Wale Tulisoma Advanced kwenye Shule za Technical

Wale Tulisoma Advanced kwenye Shule za Technical

Technical School walikua wanafaidika sana na Engineering Science kama mbadala wa Ordinary Physics
Unakuta Darasa zima linapiga A. Wakati Ordinary Physics unakutana na Abbot hizo A zinakua za manati
Ni kweli kwenye kufaulu A za kutosha kwa upande Engeering Science nadhani

ni msingi mzuri na kusoma kwa vitendo
 
Mimi ni mmoja wapo wa tuliosoma advance kwenye hizi shule za
ufundi yaani Technical Secondary School wakati Olevel nimetokea
shule ambazo sio ya ufundi.

Shule zile ni zuri sana kwa Olevel kwa sababu wana jifunza ufundi
kwa vitendo, wana karakana na mitambo ambayo inawasaidia
kupata ujuzi.

Nakumbuka ilikuwa ikitokea shida/tatizo la umeme hao Olevel
wanao soma mkondo wa umeme (Electrical) wanakuja kutatua
wakati si tunao jiita form six tupo ila tuna theory tu ya Sayansi 🤣

Wanaume wazima tunakuja kubadilishiwa taa na wadada wa
form three au form four 🤣🤣🤣
HIvyo hivyo kwa issue ya maji plumber nao wanakuja kufix.

Nakumbuka mengi sana ila mengine mtayasema nyie

Mimi nilisoma Tanga School (Tanga Technical Secondary)

The first Government Secondary School in Tanzania.

SERVICE NOT SELF

Tanga shule ya Sifa.
A level 1993 - 1995 Tanga Tech historia isiyofutika wakuu
 
Ni sawa mkuu lakini kumbuka hawaishii pale nao wanaendalea
na Advance hadi chuo kikuu ila katika hiyo level ya kabla ya kufika huko chuo kikuu

wanakuwa na uwezo wa kuslove baadhi ya mambo tofauti na
na ambao hawakusoma technical schools Olevel.
Kwa zamani ni wachache sana wanakwenda Advance, wengi walikuwa wanakwenda technical college wachache sana advance kama ilivyo kwa waliosoma shule za kawaida wachache sana walikuwa wanachaguliwa technical college

Maana tofauti ilikuwa kwenye somo moja wao wanasoma Engineering Science (physics yao) alafu huku kwingine unapiga Physics
 
Kwa zamani ni wachache sana wanakwenda Advance, wengi walikuwa wanakwenda technical college wachache sana advance kama ilivyo kwa waliosoma shule za kawaida wachache sana walikuwa wanachaguliwa technical college

Maana tofauti ilikuwa kwenye somo moja wao wanasoma Engineering Science (physics yao) alafu huku kwingine unapiga Physics
Ni kweli lakini walikuwa more practical zaidi. Ila kwa sasa nadhani ni uamuzi wa mtu.

kwenda Diploma au kwenda Advance.
 
Vijana wengi Form 6 waliotoka Technical walikua wanafeli sana tofauti na waliofanya Pure Physics, Maths & Chemistry.. ingawa walikua wanajivunia Additional Maths
Sawa sawa, na Physics sio mchezo ni kinoma kuanzia Olevel, advance ndio

balaa zaidi angalau kwa waliosoma PCM ila kwa PCB ilikuwa
ni mwiba mkali, unga'ng'ane ni Biological Sciences (BS) alafu
uje uanze tena kudill na Roger Muncaster, Chand na UP sio mchezo
 
Ni kweli lakini walikuwa more practical zaidi. Ila kwa sasa nadhani ni uamuzi wa mtu.

kwenda Diploma au kwenda Advance.
Siku hizi rahisi tu unakuta mtu katoka shule za kawaida anakwenda technical college, zamani mwanafunzi mwenyewe ndo anataka kwenda FTC mpaka na sie tusiokuwa wa ufundi tulikuwa tunawinda kwenda huko matokeo yake unajikuta umetupwa PCB na wengine PCM
 
Back
Top Bottom