Wakristo tujitafakari upya taratibu zetu zote za mazishi. Kuna mambo hayako sawa

Wakristo tujitafakari upya taratibu zetu zote za mazishi. Kuna mambo hayako sawa

Naomba kuuliza wakristo wenzangu kuhusu taratibu za msiba. Akifariki mtu wa kawaida basi Padre tu husimamia ibada. Lakini akifariki mtu maarufu au tajiri basi huja Askofu tena akiwa na viongozi wengine kuendesha hiyo ibada.

Kwanini Askofu asiendeshe hiyo misa hata angalau kwa msiba wa kapuku mmoja ili kuondoa hii hali ya kuonekana Askofu yuko kwa ajili ya watu fulani tu?

Kimsingi kama itawezekana Wakristo tujitafakari upya taratibu zetu zote za mazishi. Kuna mambo hayako sawa.
Karibuni tuchangie

Aliyenacho anaongezewa na asiyenacho ndio hivyo tena. Hata hivyo kuzikwa ma maaskofu sio mtaji wa kupata wepesi huko mbele ya safari. Tuishi maisha mema ya kumpendeza Mungu ili iwe mtaji wetu
 
Wakubwa wanazikana bana shida nini? Hatuwezi kuwa wote sawa ndio maisha yalivyo utake au usitake.
 
Naomba kuuliza wakristo wenzangu kuhusu taratibu za msiba. Akifariki mtu wa kawaida basi Padre tu husimamia ibada. Lakini akifariki mtu maarufu au tajiri basi huja Askofu tena akiwa na viongozi wengine kuendesha hiyo ibada.

Kwanini Askofu asiendeshe hiyo misa hata angalau kwa msiba wa kapuku mmoja ili kuondoa hii hali ya kuonekana Askofu yuko kwa ajili ya watu fulani tu?

Kimsingi kama itawezekana Wakristo tujitafakari upya taratibu zetu zote za mazishi. Kuna mambo hayako sawa.
Karibuni tuchangie
Madaraja ya Bindamu yalikuwepo hata wakati wa Mitume.Ukuu unaishia hapa duniani ,Usawa utakuweko tutakaporejea kwa Muumba wetu.kwenye Hukumu ya Haki.
 
Mkuu lazima ukalubali tu kwamba hats huko mbinguni lazima kuna classes isitoshe hapa duniani ??? Ila yote kwa yote mwisho wa ujanja wa mwanadamu ni hapo mwenye kulamba udongo.
 
Jimbo katoliki la Dsm lipo chini ya Askofu mkuu mwandamizi Baba askofu Ruwaichi Yuda Thadei
Mkuu usiseme tu Jimbo katololiki la Dsm. Sema Jimbo KUU katoliki la Dsm. Nafikiri kuna utofauti Mkubwa kati ya Jimbo na Jimbo Kuu kwa imani ya Kikristo ya Kikatoliki. Niko tayari kurekebishwa.
 
Mkuu usiseme tu Jimbo katololiki la Dsm. Sema Jimbo KUU katoliki la Dsm. Nafikiri kuna utofauti Mkubwa kati ya Jimbo na Jimbo Kuu kwa imani ya Kikristo ya Kikatoliki. Niko tayari kurekebishwa.
Jimbo ni jimbo tu, nyingine mbwembwe
 
Yule Ngalekumtwa wa Iringa ndo mkuu wa Baraza la maaskofu TEC ( Sijui anaitwa Rais wa TEC/mwenyekiti)

Kwa maana hiyo ndio kiongozi wa Maaskofu wote wa Katoliki Tanzania
SI kweli.
 
Alichofanya ni kusafiri na Padre wake pamoja na wasaidizi kutoka parokia aliyokuwa anasali town hadi kijijini wakamaliza kazi. Infact,kama hakuna anayekujua kwenye haya madhehebu ni kisanga.
Nakuhakikishia 100% kwamba hakuna Padre wa Kanisa Katoliki anayeweza kuendesha hata ibada tu ndani ya Parokia nyingine bila ya ruhusa ya Paroko wa hiyo Parokia. Huenda alienda kuchukua mchungaji fulani tu, lakini kwa muundo wa utendaji wa Kanisa Katoliki HAIWEZEKANI kuleta Padre wako kimya kimya
 
Yule Ngalekumtwa wa Iringa ndo mkuu wa Baraza la maaskofu TEC ( Sijui anaitwa Rais wa TEC/mwenyekiti)

Kwa maana hiyo ndio kiongozi wa Maaskofu wote wa Katoliki Tanzania
Update bank yako ya taarifa

Baba Ngalalekumtwa sio tena Rais wa TEC
 
Peponi ndio wapi? Tuanzia hapo kwanza, binadamu ni kama mnyama au majani, jani likikauka na kuoza ni mbolea kwa mimea mingineyo.

Huko Peponi hakujai? Huo uwanja wa parapanda ikilia siupatii picha utakuwaje maana Tangia tuambiwe kuhusu akina Zinjanthropus mpaka kizazi hiki cha kina Lisu sipati picha wameishi binadamu wangapi.

Jiulize tu, Noah eti alitengeneza safina iliyobeba wanyama na viumbe wote kwa pair, Watu walimsusia akatengeneza yeye mwenyewe na Familly yake, huo uwanja walipolitegesha ilo safina from the scratch mpaka linaisha kwangu haimake sense, labda kuwe na story mbadala wake kama ile ya kula tunda mtaani tunaambiwa ni kugegedana.

Mafundisho mengi ni mind control tu hamna kitu. Sali sana utakufa tu, kuwa chinjachinja utakufa tu, toa sana sadaka bado utakufa tu. Jifunzeni wanyama pori mfano ambao nao ni viumbe wa Mungu, Simba anakula Swala na yeye akiotewa na manyamela kina fisi analiwa vizuri tu. Mungu tu ndio ataishi milele.

Usiniambie eti sisi ni bora kuliko wanyama, utakuwa umechanganyikiwa, kata miti na mimea yote itowayo Oxygen uone kama wewe ndio bora sana, ondoa nyuki uone kama wewe utatengeneza asali.

Far from mental slavery.
mkuu tukiwa duniani we must believe in something ili mambo yaende
 
Mkuu usipotoshe uma Kama huna taarifa sahihi kukaa kimya ni busara.
Mhashamu baba Askofu Ngalalekumtwa ni Askofu wa Iringa. (Rais mstaafu wa TEC)
Rais wa TEC ni Askofu Gervas Nyaisonga.
Nyaisonga ni mtu wa eagle haya Mambo haya dah....
 
Back
Top Bottom