Wakuu Msaada , je Huu si uchepushaji wa Mshahara?

Wakuu Msaada , je Huu si uchepushaji wa Mshahara?

Dogo (mtoto wa Bro ) anamiezi mitatu ya Ajira Mpya bila kupokea Mshahara.

Katika jitihada za kujua nini sababu, akagundua akaunti Namba iliyowekwa kupokea Mshahara, sio yakwake .

Na anadai kwenye kureport walikua wanapeleka kilakitu Kwa Nakala ,hivo sio rahisi kusema kwamba labda aliandika namba ya kaunti mwenyewe Kwa kunikosea.

Zaidi japo sijaielewa hii imekaaje, anasema Mishahara yake inaonekana inaingia yaan kwenye Mfumo anaonekana mshahara unalipwa vizur, ila haupati yeye kwakua Akaunti namba sio yake.

Ofisi ya utumishi wamedai inawezekana wao ndio walikosea kuingiza namba hiyo.

Ushauri nilompa, nikuandika Barua Kwa DED akimuomba uchunguzi wa suala Hilo.

Je GT, Kwa scenario kama hii, sio kwamba Dogo alikua anapigwa ?? Inawezekana vipi Hazina kuruhusi mishahara kuingia katika akaunti ambayo haiendani na Taarifa za Dogo?
Je haya sio mambo ya Akaunti hewa Enzi za JPM??.


Je achukue hatua gan?.
Sema wewe ndio mhusika, nyooka kijana unaogopa nn ID yenyewe feki
 
Back
Top Bottom