mimi niliwahi tetea lini? Mimi ndio niliqaambia ukweli ambao Maharage Chande na January walikuwa wazi.
 
Aisee Kazi ipo ....., Hivi unapouziwa perfume laki moja na kununua nanasi tshs 500 inamaanisha gharama za kutengeneza hio perfume ni kubwa kuliko nguvu kazi ya kufanikisha hilo nanasi ?

Issue ni kwamba kumalizika kwa Bwawa uzalishaji unatakiwa uwe zaidi ya mara mbili na uendeshaji unapungua sababu overheads za kununua mafuta kwa madalai zinaondoka.....

Sasa kama hio faida inaamuliwa kuliwa na walamba asali hapo katikati hio ni issue nyingine wala haimaanishi kwamba uongozi wenye busara usingeweza kupunguza bei kwenye hii huduma

Sasa mtu mwenye busara angehoji iweje production iongezeke na uendeshaji (gharama zipungue) na bado bei ipande ? Na sio kukubaliana bei inayoletwa mezani kwa ngonjera yoyote ile
The oversimplification aside, lini umeona uwekezaji mkubwa hivi umefanywa ili kuleta nafuu Kwa mlaji? Sizungumzii maneno wanayotumiaga ku 'uza' mradi kwa umma, kama Una mfano wa mradi halisi na matokeo yakawa kama yaliyoahidiwa. I am genuinely curious
 
The oversimplification aside, lini umeona uwekezaji mkubwa hivi umefanywa ili kuleta nafuu Kwa mlaji? Sizungumzii maneno wanayotumiaga ku 'uza' mradi kwa umma, kama Una mfano wa mradi halisi na matokeo yakawa kama yaliyoahidiwa. I am genuinely curious
Kwa Tanzania nothing will work especially now watu hawana machungu na nchi bali matumbo yao..., ila sababu Tanzania kitu hakifanyiki sababu ya utendaji mbovu haimaanishi kitu kile / idea ni mbaya bali utendaji ndio mbaya.

Kwahio wewe ukifanya hesabu moja kujumlisha moja ukapata tatu haimaanishi kwamba jibu sio mbili wala haimaanishi tuache kujumlisha bali wewe ndio uache kujumlisha vibaya
 
Ina maana wewe ni mgeni namna mwendazake alikuwa anaongoza nchi? Sasa huu ujinga unaoendelea sasa si ni utashi wa aliyeko madarakani na genge lake?

Mbona unajizima data. Hii nchi haina mipango na hata hiyo tume ya mipango ipo geresha.
Lione hata bunge letu, hivi utasema tuna bunge kweli?
Tanzania tulihitaji mtu mwenye uzalendo na utashi,maamuzi chanya ya kikatili.
Tulimpata bahati mbaya akaenda zake kabla hajamaliza aliyoyakusudia.
Ndio maana nasema angekuwepo watanzania tungekuwa na furaha sana kwakuwa huzuni zilipotea,zimeanza kurudi baada ya yeye kufariki.
Katuacha yatima. Leo hii hakuna kiongozi hata mmoja anayewapigania wananchi.
Huzuni hazikuwahi kuondoka wakati wa Magufuli, bali hakukuwa na uhuru wa kusema madhila ya wananchi, maana ilikuwa marufuku kutangaza jambo negative wakati wake. Wakati wa utawala wake hatukuwa nje ya nchi boss. Ndio maana nimekupa mfano wa nauli za ndege akiwepo, mbona hazikuwahi kushuka? Ajira hazikuwepo nk. Ni kweli alifanya project kubwa kwa mikopo, na akahakikisha media inatangaza hiyo kwa nguvu zote, lakini sio unafuu kwa maisha ya wananchi. Kikubwa alichofanya ni kupunguza kelele kwa wamachinga baada ya kuruhusu biashara holela.
 
