Wakoloni walituletea dini kama kinga kwao ili watutawale

Wakoloni walituletea dini kama kinga kwao ili watutawale

habari ya hapa

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
12,791
Reaction score
8,749
Heshima kwenu mabibi na mabwana ni imani yangu kuwa hamjambo, poleni na heka heka za maisha

Km kichwa cha habari kinachojieleza hapo juu, nimeona leo nitoe dukuduku langu kuhusiana na hizi dini zilivyo tushika, na kweli tumeshikika na wametuweza na wamefanikiwa sana katika hili, na sisi pasi na kujiuliza tulikubali kuzipokea tukapumbazika, tukawaacha wakawekeza dini zao km vitega uchumi, haikutosha ili kutumaliza kabisa wakadai kuwa, dini zote za watu weusi, zikiwapo mila, desturi na tamaduni zao zote ni zamashetani.

Ndio maana adui wa maradhi, ujinga na umasikini ametuganda kwa sababu akili zetu zimedumaa, tunaendeshwa km gari bovu, hii ni kwasababu tumekubali kuwa vibaraka wa kupigania dini za watu, kupitia dini wametugawa vipande vipande, hawa watu waliotuletea dini wanadai kuwa wao ni mitume na manabii wa Mungu, shetani kwa mujibu wadini zao wanadai kuwa ana sura na maumbile mabaya eti ana mikia mingi mwenye rangi nyeusi km mwaafrika, huu ni upuuzi kabisa.

Tupo hivi tulivyo kwa sababu tuliacha mila, desturi na tamaduni zetu badala yake tukaamua kukumbatia mila na desturi za wengine. Kupitia tamaduni zao wanatudharau sasa kwa kusema kuwa mila, tamaduni na desturi zetu nitatokana na mashetani. Kwa mujibu wa dini hizi wanadai kuwa hapajawahi wala kupata kutokea kwa malaika mweusi tangu kuwapo kwa dunia,


Binafsi huwa nasema na nasema tena dini ni ujinga, tufundishwa ujinga na tumeamini ujinga na huenda waliamua kuletea dini kwa sababu kuna kifo na pengine kifo kisingekuwepo kusingekuwa na kitu dini, hebu tuache kudharauliana na kutengana sisi kwa sisi kwa sababu tu wewe wazijua mila za kiarabu na wewe wazijua mila za kizungu, turudi kwenye asili yetu, hizi dini za kiyahudi na kiarabu hazitatufikisha popote zaidi ya kuendelea kutufanya wajinga.
 
Nakuunga mkono kwa asilimia zote.

Dini ni moja ya alama ya utamaduni[Cultural element]
Ni kama ilivyo lugha, mtindo wa mavazi, mila na desturi n.k.

Sasa walipokuja wazungu, wakaanza ku-undervalue kila kilichokuwa cha mwaafrika,
Waka waambia waafrika lugha zao ndo bora zaidi, dini zao ndo bora zaidi maana zinatoka kwa Mungu tofauti na za waafrika zinazotoka kwa Shetani.
Hata majina ya waafrika yalidharaulika na kupewa yale ya waleta dini.

Dini hazikuwa na lengo la kufanya penetration ya ukoloni pekee bali kumtawala mwaafrika milele.
Dini ni aina ya utawala kama zililvyo tawala zingine.
 
Nakuunga mkono kwa asilimia zote.

Dini ni moja ya alama ya utamaduni[Cultural element]
Ni kama ilivyo lugha, mtindo wa mavazi, mila na desturi n.k.

Sasa walipokuja wazungu, wakaanza ku-undervalue kila kilichokuwa cha mwaafrika,
Waka waambia waafrika lugha zao ndo bora zaidi, dini zao ndo bora zaidi maana zinatoka kwa Mungu tofauti na za waafrika zinazotoka kwa Shetani.
Hata majina ya waafrika yalidharaulika na kupewa yale ya waleta dini.

