Wakurugenzi wa Makampuni ya Mafuta ya PUMA, Oryx, TOTAL na Lake Oil wakamatwa na Polisi kwa kuvuruga mfumo wa usambazaji!

Watapigwa faini ya mabilioni siku chache zijazo kisha wanadunda kitaa. Ni namna nyingine ya dikteta kujipatia mabilioni ya haraka haraka ambayo katika MAPATO ya serikali hayaonyeshwi.

 
Usijifanye mjuaji wewe kiazi, najua shell ni jina la kumpuni ya mafuta na watanzania tunaviita vituo vya mafuta sheli kwa sababu ya umaarufu wa kampuni hiyo. Lengo la lugha ni mawasiliano, kama vile tunavyoziita zile pikipiki za miguu mitatu bajaji.
Una akili za kike mno
 
makampuni yote yaondolewe serikali inunue na kuuza mafuta mbona kwenye ndege tumeweza huku hatushindwi pia Mkulu akiamua na kuagiza, kuna hela sana huku!!
Mambo mengine kujifurahisha tu, hizo ndege wanacheka hadharani tu hila hakuna faida.

Ndio wajiingize kwenye mafuta nchi nzima, logistic ya dawa inawashinda tu mpaka zinakosekana. Kwenda kuwaachia serikali pekee biashara ya mafuta ndani ya Tanzania ni kuchezea uchumi.
 
Kesi ziendeshwe kwa uwazi na Takukuru wafuatilie hilo jambo kwa ukaribu mkubwa
 
Biashara ya mafuta kuendeshwa na Serikali italeta shida mkanganyiko mkubwa na hilo lilimshinda nyerere mwinyi na ndipo mkapa akaamua kuifanya iwe na ushindani, Serikali wameshindwa kufufua viwanda kibao wakija kwenye mafuta lazima watavirunda sana.
 
Biashara ya mafuta kuendeshwa na Serikali italeta shida mkanganyiko mkubwa na hilo lilimshinda nyerere mwinyi na ndipo mkapa akaamua kuifanya iwe na ushindani, Serikali wameshindwa kufufua viwanda kibao wakija kwenye mafuta lazima watavirunda sana.
Hawana hizo hela wala maarifa ya kuendesha biashara ya mafuta peke yao Tanzania.

Hakuna ubaya wa wao kushiriki kwenye soko la ushindani lakini wasije na mambo yao ya ovyo mafuta ni uchumi kuchezea hiyo sector kuna madhara.
 
Kwenye mafuta waweke misingi imara ya wazi jinsi ya kuangalia bei hasa mafuta ya ndani ya Nchi kwani huwa kuna kipindi waagizaji huagiza mafuta kwa bei kubwa wanalipa kodi zote na ikija kushuka bei wakati mafuta ya awali yakiwa bado yako sokoni huathirika kwa kupata hasara kubwa, yapo mapungufu mengi kwenye mfumo wa biashara ya mafuta yafaa Serikali waunde tume maalum kuliweka sawa hilo jambo.
 
Hawana hizo hela wala maarifa ya kuendesha biashara ya mafuta peke yao Tanzania.

Hakuna ubaya wa wao kushiriki kwenye soko la ushindani lakini wasije na mambo yao ya ovyo mafuta ni uchumi kuchezea hiyo sector kuna madhara.
Hata watumishi wa Serikali hawana uelewa mzuri juu ya biashara hiyo na lazima kutakuwa na ufisadi mkubwa ni vigumu Serikali ya CCM ifanye biashara kwa ufanisi
 
Hata watumishi wa Serikali hawana uelewa mzuri juu ya biashara hiyo na lazima kutakuwa na ufisadi mkubwa ni vigumu Serikali ya CCM ifanye biashara kwa ufanisi
Jukumu la kwanza la serikali kwenye biashara ya mafuta ni kuwekeza kwenye storage facilities na pipe line network (bei ya mafuta inatakiwa kuwa sawa nchi nzima) Kwa ivyo ni jukumu kuhakikisha wanawekeza kwenye infrastructure.

We mwenzangu kuna storage yoyote ya serikali ya mafuta unaijua iliyopo Tanzania nje ya bandari?

Wao wakishaona vinaelea ndio udandia, hii nchi serikali ijufinze huko kwenye kuandaa vijana wa kesho tunahitaji akina Bashe 30 kuendana na kasi ya uwekezaji unaofanywa leo.

Sio vijana ambao kila wakikaa Nyerere tu sijui sasa hivi wanasoma vitabu gani etc with nonsense, lakini awana political agenda unataka kuifanyia nini Tanzania.
 
Ngozi nyeusi tumekuwa viumbe wa ajabu sana.
Nikiona mfanyabishara anasumbuliwa huwa naumia sana maana najua usumbufu wa kufanya biashara hapa Tanzania
Walivyoingia ktk biashara hii hawakujua kwamba kuna regulator ambaye ni Chombo cha serikali ??
Hawakukubaliana na bei ilekezi kufuatia mzigo ulinunuliwa kwa bei gani ??
 
