Wakristo tujirekebishe katika hizi nyimbo za maombolezo

Wakristo tujirekebishe katika hizi nyimbo za maombolezo

raslimali

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2014
Posts
1,958
Reaction score
1,744
Hainiingii akilini kwa nini wakristo wanaoamini kwamba Yesu ameshinda mauti lakini ikitokea mmoja wetu amefikia mwisho wa uhai wake tunakisujudia kifo badala ya kutangaza ushindi juu ya kifo. Nimekulia kwenye kanisa Katoliki na hizi nyimbo za maombolezo zinanitia kisirani kabisa. Fikiri wimbo wenye maneno kama haya za kuudhalilisha ushindi wetu dhidi ya kifo:

- SHUKA LANGU NA BLANKETI LANGU NI UDONGO MZITO, WANIELEMEA
Kweli kabisa? seriously? Maiti anaelemewa na udongo uliomfukia? Akili ya wapi hii ya kuongeza huzuni isiyokuwa na ukweli?

Kwa nini wakristo hatuimbi nyimbo za ushindi juu ya kifo kama tunavyoahidiwa katika imani yetu? Nawasihi sana hasa kanisa katoliki jirekebisheni kwenye hili. Nyimbo hizo zinaongeza huzuni badala ya kuleta faraja kwenye msiba.
 
Sio hapo tuu error ni nyingi ambazo ubinadamu umeingia
 
Taja jina la wimbo na mtunzi wa wimbo, kwaya iliyoimba huo wimbo plus mpiga kinanda, bila kufanya hivyo hii mada yako haina maana huna tofauti na yule aliekua akimlaumu Yusuph Bakhresa na salamu za Christmas
Kama theme ya uzi wangu hujaielewa sina haja ya kukidhi matakwa yako.
 
Wakati wa msiba ni msiba tu mkuu hata makanisa mengine wanavitabu vya nyimbo za maombolezo.
Then ufufuko wa Yesu hauna maana yoyote. You nullify the word of God for the sake of your own tradition. Huo ni upumbavu na Yesu aliukemea sana.
 
Una matatizo kwenye kufikiri.Usiuchukulie wimbo kwa namna unavyowaza.Kila neno linalowekwa huwa lina maana zaidi ya unavyoliona na kulitafsiri.Jifunze kuhusu fasihi kwa ufasaha.Kama unataka kwenda makanisa ya walokole weye nenda.Usitafute vijisababu.
Vema. Nipe maana halisi ( the conveyed message) ya maneno hayo niliyoyaweka kama mfano tu.
 
Mkuu nimebaini kwamba wewe ni mlokole, Ila unawasemea wakatoliki acha hizo basi semea wanaokuhusu kuna Rose Muhando juzi katoa Hit Song kwanini usiizungumzie?!,
Mkuu mimi si mlokole. Mimi ni mfuasi wa Yesu wala sina institutional affiliation yoyote na haya madhehebu ya kikristo ( labda utashangaa na kuniuliza) japo nimezliwa na kukulia kwenye imani katoliki na kujifunza Theolojia (Theology) ya kikatoliki. Kama una la zaidi sema.
 
Mkuu mimi si mlokole. Mimi ni mfuasi wa Yesu wala sina institutional affiliation yoyote na haya madhehebu ya kikristo ( labda utashangaa na kuniuliza) japo nimezliwa na kukulia kwenye imani katoliki na kujifunza Theolojia (Theology) ya kikatoliki. Kama una la zaidi sema.
Umezaliwa,kukulia na kujifunza teolojia ya kikatoliki halafu hujui kuchambua maudhui ya nyimbo za kikatoliki?🤔🤔🤔🙄🙄🙄
 
Yanakuhimiza kunyenyekea na kuwa mwema ili adhabu za dhambi uziepuke.Siyo uzito wa udongo na giza.😂😂😂😂
Unaokolewa kwa neema au kwa matendo? Labda hapo mtizamo wetu unaweza kutofautiana na sitakulaumu kwa hilo mkuu
 
Mkuu mimi si mlokole. Mimi ni mfuasi wa Yesu wala sina institutional affiliation yoyote na haya madhehebu ya kikristo ( labda utashangaa na kuniuliza) japo nimezliwa na kukulia kwenye imani katoliki na kujifunza Theolojia (Theology) ya kikatoliki. Kama una la zaidi sema.
Sawa Asante kwa maelezo mkuu, leta vielelezo taja jina la wimbo, mtunzi, kwaya na mpiga kinanda
 
Back
Top Bottom