Dini hazikuwa na lengo la kufanya penetration ya ukoloni pekee bali kumtawala mwaafrika milele.
Dini ni aina ya utawala kama zililvyo tawala zingine.
asante sana mkuu,huo ndo ukweli uliopo nyuma hizi dini, afrika ndio baba wa dunia kwa utajiri wake na ardhi nzuri yenye rutuba, ili watutawale na kuchukua kila kilicho chetu wakoloni walihakikisha wanawafundisha wa afrika kuwa Mungu hakai duniani ana makao yake mbinguni, wanatuambia watu kuwa eti ni marufuku kuhoji mambo ya dini, wanasema eti kuhoji mambo ya dini ni kumpinga Mungu maana Mungu hahojiwi, wametujaza ujinga kuwa, dunia haimilikiwi na Mungu baali inamilikiwa na shetani pamoja na vitu vyote vilivyomo, yaani utajiri wake wote, hii yote tu watu weusi tusije kujuwa kuwa Mungu ndiye mtawala wa dunia na mambo yote km tukiifahamu kweli, kwa sababu matarajio yao ya kuitawala Afrika yasingelifanikiwa.
 
asante sana mkuu,huo ndo ukweli uliopo nyuma hizi dini, afrika ndio baba wa dunia kwa utajiri wake na ardhi nzuri yenye rutuba, ili watutawale na kuchukua kila kilicho chetu wakoloni walihakikisha wanawafundisha wa afrika kuwa Mungu hakai duniani ana makao yake mbinguni, wanatuambia watu kuwa eti ni marufuku kuhoji mambo ya dini, wanasema eti kuhoji mambo ya dini ni kumpinga Mungu maana Mungu hahojiwi, wametujaza ujinga kuwa, dunia haimilikiwi na Mungu baali inamilikiwa na shetani pamoja na vitu vyote vilivyomo, yaani utajiri wake wote, hii yote tu watu weusi tusije kujuwa kuwa Mungu ndiye mtawala wa dunia na mambo yote km tukiifahamu kweli, kwa sababu matarajio yao ya kuitawala Afrika yasingelifanikiwa.
Dini na mambo yake yaliyo mengi ni uongo mtupu.

Dini zimepotosha historia ya watu duniani..... Eti Mungu ndiye aliyetenda yote.

Wanakwambia Mungu ni tajiri wa kila kitu halafu Mungu huyohuyo anahitaji kusifiwa, kuabudiwa,kutukuzwa,pamoja na sadaka kama vile fedha kutoka kwa watu,....... Mungu gani mwenyewe dhiki hivyo ???
 
Dah! Ukiwasikiliza hawa mwishowe utajuwa KAFIRI
 
Hii ni dalili ya kuchoka na maisha. Watanzania tumeanza kufa pole pole na chanzo cha kifo hicho hamtakijua kamwe. Mleta mada inaonekana anafikiri sana lkn khali mbaya ya maisha imemfikisha hapo alipo.
 
Bnafsi dini imenisaidia sana malezi yao walivyonielekeza na kunielea kiutu na kimaadili ni mtu muhimu sana ktk position yangu kama mtumishi wa umma na mwanadamu kweli ninayejiheshimu n kuwaheshimu wenzangu
 
asante sana mkuu,huo ndo ukweli uliopo nyuma hizi dini, afrika ndio baba wa dunia kwa utajiri wake na ardhi nzuri yenye rutuba, ili watutawale na kuchukua kila kilicho chetu wakoloni walihakikisha wanawafundisha wa afrika kuwa Mungu hakai duniani ana makao yake mbinguni, wanatuambia watu kuwa eti ni marufuku kuhoji mambo ya dini, wanasema eti kuhoji mambo ya dini ni kumpinga Mungu maana Mungu hahojiwi, wametujaza ujinga kuwa, dunia haimilikiwi na Mungu baali inamilikiwa na shetani pamoja na vitu vyote vilivyomo, yaani utajiri wake wote, hii yote tu watu weusi tusije kujuwa kuwa Mungu ndiye mtawala wa dunia na mambo yote km tukiifahamu kweli, kwa sababu matarajio yao ya kuitawala Afrika yasingelifanikiwa.
'Ukiijua kweli, nayo kweli itakuweka huru'. Entry point ya wazungu/waarabu kwa Afrika ilisaidiwa na kufanikishwa kupitia dini. tulipumbazwa na tunaendelea kupumbazwa kupitia dini tulizoletewa na kudharau na tunaendelea kudharau mila na tamaduni zetu ambapo tunatoa fursa kwa wageni kuendelea kunyonya mali zetu mpaka damu zetu. Afrika ndio asili ya ubinadamu (Binadamu wa kwanza aliishi Afrika). Ustaarabu na elimu vilianzia Afrika (falme za songai na mwanamtapa na uwepo wa piramids) ambapo kwa wakati huo nchi za ulaya hazikuwanavyo. Siraha (physical) haina madhara makubwa sana ukilinganisha na madhara yaletwayo na 'deception'(upotoshwaji wa kifkra). Kwa miaka zaidi 300,000 Afrika na waafrika tumelishwa uongo na tunaendelea kulishwa uongo na kuuamini na tunaelekea kupoteza mwelekeo ukilinganisha na jamiii zingine duniani na hii pamoja na mambo mengine inachangiwa na namna tunavyo practice dini tulizoletewa na wala sisemi eti Mungu hayupo Mungu yupo kwani waafrika walimjua hata kabla ya ukoloni.

