Wakuu wa Mikoa wanapogeuka madalali wa kutangaza biashara za makampuni

Wakuu wa Mikoa wanapogeuka madalali wa kutangaza biashara za makampuni

Mkuu, kuandaa tamasha la nyama ni gharama,
Na huwezi kula bila kuliwa 🤣🤣🤣

Tamasha la land rover liliichangamsha Arusha,

Tamasha la nyama litaichangamsha Dar, litaleta ajira, litaleta kodi nk,
Usiangalie utakosa nn, angalia utapata nn?
Mkuu ni kama nakuelewa; basi tusaidie kwa takwimu, Ajira za Moja kwa Moja za kudumu na za muda mfupi ambazo tukizipeleka NBS Wizara husika inaweza kuliambia bunge kwamba kazi Ile imechagia kuleta Ajira nvhini na kwahiyo viongzi kama hao tuwatambue kama ni wanunifu na njia ya matamasha iigwe hata na serikali kuu katika kupanua wigo wa Ajira! Na kutatua changamoto kubwa ya Ajira inayotukbali kama taifa! Ahsante
 
Balozi wa Tz uingereza aandaa tamasha, Serengeti Festival, jijini London kwa ajili ya kutangaza utalii na fursa nyingine za uwekezaji Tz vs RC wa Arusha aandaa Landrover Festival kwa ajili ya… Africans are bearly out of the bush
 
Mtoa mada jifunze kitu kwenye ishu za promotion, ili kuongeza mapato ya ndani ya halmashauri wewe umetengeneza hisia zaidi badala ya uelewa
 
If it works it's not stupid.

Mapato yaliongezeka siku hiyo na miezi ya nyuma yake wauzaji wa spare parts na mafundi walipata kazi nyingi kwahiyo ilikua ni fursa
 
Hahaha hawa wtu hawana kazi kabisa, yani Ukuu wa mkoa hata mtoto aliyemaliza darasa la saba ana umudu. Angalia wanavyoteuliwa, hakuna special skill au knowledge au ability inayohitajika. Unakuata mkuu wa wilaya ana PHD, Mkuu wa mkoa ana Degree moja. Majukumu yao hayaeleweki ni yapi hivyo wanajikuta wanayatafuta kila kukicha, yani ukienda na kesi ya ardhi, yake, ukienda na tamasha la wauza mboga lake, daladala wakilalamika lake, sijui walimu wakilala mika yeye.

Kwa kifupi, Hawana kazi ni kama Antena wao hunasa kila kinachopita mbele yao bila kujali ni majukumu yao au la, utasikia mimi ndiye mkuu wa mkoa.

Mi ningetamani tungekuwa tunachapishiwa kwenye gazeti la serikali, majukumu ya hawa wanaoteuliwa na Rais ili tuwe tuna wapima kwa wanayotakiwa kuyafanya, kuliko hivi sasa ilivyo holela holela.
 
Hauna Exposure una mawazo mgando.

Kama exposure inahusu petty issues basi ni exposure feki. Wakuu wa mikoa wanatakiwa kuwa front kwenye mambo makubwa siyo kuwa agents wa biashara za watu. Unaumiza biashara za walipa kodi wengine kwa kuwa promoter wa washindani wao wengi.

Hayo mambo ya festivals wawaachie watu binafsi kama redios na makampuni ya starehe yafanye promo. Mbona kuna Fiesta za Clouds FM toka zamani na walikuwa wakifanya promo wenyewe?
 
Juzi hapa kulifanyika tamasha la Landrover. Mkuu wa mkoa wa Arusha akapigia debe kwelikweli jambo hilo. Akatumia resources za ofisi ya umma ikiwemo wakati kupigia promo jambo hilo. Lakini hayo yakifanyika, bila shaka anatambua wazi kuwa anapigia debe kampuni ya magari ya Landrover. Hasa ukizingatia huo ni mkoa wenye vyanzo vingi vya utalii na magari hayo huingia mbugani kupeleka watalii, basi ameitangazia biashara kampuni hiyo kwa kiwango kikubwa. Sijui kama kalipwa lakini vitu rahisirahisi kama hivyo siyo kazi ya mkuu wa mkoa.

The same imetokea hapa Dar es salaam, Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam naye anautangazia umma kuwa kutakuwa na Tamasha kubwa la kula na kunywa lilioandaliwa na kampuni ya pombe ya HEINEKEN. Yaani matangzao ambayo zamani yangefanywa na redio zetu, ama watu binafsi leo ofisi ya mkuu wa mkoa ndiyo inaenda kutangazia kampuni ya pombe tamasha lao. Sasa Sijui kazi waliotumwa hawa wakuu wa mikoa ni kugeuka na kuwa madalali wa makampuni makubwa au kufanya shughuli kwa miongozo ya taratibu za kazi zao.

Zamani enzi za mwalimu wakuu wa wilaya na mikoa walikuwa wanashindana kubuni vitu kama uanzishwaji wa kilimo fulani katika maeneo yao ili kukabiliana na njaa, kuhimiza elimu ya watu wazima na watoto, kusaidia kuzunguuka na kuangalia wapi kuna matatizo kama maji na kusaidiana na wananchi kuchimba visima, kujenga madaraja etc. Ila wakuu wa mikoa wa Rais Samia wao wanatangaza bash, landrover festivals na mambo mengine madogomadogo yasiyo na tija pana kwenye equation nzima ya kupambana na umasikini, ujinga na maradhi.

Labda huenda kwa sababu bosi wao juzi wakati akihojiwa kasema Tanzania siyo masikini (kwa kuwa hata watu tunaodhani ni masikini kama vile Wahadzabe wana matunda mengi kama 30 hivi ya kula na nyama tele wakati ulaya hayo ni ghali, basi hiyo ni proof kuwa sisis siyo masikni!!!) , basi huenda wateule wake nao wananadhani kuwa kwa kuwa Tanzania siyo masikini basi kazi yao kubwa siyo kuchagiza jitihada za kupambana na umasikini. Wao changamoto yao ni namna kali zaidi ya kula bata, kuenjoy, kustarehe!. Hiyo ndiyo kazi kubwa wanaoyadhani wanayo!.
Rushwa haitakuja kuisha
 
Kama exposure inahusu petty issues basi ni exposure feki. Wakuu wa mikoa wanatakiwa kuwa front kwenye mambo makubwa siyo kuwa agents wa biashara za watu. Unaumiza biashara za walipa kodi wengine kwa kuwa promoter wa washindani wao wengi.

Hayo mambo ya festivals wawaachie watu binafsi kama redios na makampuni ya starehe yafanye promo. Mbona kuna Fiesta za Clouds FM toka zamani na walikuwa wakifanya promo wenyewe?
Mambo makubwa Tanzania ni yepi kama sio hayo yanayohusu watu moja kwa moja hizo redio hawakukatazwa kugundua wakifikiri wafanye huyu jamaa mimi simkubali ila kwenye hili nipo nae moja kwa moja Nchi masikini pamoja na watu wake mtu anakuja na vitu vya kujikwamua mnapinga mnataka nini sasa..
 
Back
Top Bottom