Walaji wa kitimoto tujuzane kijiwe kipi kizuri kwa hapo ulipo

Kumbuka ni haramu-najisi (najisi kwa kiingereza it is harmful) ina minyoo isiyokufa hata ikipikwa na ni kisababishi cha magonjwa kadhaa. Jiepushe nayo. Kula kiti moto Ni sawa na kuweka diesel kwenye gari la petrol
Etii..?
 
Alichokiumba Mungu usikiite najisi...!

Unaisi utoka ndani (moyoni) mwa mtu huko utoka uasherati, uzinzi, masengenyo, uuaji, na dhuluma, ila kiingiacho mdomoni hutoka na kutupwa chooni..!

Ila kitokacho moyoni ni kibaya zaidi ya kiingiacho mdomoni.
Ameen
 
moshi fika pale maduka ya chini barabara ya KCMC kuna kitimoto moja matata sana
 




WE BWANA NDO NINAKITENGENEZA
 
Wakuu fanyeni summary kwa mikoa basi ya huu uzi tukianzia Dodoma, Mwanza, Arusha, Dar ...n.k
 
Kilimanjaro (Boma) - Barabara ya kwenda Lawate, upande wa kushoto kuna Bar ndogo ndogo ina hii huduma.

Kilimanjaro (Mtaa wa Karanga opposite Magereza) - Kuna fundi mmoja yuko mwisho kabisa wa zile frame za biashara. Ana balaa huyu jamaa. Anatoa kitu safiii sana.

Mbeya (mjini) - Penge restaurant maeneo ya Mzumbe Uni.

Mbeya (mjini) - Barabara ya kwenda hotel za Mfikemo kuna vibanda vingiii.

Mbeya (mjini) - Chini ya Chaula Pub karibu kabisa na chuo cha mzumbe.

Arusha - Kimandolu eneo la Njia ya Ng'ombe pale kuna mtaalam kajiwekea kibanda safii.

Arusha - Mianzini mkabala na CRDb office kuna vibanda vingii.

Arusha - Mwanzo wa Barabara ya kanisa la Father babu ukitokea ALMC hospital.. karibu na mafundi wa furniture wameweka vitanda nje na makabati. Kuna Bar siijui jina. Wako vizuri sana.

Arusha - Karibu na mahakama ya Wilaya kuna bar inaitwa Apache. Huduma safi na salama.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ewaaaaa...this is wat i mean
 
DODOMA ...KWA MASISTA UASKOFUNI NI BALAA!
afu kwa Wale wanaopenda ile inayotengenezwa kwenye Vibanda umiza😀Pale Mkabala na RC NKUHUNGU Kama unaanza kuelekea Chang'ombe kuna Kina Manka Kibao na wamekubuhu katika maandalizi ya hii haramu.
Pia Mkabala na Bunge kule kwenye Vibanda vya Mama Nchimbi kuna Bar sio nzuri kivile lakini wanatengeneza kitu inachanganywa na mchicha ni hatari!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…