1. Je, Kisheria baada ya jana Haji Manara kuitaja Kampuni ya Azam akiihusisha kuwa na Vita ya Chuki na Kampuni za Mohammed Dewji yuko salama kama aliyeguswa akitaka Kumshtaki?
2. Je, kati ya aliyekuwa CEO Magori ambaye hakuwa kumpa Mkataba wowote Haji Manara na CEO Barbara ambaye kwa mwaka mzima alimpa Mkataba wa Milioni 4 kwa Mwezi ila akawa hataki nani ni Mzuri Kwake na nani alikuwa hamthamini?
3. Katika Sheria za Ajira na Miiko ya Kazi moja wapo ikiwa ni Kutokutoa Siri za Taasisi / Kampuni hivyo basi je, leo hii kwa Mambo ya Siri (ya ndani ya Menejimenti) ya Klabu aliyoyasema Haji Manara Simba SC ikiamua Kumshtaki Mahakamani atakuwa salama?
4. Je, kati ya Haji Manara ambaye amekiri kuwa amekaa Simba SC miaka Sita (6) bila kuwa na Mkataba huku akiridhika na Hali hiyo na Klabu ya Simba ambayo haikumpa huo Mkataba ni nani ni Mjinga (Ngumbaru) na Mpumbavu (Popoma ) hasa?
5. Haji Manara mara kwa mara amekuwa akisikika akiwadhihaki na akiwadharau Waandishi wa Habari akiwaita Takataka je, Haji Manara jana kaongea na Waandishi wa Habari Takataka au Waandishi wa Habari wa Kimataifa?
6. Je, ni kweli kuwa Haji Manara ndiyo Kainyanyua Simba SC Kiumaarufu tokea ianzishwe mwaka 1936 na kwamba Yeye ndiyo ana Thamani Kubwa kuliko Wazee wote wa Simba SC ambao tena wameifia Simba kwa kujitoa Mhanga ili aikute Simba SC hii aliyoikuta Yeye? Mfano Mzee Bamchawi na Wengineo.
7. Je, kwa tabia ya Umbea na Kuropoka aliyonayo Haji Manara mpaka ya Kutoa Siri za Taasisi na Kampuni unadhani kuna Vilabu vingine au Kampuni ( Corporates ) zingine leo hii zitathubutu kutaka Kufanya Kazi nae?
Ninayasubiri sana tu Majibu yenu hapa.
1. Muachie Azam, Manara kaisifia Azam humohumo. Tumia akili kujua Azam anaijua hii press kabla hata ya jana.
2.Manara kaishasema CEO hatoi Ajira wala hawezi kuajiri. Yupo anayeajiri(sikiliza tena). Pia Hajji kasema mkataba wa abt 3M alipewa baada ya Deal ya YAKE NA aZAM (Wivu wa Mo)
3. Manar hajawahi kuajiriwa Simba Sc. Alikuwa kibarua tu.
4.Mjinga, Mpumbavu na Popoma ni Manara. Lakini Brabd yake imekuwa sana kwa miaka hiyo sita ndo maana ana mikataba minono ASAS, AZAM NA GSM
5.Hakumaanisha wote, LAKINI AMEWAOMBA RADHI MAPEMA TU JANA. hILO WAACHIE WENYEWE TAKATAKA WATAJUA CHA KUAMUA. Waandishi hawasusi kama wewe, wao wanahitaji Headlines
6. Manara hajasema kuwa yeye ni Mkubwa kuliko Simba, na hajasema kama yeye ndo kainyanyua Simba. Manara kaeleza harakati zake na jitihada zake kuipigania timu wakati wa NJAA na matukio kadhaa yaliyotukia. Akasema kama alipambana wakati wa njaa basi hawezi hujumu wakati wa mavuno. Mje mkanushe kuwa hizo jitihada hakuzifanya au alikuwa halipi tiketi zeke binafsi kusafiri na timu.
7.Manara siyo Mbeya bali ni Mropokaji kwa maana halisi ya Umbea. Kama kampuni itakuwa na tabia Mbovu za Mo na Babra sidhani kama watakubali.
Mind You , ile Press ya jana Imemvua nguo Mo. Na kwa kuogopa kuwekwa Uchi zaidi Mo akae kimya. Hajji kafagia tu Uwanja ana Mengi mpaka ya huyo BM23.
tUSUBIRI PIA sENZO NA dIAMOND pLATINUMZ WAJE WAKANUSHE ALICHOSEMA manara. Kwa ukimya wao inaonekana wazi Mo na Babra ndo Simba na Sc