koba lee
JF-Expert Member
- Sep 29, 2016
- 981
- 1,606
Hbari za muda huu wakuu,
Niende kwenye mada, kuna office moja ya kukopesha nilichukua hela kiasi cha Tsh. laki 2 kwa mwezi mmoja na ikatakiwa nilipe laki mbili na sitini,kama ikishindikana niwe natoa riba. Sasa bana nimeenda nao vizuri na ilikuwa mwaka jana mwanzoni, nimewalipa vizuri tu riba zao, sasa kafika mahali mambo yakawa magumu riba haionekani wakipiga simu wanakula sound,wakipiga tena sipatikani.
Kumbe walikuwa wananilia timing imepita miezi minne sijafanya rejesho lolote na mimi nikawa najipa moyo kua labda wamepotezea maana laki mbili kitu gani.
Leo sasa niko kazini mara simu ya mezani inaita nikapokea upande wa pili anaongea HR akanambia "come to my office as soon as possible"., chale zikanicheza nikasema potelea pote naenda maana hapakuwa na jingine la kufanya, kufka mule ofisini namkuta mshkaji mmoja na binti wa kike, nikajua ndo walewale nikajisemea kumekucha
Yakaanza maneno mengi pale mi mdogo kama sh mia hapo, nashukuru HR kidogo alikuwa upande wangu lakini mwisho wa siku inabidi niwalipe hela yote ndani ya miezi miwili ambayo malimbikizo yake ni kama mara tatu ya hela niliyochukua,haya mambo haya.Sasa hapa nawaza naanzia wapi maana hata salary yenyewe ina viraka kila mahali.
Inawezekana mliokuja leo ofisini mpo humu na mnausoma huu uzi, hela yenu nitawalipa.
Wakuu tulipe madeni ikiwezekana tukishalipa tuachane na haya mambo ya mikopo japo upande mwingine ni ngumu maana vyuma vikiumana unaanza kuhaha kila microfinance kupata mkopo.
Ni hayo tu wakuu.
Niende kwenye mada, kuna office moja ya kukopesha nilichukua hela kiasi cha Tsh. laki 2 kwa mwezi mmoja na ikatakiwa nilipe laki mbili na sitini,kama ikishindikana niwe natoa riba. Sasa bana nimeenda nao vizuri na ilikuwa mwaka jana mwanzoni, nimewalipa vizuri tu riba zao, sasa kafika mahali mambo yakawa magumu riba haionekani wakipiga simu wanakula sound,wakipiga tena sipatikani.
Kumbe walikuwa wananilia timing imepita miezi minne sijafanya rejesho lolote na mimi nikawa najipa moyo kua labda wamepotezea maana laki mbili kitu gani.
Leo sasa niko kazini mara simu ya mezani inaita nikapokea upande wa pili anaongea HR akanambia "come to my office as soon as possible"., chale zikanicheza nikasema potelea pote naenda maana hapakuwa na jingine la kufanya, kufka mule ofisini namkuta mshkaji mmoja na binti wa kike, nikajua ndo walewale nikajisemea kumekucha
Yakaanza maneno mengi pale mi mdogo kama sh mia hapo, nashukuru HR kidogo alikuwa upande wangu lakini mwisho wa siku inabidi niwalipe hela yote ndani ya miezi miwili ambayo malimbikizo yake ni kama mara tatu ya hela niliyochukua,haya mambo haya.Sasa hapa nawaza naanzia wapi maana hata salary yenyewe ina viraka kila mahali.
Inawezekana mliokuja leo ofisini mpo humu na mnausoma huu uzi, hela yenu nitawalipa.
Wakuu tulipe madeni ikiwezekana tukishalipa tuachane na haya mambo ya mikopo japo upande mwingine ni ngumu maana vyuma vikiumana unaanza kuhaha kila microfinance kupata mkopo.
Ni hayo tu wakuu.