Wako wapi waliodai Tume ya Katiba haina weledi na wala si huru!??


Kama si uimara wa tume na serikali iyopo madarakani basi matakwa ya wanakususasusa yangefuatwa. Tulishuhudia wakisusa bungeni, walipoona hawasikilizwi wakaamua kwenda Ikulu ambako nako mkuu wa kaya akawapa msimamo wake. Wasivyo watu wa kufikiria nini mbeleni wakatangaza kugomea mchakato wa katiba kwa sababu za kipuuzi huku wakimlazimisha professa wa watu ajitoe. Profesa kwa umakini wake akawaambia maslahi ya taifa ni zaidi kuliko maslahi ya chama. Sasa lrasimu imetoka na tumeona ilivyo na matarajio makubwa kwa wananchi tofauti na CDM walivyokuwa wakihubiri na kuwanywesha sumu wananchi. Ninawapongeza wazi wajumbe kwa kuliona kwa umakini suala la majimbo kuwa litaigawa taifa na litakuwa mwanzo wa ukabila, udini na nchi kuanza kumeguka. Kuna watu humu wanadai kuwa CCM imevamia mabaraza kwa ajili ya kuchakachua, kwa upande wangu naona ni wakosefu wa uelewa kwani kama ishu ingekuwa ni kuchakachua katiba wangeaza kabla rasimu haijatolewa ili wananchi wasijue nini kimepependekezwa na baraza. Leo hii wanaanza kuiona tume ipo makini wakati walikesha humu kwenye mitandao wakiichafua tume kuwa inatumika na hata viongozi wao wa chama kuichafua tume kupitia Bunge kuwa haina weledi. Leo hii huo weledi wanauona baada ya rasmi kuwasuta uongo wao. Hizi akili za kushikiwa sijui zitakwisha lini.
 
Hebu funguka, nepi ni kaka yako?
 

Nadhani tungeacha maswala ya kulumbana tukaijadili zaid hii rasimu ya katiba masalani kuna mambo mengi ambayo najiuliza kutokana na rasimu hii japo watu wengi wanaonekana kuifurahia lakini bado kunamaswala ya msingi ya kujiuliza
Masalani suala la kuwepo kwa serekali tatu je litatupunguzia gharama au litatuongeza gharama? Kwa sababu kutakuwa serekali tatu ya muungano yenye raisi sijui kama itakuwa na waziri mkuu pia. baraza la mawaziri la jamhuri ya muungano wa tanzania yamkini kutakuwa na baraza la mawaziri wa serekali ya zanzibar na serekali ya tanzania bara sijajua upana wa baraza la mawaziri wa serekali hizi mbili utakuwaje. Lakini pia tutakuwa na mabunge matatu, Bunge la jamhuri ya muungano, bunge la zanzibar ambalo linaitwa baraza la wawakilishi na bunge la tanzania bara. sijajua kwa upande wa bara tutakuwa na wabunge wangapi. Je sheria ya upatikanaji wa wabunge wa serekali hizi mbili ya zanzibar utakuwa sawa na wa upatikanaji wa wabunge wa muungano yaani kwa hivi sasa kwenye muungano tunazungumzia kuwa na idadi sawa ya wabunge wanawake na wanaume je kwa serekali hizi mbili sheria hii itaapply?

Swala la pili ni je ikitokea raisi wa bara masalani ametoka chadema, zanzibar ametoka CUF na Muungano ametoka CCM je itakuwaje katika suala la uongozi wa nchi ikiwa vyama vyote hivi vinaitikadi tofauti? Kwa mantiki hiyo katiba hii ingekuwa nzuri zaidi kama itaka kuwepo na serekali moja badala ya serekali tatu.
 
Ushauri Mzuri sana.

 
kumbe siku zote hizo una wapinga hujui wanaongelea nini.
daaa NAPE UNATIA HURUMA, HEBU ULIZA WALIKUWA WANAPINGA NINI.
 

be wise my brother! ulipaswa kuwaza pia kwamba inawezekana kelele zao ziliwafanya wabadili madudu mliyowalazimisha wayaandike kama rasimu ya katiba. they played their role of allerting the commission.
 
Wote hao watakuwa wanaongozwa na katiba.
 


