Nakadori
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 8,778
- 21,010
Wakuu habarini za majukumu?
Ninatumaini jitihada za kujipatia mkate wa kila siku zinaendelea salama... Siku ya leo nimeitumia kwa asilimia kubwa hapa stend ya mabasi ya kwenda mkoa baada ya basi nililokuwa ninalisubiria kuchelewa kufika na hivyo nikajikuta nazoeana na baadhi ya abiria niliokuwa nimekaa nao akiwemo baba Agness na Agness mwenyewe. Agness alionekana amevaa mavazi mazuri lakini yamepoteza nuru kwa vile hayasafishwi vizuri...hata nuru yake ya ngozi nyeupe imepotea kutokana na kutoweza kujiogesha vizuri kwa umri wake mdogo, jacket la jeans alilovaa halijafuliwa pia.
Baba Agness alifika jijini akiwa na binti yake wa miaka 10 kufwatilia cheti nadhani ni cha ubatizo wa mwanae baada ya maisha kumshinda hapa jijini na kuhamia Morogoro mjini ambapo anajishuhulisha na kilimo cha bustani. Anadai alishindwa kumuacha peke yake kwani dunia imeharibika na amekuwa akisikia kila siku matukio ya kutisha kuhusu ukatili wanaofanyiwa watoto.
Katika story za hapa na pale akanieleza kwamba mama Agness alimtelekeza Agness akiwa na miaka 3 tu baada ya kumpata mwanaume ambaye wanaishi nae gongolamboto hadi leo na wamefanikiwa kuzaa watoto wengine 3. Na kazi ya malezi ya agness amekuwa akiifanya baba yake kuanzia hapo hadi leo. Anadai mama agness akikuja kumuona mwanae akiwa na miaka saba baada ya baba mtu kumtafuta kwamba wamekuja jijini ili angalau amuone mwanae. Alipokuja alimpatia shilingi mia tano kama zawadi. Baba agness mwenyewe anaonekana msela sana...
Kiuhalisia wanaume sio walezi wa watoto kulingana na maumbile yao. Sasa inakuwaje mwanamke uliyebeba mimba na ukaenda leba uje utelekeze kiumbe katika umri mdogo kiasi hicho? Mbona mama zetu walikuwa tayari kupitia mateso lakini pamoja na yote waling'ang'ana kuwa nasi hadi tukawa watu wazima?? Tulizoea kusikia wanaume ndio wanatelekeza watoto lakini siku hizi wanawake tumekuwa na roho ngumu...unalipa kisasi ambacho kinamuumiza mwanao?
Nimetamani niwe mama wa hiari wa Agness (sio mama wa kambo) ili niwe nae karibu maana anakaribia umri wa usichana na atahitaji mama wa kumshauri na kuongea nae mambo mengi yahusuyo mabadiliko ya mwili wake na mengineyo. Agness mwenyewe ni katoto kazuri sana... na kanaonekana kana upeo mkubwa sana.
Wanawake wenzangu kuliko msumbue kwenye malezi kwa kusingizia wanaume bora msizae kabisa.
Ninatumaini jitihada za kujipatia mkate wa kila siku zinaendelea salama... Siku ya leo nimeitumia kwa asilimia kubwa hapa stend ya mabasi ya kwenda mkoa baada ya basi nililokuwa ninalisubiria kuchelewa kufika na hivyo nikajikuta nazoeana na baadhi ya abiria niliokuwa nimekaa nao akiwemo baba Agness na Agness mwenyewe. Agness alionekana amevaa mavazi mazuri lakini yamepoteza nuru kwa vile hayasafishwi vizuri...hata nuru yake ya ngozi nyeupe imepotea kutokana na kutoweza kujiogesha vizuri kwa umri wake mdogo, jacket la jeans alilovaa halijafuliwa pia.
Baba Agness alifika jijini akiwa na binti yake wa miaka 10 kufwatilia cheti nadhani ni cha ubatizo wa mwanae baada ya maisha kumshinda hapa jijini na kuhamia Morogoro mjini ambapo anajishuhulisha na kilimo cha bustani. Anadai alishindwa kumuacha peke yake kwani dunia imeharibika na amekuwa akisikia kila siku matukio ya kutisha kuhusu ukatili wanaofanyiwa watoto.
Katika story za hapa na pale akanieleza kwamba mama Agness alimtelekeza Agness akiwa na miaka 3 tu baada ya kumpata mwanaume ambaye wanaishi nae gongolamboto hadi leo na wamefanikiwa kuzaa watoto wengine 3. Na kazi ya malezi ya agness amekuwa akiifanya baba yake kuanzia hapo hadi leo. Anadai mama agness akikuja kumuona mwanae akiwa na miaka saba baada ya baba mtu kumtafuta kwamba wamekuja jijini ili angalau amuone mwanae. Alipokuja alimpatia shilingi mia tano kama zawadi. Baba agness mwenyewe anaonekana msela sana...
Kiuhalisia wanaume sio walezi wa watoto kulingana na maumbile yao. Sasa inakuwaje mwanamke uliyebeba mimba na ukaenda leba uje utelekeze kiumbe katika umri mdogo kiasi hicho? Mbona mama zetu walikuwa tayari kupitia mateso lakini pamoja na yote waling'ang'ana kuwa nasi hadi tukawa watu wazima?? Tulizoea kusikia wanaume ndio wanatelekeza watoto lakini siku hizi wanawake tumekuwa na roho ngumu...unalipa kisasi ambacho kinamuumiza mwanao?
Nimetamani niwe mama wa hiari wa Agness (sio mama wa kambo) ili niwe nae karibu maana anakaribia umri wa usichana na atahitaji mama wa kumshauri na kuongea nae mambo mengi yahusuyo mabadiliko ya mwili wake na mengineyo. Agness mwenyewe ni katoto kazuri sana... na kanaonekana kana upeo mkubwa sana.
Wanawake wenzangu kuliko msumbue kwenye malezi kwa kusingizia wanaume bora msizae kabisa.