Leo hii tunaaminishwa kwamba wayahudi waliopo pale Israel (akina Natanyahu) eti ndio wale wanaosemwa kwenye Biblia na kwamba eti Yesu alikuwa mzungu this is deception. Tufikirie kwa makini ni watu gani walipelekwa utumwani kwa miaka kede kede? na huko walikopelekwa wakafanyishwa kazi na nchi hizo zikainuka na kuwa mataifa makubwa je, ni wayahudi wa leo au ni waafrika?? Je, wakati wa utumwa pale misiri ni watu gani walikuwa watumwa???? wayahudi wa leo au waafrika"". Anwal Sadat raisi wa zamani wa misiri aliwakataa wayahudi wa leo kuikalia palestina akidai kwamba hawawezi kukaa pale kwani waliondoka misiri wakiwa watu 'weusi' na wamerudi wakiwa weupe (wazungu). Hitler wakati akitekeleza maangamizi kwa wayahudi alisema wao sio wale waliotamkwa ndani ya biblia bali waliotamkwa ni 'Niggroes'. Biblia inasema ' watachukuliwa utumwani na watatawanyika pande zote za dunia na itafika wakati watadai kurudi kwenye nchi ya ahadi na hapo watakaporudi amani itatamaraki. Swali la kujiuliza watu gani walichukuliwa utumwani na kutawanyika pande zote za dunia?? wayahudi au watu weusi?? kwa watu weusi angalia nchi kama marekeani, uingereza, ubeligiji, visiwa vya carribeani na baadhi ya visiwa vya asia na asia yenyewe. Je wayahudi wa leo baada ya kurudi kwenye nchi yao ya ahadi amani imetamaraki???? Leo tunaaminishwa kupitia dini zetu kwamba wayahudi wa leo wamebarikiwa na hakuna taifa lolote linaloweza kuwasumbua na kumbe tunasahau ukweli kwamba wale ni vipandikizi vya marekani na uwezo wao wote wanaitegemea marekani na marekani aliwapandikiza pale kupunguza threats kutoka nchi za kiaarabu. Wakristo kila siku tunaenda kuhiji kwa Natanyahu tukiamini kwamba ndio wateule kumbe tumelishwa uongo kwa miaka kede kede na uongo huo umegeuka kuwa ukweli.
 
Bnafsi dini imenisaidia sana malezi yao walivyonielekeza na kunielea kiutu na kimaadili ni mtu muhimu sana ktk position yangu kama mtumishi wa umma na mwanadamu kweli ninayejiheshimu n kuwaheshimu wenzangu
This is just a fraction ukilinganisha na madhara yaliyosababishwa na dini za wakoloni. Rais wa zamani wa Kenya Mzee Jomokinyatta aliwahi kusema ' Wakoloni walikuja na Biblia mikononi, na wakaomba tufumbe macho kumwomba Mungu na tulipofungua macho tukajikuta sisi waafrika tuna biblia mkononi na wakaoloni wamechukua ardhi yoote''.
 
