Walichomfanyia jamaa yangu. Anatokwa na machozi kila anapokumbuka

Walichomfanyia jamaa yangu. Anatokwa na machozi kila anapokumbuka

Komeo Lachuma

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2014
Posts
7,926
Reaction score
17,030
Jamaa yangu tupo naye kazini kitambo sana. Si haba vijicent vipo. Shida kubwa ya jamaa ni ubabe na unyanyasaji sababu ya vijicent.

Huwa namwambia asiwe na lugha za kibabe, dharau na unyanyasaji kwa watu wa kipato cha chini. Haelewi.

Anajenga nyumba. Ashafukuza sana mafundi bila kuwalipa na matusi mengi akitishia kuwaweka ndani n.k ni jambo la kawaida kumsikia akiwaambia umaskini wenu na kukosa akili ndo kumewafanya mchague hii kazi.

Basi amejenga nyumba yake akiwalalia sana mafundi ...sana yaani kumbe nao wanajua pa kumlalia.

Leo tumeenda akakague mifumo ya maji baada ya kuunganishwa mabomba...aiseee.... Alikuwa kila akifungua bomba maji yanatokea ukutani...kumbe katika hali ya kumkomoa mafundi walikuwa wanaweka mabomba hawafikishi mwisho.

Kwa hiyo ameenda kufungua maji kwenye koki kuu...kuingia ndani anakuta kuta zinatiririsha maji tu...

Hivyo anapaswa abomoe afunge mabomba upya...Kuta zinatiririsha maji ile mbaya. Mimi kwenda gusa zaidi zile kuta aisee ....hazifai.

Yaani ukipata muda ukaanza ukuna au tekenya ukuta mchanga unamiminika chini hadi ukuta unatoboka.

Ile nyumba ina maeneo ukikaa tu kama upo idle kwa kidole tu anza kufanya kama unaukuna ukuta au fanya kama una utekenya ukuta unacheka kinyama.

Mafundi haijulikani wanakaa wapi ila nao wameshalipiza wameondoka zao.ukijua ya mbele wenzio wanajua ya nyuma.
 
Chai.
Unawezaje kumuajiri fundi na ukawa huna mawasiliano yake.
Haya mambo yanatokea sana , sio uongo

Fukara hatunzi namba ya simu kwa taarifa yako, akipoteza simu haangaiki na kurenew ananunua simu mpya na namba mpya, ndo kinachotokea kwa mafundi wengi wa ujenzi . Kuna uezekano mafundi wote alowatumia wana namba mpya.
Inashauriwa kuwa makini sana unapodeal na watu ambao hawana cha kupoteza ,
 
Nikiwaza

Utajisikiaje familia yako imeangamia kwa sababu ya mfumo mbaya wa ujenzi? Just imagine familia yako iangamie ndani ya shimo la choo!!!!🥱
Kwa maana hii hata dereva ni mtu muhimu, nawaza imagine familia yako inaangamia kwenye ajali ya bus linaloendeshwa na dereva asiejitambua.
 
Jamaa yangu tupo naye kazini kitambo sana. Si haba vijicent vipo. Shida kubwa ya jamaa ni ubabe na unyanyasaji sababu ya vijicent.

HuWa namwambia asiwe na lugha za kibabe, dharau na unyanyasaji kwa watu wa kipato cha chini. Haelewi.

Anajenga nyumba. Ashafukuza sana mafundi bila kuwalipa na matusi mengi akitishia kuwaweka ndani n.k ni jambo la kawaida kumsikia akiwaambia umaskini wenu na kukosa akili ndo kumewafanya mchague hii kazi.

Basi amejenga nyumba yake akiwalalia sana mafundi ...sana yaani kumbe nao wanajua pa kumlalia.

Leo tumeenda akakague mifumo ya maji baada ya kuunganishwa mabomba...aiseee.... Alikuwa kila akifungua bomba maji yanatokea ukutani...kumbe katika hali ya kumkomoa mafundi walikuwa wanaweka mabomba hawafikishi mwisho.

Kwa hiyo ameenda kufungua maji kwenye koki kuu...kuingia ndani anakuta kuta zinatiririsha maji tu...

Hivyo anapaswa abomoe afunge mabomba upya...Kuta zinatiririsha maji ile mbaya. Mimi kwenda gusa zaidi zile kuta aisee ....hazifai.

Yaani ukipata muda ukaanza ukuna au tekenya ukuta mchanga unamiminika chini hadi ukuta unatoboka....

Ile nyumba ina maeneo ukikaa tu kama upo idle kwa kidole tu anza kufanya kama unaukuna ukuta au fanya kama una utekenya...ukuta unacheka kinyama....

Mafundi haijulikani wanakaa wapi ila nao wameshalipiza wameondoka zao.ukijua ya mbele wenzio wanajua ya nyuma.
Kwa hiyo hiyo nyumba itundikiwe bango kuubwaa liandikwe..."SCRATCH MY BACK, I SCRATCH YOURS IN TURN"...?Atajicheki!😝😝😝😝
 
Kuna bwana mmoja alipenda kiwanja cha kwenye corner, kile kiwanja kilikua bonde la mpunga. Alinunua kwa pesa nyingi, wakati mafundi wanachimba msingi walikua wanavua pelege. Kumbe chini kuna chemi chemi.

Aliweka kifusi kingi sana cha mchanga na alijenga msingi wa nondo na zege. Maji ya chemi chemi yaliendelea kutafuta njia taratibu. Sasa hivi kuta zake zote zina unyevu nyevu na zinatoa fungus.
 
Kuna bwana mmoja alipenda kiwanja cha kwenye corner, kile kiwanja kilikua bonde la mpunga. Alinunua kwa pesa nyingi, wakati mfaundi wanachimba msingi walikua wanavua pelege. Kumbe chini kuna chemi chemi.

Aliweka kifusi kingi sana cha mchanga na alijenga msingi wa nondo na zege. Maji ya chemi chemi yaliendelea kutafuta njia taratibu. Sasa hivi kuta zake zote zina unyevu nyevu na zinatoa fungus.
Kwahiyo nyumba itaanguka au?
 
Back
Top Bottom