Kwa Tanzania nothing will work especially now watu hawana machungu na nchi bali matumbo yao..., ila sababu Tanzania kitu hakifanyiki sababu ya utendaji mbovu haimaanishi kitu kile / idea ni mbaya bali utendaji ndio mbaya.

Kwahio wewe ukifanya hesabu moja kujumlisha moja ukapata tatu haimaanishi kwamba jibu sio mbili wala haimaanishi tuache kujumlisha bali wewe ndio uache kujumlisha vibaya
Ndio nimeomba mfano wa mradi au wakati ambapo it worked. Maana ili uwe hopeful aidha umewahi ona matokeo, au una taarifa za ndani. Kwa umri wangu nimesikia ya mkonga wa taifa, ving'amuzi, SGR, ndege, mwendokasi, ninayoikumbuka kwa haraka.
 
Wakati ujenzi wa bwawa la Mwalimu Nyerere unaanza, watetezi wake walikuwa wanatoa mishipa ya shingo kuwa bwawa hilo likianza kazi umeme utashuka bei. Nikawa nasema miaka yote tumekuwa tukitumia umeme wa maji, lakini hatukuwahi kuwa na sifa ya umeme wa bei rahisi, maana sababu ya umeme kuwa ghali hapa nchini haiendani na gharama za uzalishaji, bali sababu nyingine kabisa.

Watetezi wakawa wanasema gharama kubwa haiwezi kupungua kwa kutumia umeme wa mafuta. Wakajiapiza umeme wa maji ukianza automatically bei itashuka.

Wakati umefika na kile nilichosema kinaonekana. Bwawa limeanza kazi, umeme unazidi kupanda bei, na kibaya zaidi bado sio wa uhakika maana mgao bado upo, hata kama sio kwa kiwango kikubwa. Kwenye hili la bei wote ni mashahidi kwa walioanza kununua umeme hivi karibuni. Na hapo bado.

Paskali Mayalla Choicevariables, Lucas Mwashamba
Wapo humu humu kapuni wamekunja mikia ka mbwa koko!
 
Kuna uzi mmoja nilichangia kuwaambia Watanzania wajiandae kulipia umeme zaidi. Watu hawakuelewa.

Juzi kuna mdau kafukua kakubali utabiri wangu.
Nakumbuka sana uzi ule. Leo watetezi kwa aibu wanasema muanzilishi hayupo ndio maana tunapigwa! Nawauliza kwenye ndege alikuwepo, mbona hakushusha nauli iwe chini ya fastjet, hawataki kurudi!

Nilisema hakuna uwezekano umeme kuwa bei nafuu maana ni fedha za mkopo, na sababu nyinginezo. Watetezi walisema ni fedha za ndani kama walivyokuwa wanalishwa propaganda!
 
Siyo kwa ccm ya huyu chura kiziwi!

Chura kiziwi anatafuta wapi pa kukamua alafu akupunguzie wewe gharama za umeme?
 
Huzuni hazikuwahi kuondoka wakati wa Magufuli, bali hakukuwa na uhuru wa kusema madhila ya wananchi, maana ilikuwa marufuku kutangaza jambo negative wakati wake. Wakati wa utawala wake hatukuwa nje ya nchi boss. Ndio maana nimekupa mfano wa nauli za ndege akiwepo, mbona hazikuwahi kushuka? Ajira hazikuwepo nk. Ni kweli alifanya project kubwa kwa mikopo, na akahakikisha media inatangaza hiyo kwa nguvu zote, lakini sio unafuu kwa maisha ya wananchi. Kikubwa alichofanya ni kupunguza kelele kwa wamachinga baada ya kuruhusu biashara holela.
No ! Hali ilikuwa na fuuu na furaha ilikuwepo ndio maana hata leo ukiweka pol ya marais wote wanne Magufuli atapata asilimia 70+ na samia hafikishi asilimia hata 10 ya kura zote.
Nchi kipindi cha Magufuli ilikuwa ina muelekeo,wananchi tulikuwa tunajua hiki ni hiki sio kile... na kwanini ni hiki.
Tulishaanza kujitambua na hata wazungu walikuwa hawaji kichwa kichwa inabidi wawaze vizuri kuleta proposal ya jambo lolote maana nchi ilikuwa inaongozwa na mtu makini.
Yule baba alikuwa mzalendo nakwambia tusingekuwa tunalalamika mambo madogo kama gharama za umeme kupanda.
Hapa shida ya sasa ni roho mbaya,mama hana huruma na wananchi wake.
 