Hii ni dalili ya kuchoka na maisha. Watanzania tumeanza kufa pole pole na chanzo cha kifo hicho hamtakijua kamwe. Mleta mada inaonekana anafikiri sana lkn khali mbaya ya maisha imemfikisha hapo alipo.
Mleta mada amezungumzia ujio wa dini za kigeni na matokeo yake kwa waafrika. Hakusema eti Mungu hayupo la hasha amezungumzia the way tunavyo practice ukristo au uislam ni tofauti kabisa na maandiko yanavyosema. Biblia inasema ni vigumu tajiri kuuridhi ufalme wa mbinguni lakini wakoloni hao hao ndio walitukataza kumiliki mali wao kwa njia ya hadaa wakitwaa migodi ya madini, wakimiliki mashamba makubwa ya katani, chai, pamba , cocoa n.k na kuwafanyisha kazi babu zetu ama kwa ujira mdogo au bila ujira wowote. Biblia inasema jiwekeeni hazina kubwa mbinguni ambapo hakuna kutu wala nondo waharibuo hayo tuliambiwa na wakoloni kwa upande wao mali zote walizochuma walizihamishia kwao kujenga miuundo mbinu ya gharama tunayoiona sasa hivi kama reli, barabara, viwanda vikubwa vikubwa na majumba ya kifahari halafu. Lakini mbali na wakoloni hao hata Maaskofu na wachungaji wetu wa leo wanafanya hayo hayo yaliyofanywa na wakoloni. Ona maisha yasiyosemekana ya baadhi ya watumishi wa Mungu kumiliki vitu vya thamani kubwa kama magari ya kifahari ya Hama, chopa, mashamba makubwa na biashara kubwa huku waumini wao wakiambiwa mali na vito vyas thamani havitakufikisha mbinguni.
 
MAULANA MOLA WANGU RHABUKA TUONGOZE NA KUTUBARIKI SISI NA VIZAZI VYETU NA NCHI YETU TANZANIA MILELE YOTE AMEN RA
 
Hawa wakoloni walitumia njia ya dini ili kutufunga akili zetu kwa sababu ukiuliza maswali magumu kuhusu bibilia wanadai unamkufuru mungu lakini bibilia inajipinga yenyewe sasa inabidi walete nyingine mpya.
 
Mleta mada ametaka kujadili jambo ambalo kimsingi naliona lina tatizo.Kwanza nadhani anazungumzia dini za Uislam na Ukristo,mimi ni Mkristo hivyo nitauzunumzia Ukristo na Uislam nitaachana nao kwakuwa haunihusu.....

Mleta mada kwa nionavyo mimi anakosea anapohusisha utamaduni wa Wazungu na Ukristo [anaposema tumeacha mila zetu na kukumbatia mila za wazungu akimaanisha na Ukristoi ni utamaduni wa wazungu].Kwanza anapaswa ajue tu kwamba hata wazungu anaowasema walipelekewa huo Ukristo na siyo wao na wala siyo utamaduni wao na Ukristo haujabeba utamaduni wa wazungu wowote wale.....

Unaposema utamaduni unakuwa unataja vitu muhimu vinavyobeba utamaduni ambavyo ni...

1;Lugha
3;Mavazi
4;Na mengineyo...

Ukiangalia kati ya hayo hapo ni kwamba hakuna mahali Ukristo unalazimisha mtu kuzungumza lugha fulani tu na ndiyo maana leo tuna Biblia hadi za ki-China na Kichaga.Ukristo haulazimishi mtu yoyote kuvaa mavazi fulani ili awe Mkristo bali unasisitiza mavazi ya kuusitiri mwili,kama kuna dini zinasisitiza hayo basi hizo ndizo za kujadiliwa na siyo Ukristo.....

Pili,naomba tu mleta mada ajue kwamba Ukristo haukuletwa huku Afrika na wakoloni maana ulishakuwepo huku zamani sana na hata baadhi ya wafuasi wa Yesu kuna ambao walifika huku Afrika hivyo kudai kwamba Ukristo uliletwa na wakoloni siyo sahihi kabisa.....

Ninachokubaliana na mleta mada ni kwamba,ni kweli Waafrika tumeziacha mila zetu na tamaduni zetu na kuchukua za weupe,hili linaweza kuwa limesababishwa na baadhi ya dini lakini siyo Ukristo na kingine ambacho kinaweza kuwa kimesababisha jambo hili ni "maendeleo" na utumwa wa fikra tulio nao Waafrika....

