Wako wapi waliodai Tume ya Katiba haina weledi na wala si huru!??

Wako wapi waliodai Tume ya Katiba haina weledi na wala si huru!??

Nape Nnauye

MP Mtama
Joined
Dec 26, 2012
Posts
99
Reaction score
408
Ninasubiri kwa hamu kubwa kuwasikia waliosema kwa sauti kubwa nahadharani kabisa kuwa Tume ya Mabadiliko ya katiba nchini haina watu wenye weledi kwa kazi hiyo tena wakaenda mbali kuwa haiko huru tume hiyo kufanya kazi wanayotakiwa kufanya. Sasa baada ya rasimu hii natamani kuwasikia tena wakisema nakurudia maneno yale na pengine kwa kuyapigia mstari mkubwa!!
 
Ndio maana mmevamia mabaraza ya katiba kwa nguvu ili muweze kuichakachua maana ikikaa kama ilivyo mtapotezwa vibaya mno.?
 
Hofu yangu msije kuchakachua kwenye mabaraza ya katiba. Hiyo ni rasimu tu na hayo ni mapendekezo ya Tume na wananchi. Sidhani kama nyie ccm mmefurahia maoni hayo. Tungoje Bunge la Katiba loikae lijadili hayo na tuone yakibaki kama yalivyopendekezwa na si kukurupuka kuanza kusema watu kimafumbo hapa, ndugu Nape.
 
Ninasubiri kwa hamu kubwa kuwasikia waliosema kwa sauti kubwa nahadharani kabisa kuwa Tume ya Mabadiliko ya katiba nchini haina watu wenye weledi kwa kazi hiyo tena wakaenda mbali kuwa haiko huru tume hiyo kufanya kazi wanayotakiwa kufanya. Sasa baada ya rasimu hii natamani kuwasikia tena wakisema nakurudia maneno yale na pengine kwa kuyapigia mstari mkubwa!!


Tuhakikishie kuwa hutakimbia! sie sio watoto kama wewe!
 
kilicholalamikiwa nape sio tume ni mabaraza ya katiba ambayo yamejaa UCCM mkubwa na hata waliolalamika hawakulalamikia tume walilalamikia uchaguzi wa mabaraza ya katiba urudiwe na kumlalamikia mwenyekiti wa tume kwa kuruhusu uchaguzi wa mabaraza ya katiba uvurugwe
kila chama kilipeleka mjumbe wake pale acha kutoa povu kwa kitu ambacho hakikusemwa......nenda ukajipange upya uje na kingine nackia tena mna kikao cha kujadili rasimu kwani vitu vingi hamviafiki tuambie kikao lini
 
We jamaa mweupe kweli sasa unashangilia Madaraka ya raisi kuto punguzwa au kutoshitakiwa?
Unashangilia kipindi cha uraisi kuongezwa kutoka 2 kuwa 3 ? sasa hii si hatari maana tukipata Raisi kama huyu wa sasa alafu uwaambie watu atakaa madarakani kwa miaka 15, watu wanaweza kuingia msituni.
 
It might be the Devil's in details! Its just a framework lets wait, my fingers crossed!!!
 
Ninasubiri kwa hamu kubwa kuwasikia waliosema kwa sauti kubwa nahadharani kabisa kuwa Tume ya Mabadiliko ya katiba nchini haina watu wenye weledi kwa kazi hiyo tena wakaenda mbali kuwa haiko huru tume hiyo kufanya kazi wanayotakiwa kufanya. Sasa baada ya rasimu hii natamani kuwasikia tena wakisema nakurudia maneno yale na pengine kwa kuyapigia mstari mkubwa!!

Unadhani kwa Rasimu hii ya katiba TEMBO WETU WATAPONA??
 
Ninasubiri kwa hamu kubwa kuwasikia waliosema kwa sauti kubwa nahadharani kabisa kuwa Tume ya Mabadiliko ya katiba nchini haina watu wenye weledi kwa kazi hiyo tena wakaenda mbali kuwa haiko huru tume hiyo kufanya kazi wanayotakiwa kufanya. Sasa baada ya rasimu hii natamani kuwasikia tena wakisema nakurudia maneno yale na pengine kwa kuyapigia mstari mkubwa!!
...sauti zao ndo angalau zimechangia kuleta unachokiona leo kwani lengo lenu ni dhahiri halikupenda rasimu kama hii ukizingatia mlengo mapendekezo ya chama chako...
 
Ninasubiri kwa hamu kubwa kuwasikia waliosema kwa sauti kubwa nahadharani kabisa kuwa Tume ya Mabadiliko ya katiba nchini haina watu wenye weledi kwa kazi hiyo tena wakaenda mbali kuwa haiko huru tume hiyo kufanya kazi wanayotakiwa kufanya. Sasa baada ya rasimu hii natamani kuwasikia tena wakisema nakurudia maneno yale na pengine kwa kuyapigia mstari mkubwa!!

