Wakuu Kuna hii style mpya ya nyumba. Tusaidieni ufafanuzi

Style ya zamani hiyo
Iliijulikana kama Maputo style.
1. Kipindi cha joto hutaipenda.
2. Paa lake ni rahisi sana kuezuliwa na upepo mkali/kimbunga.
3. Ni vigumu kuzuia au kupunguza changamoto ya kelele za matone ya mvua hata ukiweka ceiling
4. Paa linatiririsha maji ya mvua upande mmoja kitu ambacho kama unapenda kuvuna maji ya mvua hutapata mengi
5. Wadudu hatari e.g. nyuki huingia kirahisi na kujenga
Faida:
1. Paa linatumia bati,misumari na mbao chache sana.
2. Ni rahisi sana kufanya usafi juu ya paa i.e. kuondoa takataka ziletwazo na upepo
3. Style hiyo haina complications za kitaalam e.g. Kuta zake kuhusiana na paa litakavyonekana au mkao wa paa.
4. Ni mujarabu sana kwa anayetumia solar panels kwani utaziweka juu ya paa na hivyo sio rahisi kuibiwa.
5. Ni nzuri sana kwenye maeneo yanayokumbwa na tetemeko la ardhi mara kwa mara
 
Is it more expensive than a normal design, au gharama sio za kuchangamka?
 
Ahsante kwa elaboration yako mtaalam.

Boss hapo kwenye kuta kukutana paa, kutafanyika nini ili kutengeneza kitu bora.

Je haina complications za kuvuja kama ilivyo contemporary houses?
 
Financial Analyst
 
MSUMBIJI STYLE
Walijenga wanajeshi wengi sana miaka 1980 baada ya kulipwa pesa za Ukombozi wa Msumbiji na aina hiyo ya nyumba waliiga toka huko huko Msumbiji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…