Katiba mpya haikuwa agenda yenu CCM, so long as mliamua kuiparamia TUTAWALAZIMISHA KUANDIKA KATIBA MPYA TUNAYOITAKA WANANCHI kwa kupiga kelele mara kwa mara!!

Hii ni Rasimu tu, maeneo nyeti yaliyokuwa mbeleko ya CCM(kama vile mamlaka ya Rais,uchaguzi na tume ya uchaguzi na mengine mengi) ,tume imependekeza kuyachana na kushona upya. Mmepandikiza watu wenu katika mabaraza ya katiba
, let us wait and see what are you exactly going to do there!!. And do you think this will stop us from shouting??......We will always shout until Tanzania and Tanganyika get promising CONSTITUTION!!......Congratulation CHADEMA by leading us....but the safari is still long, keep on going....YOU HAVE OUR FULL SUPPORT!!
 
Malalamiko makubwa yalielekezwa kwenye mabara ya katiba ngazi ya kata.hasa pale jaji warioba alivyotoa maneno yaliyoonyesha weledi hafifu.lakini kama unasifia,je nini msimamo wa Chama chako cha magamba?Katika rasimu hebu zungumzia hili
  1. Kinga ya Rais,ni kwa nini imependekezwa ibaki kama ilivyo sasa?lengo ni kuendelea kuwalinda marais mafisadi.
  2. Madaraka ya Rais,kwa nini imependekezwa ibaki kama ilivyo?
  3. Mahakama,hasa Supreme court,kwa nini majaji wateuliwe na rais,hata kama watapendekezwa na tume ya utumishi wa mahakama?
 
Sijui kama anapata muda wa kufikilia maendeleo ya nchi zaidi ya ukada wake. Makelele ndio yamemtisha mwenye nyumba katoka nje bila hayo angelala tu.
 


walikuwa na hoja na sio kwamba walitamka maneno bila sababu
 
si baada ya kuambiwa kuwa hawana welewdi ndio wanakuja na rasimu kidogo inafanana na kiwango!
 

Poor you akili zako zinakutosha mwenyewe sijui haya unaeneza nini wakati hata mijadala na madai ya wananchi huyajui unaleta ushabiki wa kitoto .
 
Huyu jamaa hana tofauti na wasanii wa bongo movie kule facebook,anapost harafu anakimbia,hoja kwa hoja ndio usomi na ndio ukomavu.
 

Nape hatutaki serikali tatu hatuna uwezo huo
 
Viongozi wengine wa kisiasa bwana. Mizigo mtupu na kikwazo katika ukuaji wa maendeleo ya taifa
 

Ndugu Nape nilitegemea kupata faraja ya aina yake toka kwako kuwa rasimu imetoka na hivyo tujitahidi kuijadili na kuikosoa pale tunapoona ina tatizo na kuirekebisha kweli iwe ya watanzania na sio vyama fulani.

Ninaposoma ujumbe wako huu, Nakumbuka Mail zako na Wanamtandao wenzio juu ya kuharibu mabaraza ya katiba tena kwa makusudi na kuyageuza kuwa ya chama, Kweli naweza nikakulinganisha na Wale wachawi wanaochawia watu usiku kucha na kuuwa halafu Asubuhi yake wao ndio wakwanza kulia katika misiba kwa kuondokewa na wanajamii wenzao.
Ninaamini wewe una dini hata kama ni ya kuabudu jua, Rejea kwa mola wako na jirekebishe. Usitake kuwacheza shere watanzania, na usidhani wanafurahia kuendelea kutumia T-shirt za CCM mnazotugawia wakati wa uchaguzi bali wengine tunavaa kwa ugumu wa maisha na tunashindwa hata kununua nguo zingine.
Chonde chonde jamani hakuna atakaebaki milele, Kuweni wazalendo walau watoto wetu waje wafaidi hizi rasilimali za nchi na kuwatoa katika ufukara na ukapuku uliokithiri.
Nilitegemea kuona katika Rasimu kipengele kinachoongelea kutibiwa kwa viongozi wa nchi ndani ya nchi pamoja na kudhibiti utoroshaji wa malighafi zetu ikiwemo fedha.
Mungu tunakuachia wewe udhihirishe yaliyo vifuani mwa wanadamu na sio yale wayatamkayo kuwadhihaki waja wako.
 
Mheshimiwa Nnape Moses Nnauye,vipi sheikh mkorogo utaacha lini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…