Sikutegemea kusikia kauli hiyo kutoka kwako, nilitegemea ungepongeza tume na kidogo kujaribu kufanya analysis yako kujua wapi wameweza na wapi wameshindwa. Nilitegemea pia ungeomba waendelee kuwasimamia wananchi na kuhimili pressure kutoka kwa wasioitakia mema nchi yetu. Pia nilitegemea ungetoa rai kwa watanzania kuungana katika kuhakikisha yaliyomo yanasimamiwa na kushirikiana ili kuifanya iwe bora zaidi. Kauli za majungu na kujenga mazingira ya mgawanyiko nisingetegemea zitoke kwa kiongozi mkubwa kama wewe ndani ya chama chako. Umekua mtu mzima siku hizi, jaribu kufanya au kuongea mambo yanayoendana na hadhi yako na umri wako.
 
Hapa sisi wananchi wa kawaida huku mitaani...tunaishukuru CDM...maana hatujasahau walivyoweka msimamo mpaka wakaenda IKULU kuweka mambo safi(japo vijana wako humu waliwabeza-na kusema walienda kunywa JUICE)...Na pia walivyoendelea Kuibana tume kwa nguvu, msimamo na ujasiri mpaka ikaleta hiyo rasimu inayoeleweka...lakini tutaendelea kuwaomba waendelee kukaza zaidi ili hiyo rasimu ifanyiwe marekebisho zaidi...especialy kwenye suala la kuondoa wakuu wa wilaya na mikoa...na pia kwenye madaraka ya raisi bado kidogo na uteuzi wa majaji9Na uhuru wa mahakama kwa ujumla, pamoja na swala la vyama vya siasa kuungana...na mkku nakuomba kwenye hili muweke UTAIFA mbele sio kila kitu lazima MCHAKACHUE...
 
Ninasubiri kwa hamu kubwa kuwasikia waliosema kwa sauti kubwa nahadharani kabisa kuwa Tume ya Mabadiliko ya katiba nchini haina watu wenye weledi kwa kazi hiyo tena wakaenda mbali kuwa haiko huru tume hiyo kufanya kazi wanayotakiwa kufanya. Sasa baada ya rasimu hii natamani kuwasikia tena wakisema nakurudia maneno yale na pengine kwa kuyapigia mstari mkubwa!!

Hao ndo waliosababisha i-edit*we upya. Kwaani ilitakiwa itolewe trh 7 May, na badala yke imetolewa jana.
 
Nnauye ungetulia kwanza kwa sababu wale wajumbe mliowajaza ktk mabaraza ya wilaya kwa 95% nasikia kuna maelekezo wamepewa kuhusu mambo ambayo Tume imeyaacha kwa nchi washirika yakiwepo nafasi ya mkuu wa wilaya, mkoa nk.
Pili, nini msimamo wa ccm kuhusu hayo yalitolewa kwa sasa?
 
Nape...si kwa uwezo, wala si kwa nguvu , bali ni kwa roho yangu , asema Bwana wa majeshi Zekaria 4 : 6


mix with yours
 
Ninasubiri kwa hamu kubwa kuwasikia waliosema kwa sauti kubwa nahadharani kabisa kuwa Tume ya Mabadiliko ya katiba nchini haina watu wenye weledi kwa kazi hiyo tena wakaenda mbali kuwa haiko huru tume hiyo kufanya kazi wanayotakiwa kufanya. Sasa baada ya rasimu hii natamani kuwasikia tena wakisema nakurudia maneno yale na pengine kwa kuyapigia mstari mkubwa!!

Uhuru una maana pana, usiishie kwenye urefu wa pua yako....................... look even beyond kaka
Hii rasimu bado ina vipengele vingi vya kufanyiwa marekebisho. inashangaza bado sijaona kama katiba imegusia ofisi ya CAG ambayo nayo inatakiwa iwe free independent commission ili ifanye kazi yake kwa uhuru na uweledi wa hali ya juu.
 
Ninasubiri kwa hamu kubwa kuwasikia waliosema kwa sauti kubwa nahadharani kabisa kuwa Tume ya Mabadiliko ya katiba nchini haina watu wenye weledi kwa kazi hiyo tena wakaenda mbali kuwa haiko huru tume hiyo kufanya kazi wanayotakiwa kufanya. Sasa baada ya rasimu hii natamani kuwasikia tena wakisema nakurudia maneno yale na pengine kwa kuyapigia mstari mkubwa!!
Acha hizo wewe. Bila wale kupiga kelele ingekuwa disaster. Kwani zile nyaraka kutoka kwenu za kuhamasisha viongozi wahahakishe mnashinda na zile za kupongezana zilikuwa za kughushi? Tulia kwanza. Acha mchecheto.


