Wakulima wa Tanzania hamko serious na Kilimo, Yaani Ng'ombe anatoa kilo 25kg za kinyesi kwa wakati mmoja na bado mnalia kwa kupanda bei mbolea ya YARA

ng'ombe mmoja kwa wakati mmoja tu anatoa kg 25, tufanye kwa hesabu ya chini kabisa, huyu ng'ombe atoe kinyesi mara moja tu kwa siku, zidisha kwa wiki, mwezi then mwaka mara idadi ya ng'ombe tulio nao nchini

Nadhani wenyeji wa eneo hilo wanaweza kutumia maji hayo kama mbadala wa mbolea kwenye mashamba yao, maana hiyo mbolea tayari ipo katika "solution form".
 
hahaha
 
Wewe umezaliwa wapi kushuhudia ng'ombe mmoja akijaza kinyesi chenye uzito wa kgs25 kwa mkupuo?

Hata tembo hawezi kujisaidia zaidi ya kg5 ama 6.

Labda kwa uzito huo ng'ombe unayemuongelea ajisaidie miezi mitatu na apatikane "boy" wa kumfukuzia kila aendako na kumkinga.

Tafiti zingine za hovyo sana, utadhani watu wanatoka sayari ya Mars na hawayajui maisha ya duniani hapa!
 
Mkuu unampinga Le Professor
 
1 Mbolea ya kinyesi haifanyi kazi sehemu zote ,
2 Ardhi ikishazoea artificial fertilizer kama za yara , huwa inajenga usugu wa kukubali mbolea za kawaida ,

Minjingu wana mbolea za bei rahisi tu, nenda kajaribu kulimia Ruvuma uone kama utapata mahindi ya uhakika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…