Tatizo la Africa / Tanzania ni vipaumbele & wizi

Hii methali huwa ninaupenda.

Mfano kuna haja gani ya mkurugenzi , DC , RC katika mikoa 26 yote kutembelea gari za milioni 500+ .

Je gharama za kuhudumia hizo gari , misafara isiyo na tija , matengenezo na mafuta nani anafanya??

Ukiona hilo utajua mzigo unamuangukia mwananchi wa chini hata hicho anachokamuliwa kikitoka bado [ mafisadi/majizi] yanakitolea mate na yanakikwapua ushahidi ni upi jibu ni ripoti ya CAG!

Je ikifikia hatua matumizi ya anasa kama hayo tu ya gari tuseme watembelee gari tu za milioni 10-20 nini kitapungua ?

Pesa kiasi gani itakuwa imeokolewa kwenye gari zinazohitaji pesa nyingi kuzitunza !

Hebu fikiria hayo mamilioni yakiokolewa na kwenda kuwa "subsidized " kwenye mradi wa umeme watu wapate umeme kwa gharama nafuu utahitaji kukodi vikundi vya wasifiaji eti " Mama anaupiga mwingi"??

Juzi tu hapo tumeona vilio vya kodi ya jengo kwenye umeme imeongezeka 500/= tu imekuwa story ya siku.

Watawala hawajali maana wananchi sio kipaumbele chao na hizo gharama watawala hao hata hawajui zinalipwaje maana ni jasho la wananchi linawalipia pesa ya ununuI wa gari, bili za maji, umeme, usafiri, posho, mishahara.

Halafu baadae mtu anakuja kusema "Mama ametoa bilioni......"

Bajeti ukiona pesa za maendeleo ni kiduchu ila "matumizi mengine" ni rundo la pesa kwenye mengine humo ndio wezi wanajipakulia.

Kiufupi watawala wanaiibia nchi kwa kuwarubuni wananchi kuwa wako vizuri kwa kuwapa vitu wasivyo na uhitaji navyo huku vilivyo na uhitaji hawapewi.

Niishie hapo kwa leo.
images - 2024-07-07T203804.680.jpeg
 
No ! Hali ilikuwa na fuuu na furaha ilikuwepo ndio maana hata leo ukiweka pol ya marais wote wanne Magufuli atapata asilimia 70+ na samia hafikishi asilimia hata 10 ya kura zote.
Nchi kipindi cha Magufuli ilikuwa ina muelekeo,wananchi tulikuwa tunajua hiki ni hiki sio kile... na kwanini ni hiki.
Tulishaanza kujitambua na hata wazungu walikuwa hawaji kichwa kichwa inabidi wawaze vizuri kuleta proposal ya jambo lolote maana nchi ilikuwa inaongozwa na mtu makini.
Yule baba alikuwa mzalendo nakwambia tusingekuwa tunalalamika mambo madogo kama gharama za umeme kupanda.
Hapa shida ya sasa ni roho mbaya,mama hana huruma na wananchi wake.
Hata angepata kura 100% dhidi ya marais wengine, hiyo haimaanishi kuwa maisha wakati wake yalikuwa nafuu. Na sidhani hata angekuwepo yangekuwa na afadhali maana aliingia mikopo mingi kwa pupa inatutesa hadi sasa. Haya matozo, sijui malimbikizo ni kuwahi marejesho ya mikopo ya wakati wake.
 
Back
Top Bottom