For security reasons half of the petroleum business ifanywe na tpdc au hiyo subsidiary yao , lakini wasiingie kwa pupa , bali strategic planning lazima ifanyike , kwsnza uwepo wa storage facilities za kutosha na distribution network na kumalizia retail network kama ilibidi
Ifwact waifufue tipper , au njia nyingine ni shares za makampuni ya mafuta ziwe traded dse.
Ili kuongeza uwazi ktk hii biashara .
 
Hilo ni zengwe Jiwe anataka kupiga pesa.Hilo ni kosa la uhujumu uchumi halina dhamana. Kama kawaida wataenda kumalizana nje ya mahakama na DPP.Hapo kila mmoja lazima apigwe bilioni kadhaa.Rejea kesi za kina MD wa Vodacom na kina Deo Mwanyika!
 
Sijui kuna nini nimepita kibaigwa petrol station foleni ya kujaza mafuta kama yote.
 
Price kubwa ya mafuta ni kodi ya serikali. Kila lita 1 serikali inachukuwa kodi ya 760.
Hii issue inatakiwa ichukuliwe taratibu sana. Maana mifano ya korosho, mbaazi, sukari ni matukio ambayo yametuletea shida kubwa sana
Ina maana hiyo kodi ya serikali ni Fixed?
 
Mmmh! Mbona Total ndio sheli pekee zinazouza mafuta huku mikoani, wengine ni kama wamegoma hivi.
Total ndiyo Shell pekee zinazouza mafuta!!! Unamaanisha nini?

Ni sawa na kusema Nissan ndiyo Toyota pekee zinazosafirisha mizigo.

Total ni kampuni inayojishughulisha na biashara ya mafuta

Shell ni kampuni inayojishughulisha na biashara ya mafuta, japo hapa nchini petu ilifunga virago na kuondoka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Washtakiwe na wapewe kesi ya uhujumu uchumi na wapelekwe Segerea wakae hata mwaka. Walikuwa na kikao cha nini?. Kikao cha kutulangua?. Hawakufurahi bei ilipoteremshwa siku za karibuni. Ni nani hao katika nchi hii?.

Halafu wanafanya haya kipindi tunapoelekea kwenye kampeni. Wanataka kuingiza siasa kwenye biashara.
 
You are 100% right theoritically but practically there might be problems in some aspect of your approach.

Kwenye Oil and Gas market structure, government Taxes and levies have huge influence how the industry evolves.

Share of the market at anytime time dictates how companies will fare. You can’t compare big companies with financial resources, their ability to expand and attaining efficiency; to small independent retailers who depend on commercial banks financing to attain the same goals.

Ni hivi kuandika appropriate entry strategy ya TPDC na early positioning yao ndani ya soko kwa mazingira ya Tanzania, growth strategy yao waweze shindana na likes of current large retailers inataka report kama ya maneno 10,000 hivi.

There is a lot to look at and evaluate na mtaji ni kigezo kikubwa sana kujua unaanzia wapi based on existing market structure, wanahitaji mtu aliesomea oil and gas management. Sio mtu aliesoma sijui petroleum engineering to write such report.

Either way the more the merrier ni hivi serikali kama imeamua kuingia iingie kama independent retailers wengine kushindana, ufanisi wa kwenye sector ya mafuta unatokana na large corporates competing. Kwa nchi za wenzetu imefikia hatua small independent retailers wapo sehemu ambazo makampuni makubwa awajaona sababu ya kufika which is good maana huduma inafikia watu wengi.

Isitoshe kuwa na makampuni makubwa kuna faida nyingi wakati serikali aina hela kesho Total na Puma wanaweza ingia joint venture wajenge pipe kutoka Dar mpaka Dodoma na kufungua distribution centre kubwa si kwa faida yao tu bali vituo vya mafuta mikoa ya karibu waweze kununua kwao na ku encourage new start up businesses. Vitu kama ivyo kutokea kwakuwa ni long term investment watu wanataka stability ya policies za serikali na wafanye mambo kwa strategy zao.

Swala la energy security ni kitu kingine ideally serikali inatakiwa kuwa na storage zake za kuhifadhi mafuta yenye uwezo wa kuhudumia nchi si chini ya miezi mitatu (that is according to ‘International Energy Agency’ recommendations) kwa sasa tunauwezo wa kuhifadhi mafuta kama sijakosea ya mwezi mmoja tu. Yaani atujamaliza huku tunakimbilia kuvuruga mengine.

Hii sector yetu ya mafuta ni changa sana hakuna sababu ya kuanza kuvurugua mambo.
 
kiongozi , Magu hacheki na kima, achia tawi uliloshikilia kuwa hatuwezi mkuu kwa uongozi wa Magu kila kitu kinaenda na tukiamua tutawin na huko pia punguza kasumba mambo si kama wakati ule
 
Magu awatimue wote hao kwa kuficha mafuta bei ipande serikali itaifishe hii biashara ni chanzo kikubwa cha mapato
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…