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Sikutegemea kusikia kauli hiyo kutoka kwako, nilitegemea ungepongeza tume na kidogo kujaribu kufanya analysis yako kujua wapi wameweza na wapi wameshindwa. Nilitegemea pia ungeomba waendelee kuwasimamia wananchi na kuhimili pressure kutoka kwa wasioitakia mema nchi yetu. Pia nilitegemea ungetoa rai kwa watanzania kuungana katika kuhakikisha yaliyomo yanasimamiwa na kushirikiana ili kuifanya iwe bora zaidi. Kauli za majungu na kujenga mazingira ya mgawanyiko nisingetegemea zitoke kwa kiongozi mkubwa kama wewe ndani ya chama chako. Umekua mtu mzima siku hizi, jaribu kufanya au kuongea mambo yanayoendana na hadhi yako na umri wako.


Uko sahihi,
Nape hajui kabisa ukubwa wa nafasi yake na kuwa anapaswa kuchagua kitu cha kuongea na mahali pa kuongea jambo hilo.
 
Hivi wewe nape umeshampata au kumfahamu baba yako?


ulizaliwa na huyo mama na baba yako wala hukuchagua kwanza, ulijikuta uko ni mtoto wao ....hakuna aliyeweza kuchagua wa kumzaa kwa iyo kumbeza mtu juu ya wazazi wake si hekima, ni ujinga, utoto na upuuzi usiolelezeka! HUENDA HUYO UNAEMDHANIA NI BABA YAKO SIO BABA YAKO
 
Ninasubiri kwa hamu kubwa kuwasikia waliosema kwa sauti kubwa nahadharani kabisa kuwa Tume ya Mabadiliko ya katiba nchini haina watu wenye weledi kwa kazi hiyo tena wakaenda mbali kuwa haiko huru tume hiyo kufanya kazi wanayotakiwa kufanya. Sasa baada ya rasimu hii natamani kuwasikia tena wakisema nakurudia maneno yale na pengine kwa kuyapigia mstari mkubwa!!

Nape Nnauye , Habari za siku mkubwa.

Kwanza hakuna aliyesema unnayoyasema hapa, ila malalamiko ni mabaraza ya katiba yaliingiliwa na makada wa CCM mmoja wapo ni mama yangu, dada yangu Asha rose Migiro na wewe. Mliwatengeneza watu wa kuingia kuyapigia kura haya maoni. Naomba utafute matamko ya wote waliopinga utajua wapi walipinga. Mpaka sasa tunapinga upatikanaji wa watu watakao jadili na kuyapitisha haya maoni. Je kweli watayakubali wakati wengi ni makada wa kuingizwa wa CCM?

Tutafurahi wengi kama mtawaelekeza makada wengi kuzingatia maoni ya watanzania.

Maoni yangu binafsi sikubaliani na uwakilishi wa wanaume na wanawake kwenye majimbo utaongeza gharama kubwa sana za kuendesha bunge. Kama nimeelewa vyema yaani kuwe na wawakilishi wa kike na kiume kwenye jimbo moja. No huu utakuwa ni mzigo kwa walipa kodi. yaani majimbo 239 yatoe wabunge 478??? come on haiwezekanai. ni wengi mno ukilingisha na uwezo wa nchi. Nilitegemea tume ingepunguza majimbo ya uchaguzi na kufikia walau 70 au 100. ya kudumu.

Nape tujadili hizi rasimu Tanzania ni yetu wote, wewe utapita, Jk atapita, Lowasaa atapita , Membe Atapita ila Tanzania bado tunayo sana, msifikiri ninyi viongozi wa sisasa mna maana sana zaidi ya maisha yetu la hasha ninyi mnatetea ajira tu hamna la maana mnalilifanya, hamtetei taifa, wananchi wala ustawi wa tanzania. hamna uchungu na uhalisia wa maisha magumu ya Mtanzania.

ndio maana hamjali kushuku kiwango cha elimu manapendekeza utumbo wa kuwaongezea wanafunzi alama. Tukishindwa kuwaandaa vijana wetu leo kwanini kesho tulalamike kuhusu huduma za afya, barabra, mahakama , waalimu wabovu?? Kama leo tunashindwa kuandaa wataalamu kwanini kesho tushangae ghorafa zikituangukia ?? Nape serikali yenu imeshindwa vibaya sana. Na ninaomba miradi yote ya viongozi walioshiriki kuuwa elimu ya nchi ife kwa ukosefu wa utaalamu labda mtajifunza. Nape leo mnafurahia kutibiwa nje na kuiuwa Muhimbili na hospitali zote za ndani, ila ukumbuke kesho mnastaafu uwezo wa kwenda nje kwa fedha za walipa kodi masikini mtakuwa hamna. Najua wote mnapigana vikumbo kutuibia ili kujaza mafedha ya kesho mkiwa nje ya siasa za kibazazi.

Ila Iko siku watanzania watadai fedha zao kwa nguvu.
 
Back
Top Bottom