Wale mlioomba kazi ya Sensa ya Watu na Mmakazi naamini wote mlisoma kitabu cha Ngoswe

Wale mlioomba kazi ya Sensa ya Watu na Mmakazi naamini wote mlisoma kitabu cha Ngoswe

Tanzania Nchi Yetu Sote

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2017
Posts
505
Reaction score
872
WALE MLIOOMBA KAZI YA SENSA YA WATU NA MAKAZI NAAMINI WOTE MLISOMA KITABU CHA
NGOSWE "Penzi kitovu cha uzembe" TUNAKUMBUSHANA. HATA MIMI NIMEOMBAπŸ˜πŸ˜πŸ™ˆ
πŸ‘‡πŸ½πŸ‘‡πŸ½πŸ‘‡πŸ½πŸ‘‡πŸ½πŸ‘‡πŸ½
MITOMINGI; nadhani sasa mgeni amekwisha kumaliza kula hebu nenda kaondoe vyombo

MAMA_MAZOEA; Basi fanya haraka (Mazoea anatoka, anaenda kwa Ngoswe alipo).

MAZOEA; Hodi! Hodi!

NGOSWE; Karibu

MAZOEA; (Akiingia). Ahsante. Nimekuja kuchukua vyombo.

NGOSWE; Vyombo! Kaa basi mbona unasimama kama vile hakuna viti.

MAZOEA; Nimeambiwa nifanye haraka.

NGOSWE; Mmm! Haya ngoja ninawe basi (Ngoswe ananawa kwa taratibu jicho likiwa usoni mwa Mazoea ambaye anatazama kando). Hivo mzima wee?

MAZOEA; Bee?

NGOSWE; Salama?

MAZOEA; Salama tu.

NGOSWE; Sasa ndio umekataa kukaa?

MAZOEA; (Ajidai hakusikia) Si umekwisha maliza?

NGOSWE; Bado kidogo.

MAZOEA; Basi nitakuja chukua baadaye. (Ataka kutoka)

NGOSWE; Basi nenda navyo. (Mazoea anarudi kuinama kuvichukua. (Ngoswe kwa sauti ndogo). Hivyo waitwa nani?

MAZOEA; Mie?

NGOSWE; Ndio wewe hapo kisura.

MAZOEA; (anatabasamu huku akiondoka). Mazoea!i

Simulizi ni tamu ila tulishaambiwa ya Ngoswe tumuachie Ngoswe ! ! !

πŸ‘πŸΎπŸ‘πŸΎπŸ‘πŸΎπŸ‘πŸΎπŸ‘πŸΎπŸ‘πŸΎπŸ‘πŸΎ
 
Back
Top Bottom