Pamoja na hayo kuna kubwa zaidi ya hilo ambalo ni historia ya bara letu na historia ya mtu mweusi.Hili ni jambo pana sana na usipolijua utabaki kushangaa tu lakini ukilijua litakusaidia sana kujua na kupata majibu ya mswali mengi sana...

Naomba nitambue mchango mzuri wa mkuu Fugwe hapo juu kwa kuelezea baadhi ya sababu za Waafrika kuwa kama walivyo leo.Pamoja na mchango wake huo bado tunahitaji sana kujitafuta sisi watu weusi.Kila pande ya dunia mtu mweusi anasakamwa.Mtu mweusi amekuwa nembo ya yote mabaya,yeye ndiye jambazi,yeye ndiye mwenye IQ ndogo zaidi,yeye ndiye hana maendeleo,yeye ndiye anapenda ngono zaidi na meengi menmgine....

Hayo yote tumeyakubali na kujiona kuwa sisi ndiyo tunayafanya hayo wakati ukiangalia siyo kweli kabisa,hebu chukulia mfano suala la ngono tu.Nchi yenye watu wengi zaidi duniani haipatikani Afrika,sasa tunapendaje Ngono zaidi? Ukichukua idaid ya Wahindi tu kwa mfano,utaona ni wengi zaidi ya watu wote wanaoishi kwenye bara la Afrika,halafu bado tunaambiwa sisi ni wapenda ngono na sisi tunaukubali huu ujinga.Mtu mweusi kinachomponza ni ubora wake kwasababu hakuna binadamu anayeweza kuhimili hali zote za kimaisha kama mtu mweusi....

Mtu mweusi ndiye binadamui wa kwanza kuwepo hapa duniani,weupe wametoka kwenye nyeusi,hakuna nyeupe inayotoa nyeusi hata mara moja.Waisraeli kama alivyosema Fugwe hapo juu walikuwa weusi lakini hili tunaliona kama ni ujinga mkubwa wakati ni kweli kabisa....

Waisraei waliokuwa utumwani Misri walikuwa weusi,ndugu zake Yusuph wasingeshindwa kumtambua kama angekuwa ni mweupe miongoni mwa wa Misri weusi.Tuache kabisa kufikiria kwa mtindo wa wale wasiotaka amani na faraja kwa watu weusi....

Kwa maana hii niseme tu kwamba matatizo ya Afrika kama yameletwa na dini basi dini hiyo siyo Ukristo bali ni dini zingine zinazolazimisha wafuasi wao kubadili utamaduni wao na kufuata mwingine....

Lakini kwa mtazamo wangu mimi dini hizo ambazo zinalazimisha wengine kufuata utamaduni mwingine ni sehemu tu ya kilichochangia leo Afrika kuwa kama ilivyo maana sababu ni nyingi zaidi.....

Ahsante.....
 
This is just a fraction ukilinganisha na madhara yaliyosababishwa na dini za wakoloni. Rais wa zamani wa Kenya Mzee Jomokinyatta aliwahi kusema ' Wakoloni walikuja na Biblia mikononi, na wakaomba tufumbe macho kumwomba Mungu na tulipofungua macho tukajikuta sisi waafrika tuna biblia mkononi na wakaoloni wamechukua ardhi yoote''.
Hapa mkuu naona unapotoka....

Kwenye suala hili Biblia inahusikaje na udanganyifu walioufanya hawa wakoloni?

Mfano nikija na kukudanganya halafu nikakupa andazi kisha wewe ukanipa hati ya nyumba yako,andazi litakuwa linahusika namna ipi kwenye udanganyifu niliokufanyia?
 
Hizi dini nimeachana nazo tangu 1999 baada ya kutumika kwa miaka mingi. We jiulize swali dogo tu, eti mtu akifariki wanamwita mzimu! Yaan leo baba yako akifariki ndio mwisho wa kumuita baba? Akili ni zako chagua mwenyewe ila najua mwisho wa siku wataumbuka baada ya waafrika kujitambua
 
Back
Top Bottom