Walimu kuajiriwa na TSC badala ya Wizara kunaenda kutengeneza rushwa, undugu na kujuana kwenye ajira. Rais litazame hili linaenda kukuharibia

Walimu kuajiriwa na TSC badala ya Wizara kunaenda kutengeneza rushwa, undugu na kujuana kwenye ajira. Rais litazame hili linaenda kukuharibia

Ninadhani wahusika wamesikia changamoto za utaratibu mpya,lakini tuwape "benefit of doubt " waanze utekelezaji wakikwama watarekebisha utaratibu.
Si vema kuhukumu kuwa huko halmashauri za wilaya rushwa na upendeleo umetamalaki,kiasi kwamba watendaji wote wilayani wataleta ndugu zao au watapokea rushwa kuleta watu wao.
Kwa uelewa wangu, wilayani Kuna Takukuru na Usalama wa Taifa ambao wako Kyle kuhakikisha kuwa haki inatendeka na taifa linakuwa salama.

Ushauri wangu
1). Maombi yatumwe kwenye hizo tume za Walimu za wilaya kupitia mfumo wa ki Electronics.
2). wakati wa kupanga ajira ,hizi tume zishirikishe tukukuru na TISS.
3).Tamisemi iwe inatoa vigezo na miongozo ya uendeshaji wa zoezi zima.
4).Tume itakayobainika kukosa maadili ya kazi zao iwajibike Mara moja.

Manufaa ya utaratibu mpya
1).Walimu wengi watapangiwa kazi maeneo waliyoombea kazi
2).Tume ya Walimu ya Wilaya husika itakuwa inafahamu mahitaji halisi ya Walimu kwa kila shule wilayani
3). Utaratibu wa kuajiri Walimu kutoka Makao Makuu Tamisemi,mara ya mwisho,ulisababisha Mwalimu mmoja jina lake kujirudia mara 196,(unapokuwa na idadi kubwa ya Waombaji na watalaam wa IT wasio na weledi).
4). wilaya za pembezoni,nazo zitapata Walimu waliokubaliana na mazingira ya eneo hilo (itaondosha walimu wengi kutoripoti vituo vya kazi au kuomba uhamisho ndani ya muda mfupi)
 
Waziri wa nchi, ofisi ya Rais-Tamisemi ameiagiza tume ya utumishi wa walimu 'TSC' kuandaa utaratibu wa kuanza kuajiri walimu kupitia halmashauri kwa niaba ya wizara ya ofisi ya Rais-Tamisemi.

Japo utaratibu wa kuomba hizo ajira bado haujafahamika lakini nadhani maombi yatakuwa yanatumwa moja kwa moja kwenye ofisi za tume ya utumishi wa walimu(TSC) zilizopo kwenye kila wilaya.

Baada ya utaratibu huu kuanza kutumika tutarajie rushwa kuwa moja ya kigezo kwenye upatikanaji wa ajira. Maana yake kama unatokea familia duni sasa sahau kupata ajira ya ualimu.

Najua kwa sasa naweza nisieleweke lakini ukweli ndio huo kwa sababu watumishi wa TSC nao ni binadamu wana ndugu zao. Je, unadhani wataacha kuchomeka ndugu zao wakupe ajira wewe mtu baki?

Tukumbuke kuwa ofisi za TSC zipo kila wilaya kwenye majengo ya halmashauri ambako kuna watendaji na maafisa wa idara mbali mbali na hawa watu wana fanya kazi kwa ukaribu sana. Sasa tuchukulie baada ya ajira kutangazwa, mkurugenzi wa halmashauri achomeke watu wake, DC achomeke watu wake, afisa mipango achomeke watu wake, afisa utumishi achomeke mtu wake, afisa elimu achomeke mtu wake, afisa ardhi achomeke mtu wake, afisa tehama naye achomeke wakwake katika mgawanyo kama huu ajira zitaishia kuwa za watu wa halmashauri na wenye ukaribu na watumishi wa TSC kwahiyo mtoto wa mkulima hatakuwa na nafasi ya kupata ajira tena.

Pia tukumbuke baada ya ajira kurudishwa TSC kuna vigezo vipya vitaibuka moja wapo kitakuwa kigezo cha kujitolea, ufaulu, chuo ulichosoma, umri, jinsia nakadhalika. Kimsingi vigezo hivi vitawekwa kimkakati ili kutengeneza mianya ya rushwa ili kwa yoyote atakayeshindwa kuvitimiza atoe pesa ili apatiwe ajira.

Sasa kwakuwa hili ni jambo la kitaifa na linagusa maslahi ya wananchi naomba kushauri mambo yafuatayo,

1. Namuomba waziri wa Tamisemi, ummy mwalimu asitishe mchakato huu kwani unaenda kutengeneza undugu, kujuana na rushwa kwenye ajira.

2. Nashauri utaratibu unaotumika sasa kuajiri walimu uendelee kama kawaida kwani kwa kiasi fulani umesaidia kupunguza kama sio kuondosha kabisa urasimu kwenye ajira. Na katika hili napendekeza pia utaratibu uliotumika kwenye ajira zilizopita wa kutumia kigezo cha mwaka wa kuhitimu chuo ndio uendelee kwani kuna vijana wamemaliza chuo muda mrefu na wameanza kukata tamaa hata kukosa matumaini kwa serikali yao.

3. Namuomba mheshimiwa Rais mama yetu Samia aliangalie hili kwa uzito wake kwani linaenda kumchonganisha yeye binafsi na serikali anayoiongoza kwa wananchi wake.

4. Namuomba mheshimiwa Rais atafakari upya na kurudisha usimamizi wa masula ya elimu kwenye wizara husika(wizara ya elimu) kwani mapendekezo haya ya waziri ni dalili kwamba TAMISEMI imeanza kuelemewa kutokana na mzigo wa kimajukumu iliyonayo ya kuhudumia sekta nyingi kwa wakati mmoja.

5. Kwakuwa waziri wa Tamisemi, ummy mwalimu alianza vizuri na hapa kati kati ameanza kulega nilikuwa nashauri amwombe mheshimiwa Rais ambadilishie wizara kabla mambo hayajaharibika kwa sababu huku anakotaka kwenda siko.

Mwisho kabisa natoa Rai kwa ndugu wazazi na vijana mnaotarajia kuomba ajira ya ualimu kukataa utaratibu huu kwani unaenda kuwaumiza zaidi badala ya kuwaponya. Hata mimi binafsi naupinga kwa nguvu zote kwani umewahi kutumika miaka ya nyuma na rushwa ilikuwa inatembea sana ndipo serikali ikabadili utaratibu wa kuajiri sasa nashangaa leo serikali inataka kuturudisha kulekule. Katika hili tuseme HAPANA kwa sauti kubwa
Rushwa ipo siku nyingi huko TAMISEMI
 
Ummy mwalimu alifanya vizuri akiwa waziri wa afya hususani katika mapambano ya corona na alisifiwa sana!

Sasa naona sifa alizozipata akiwa waziri wa afya zimeanza kumlewesha kwa matamko yake ya hovyo hovyo yasiyo zingatia matakwa ya kisheria!

Watangulizi wake walitengeneza mfumo mzuri wa kuajiri na umekuwa na matokeo chanya licha ya changamoto za hapa na pale. Yeye amekuja sasa anataka kuubomoa aturudishe nyuma tulikotoka!

Kwangu naona ni bora akarudishwa wizara ya afya huku Tamisemi hapamfai ana haribu mno!!
Miaka 50 nyuma
 
Ninadhani wahusika wamesikia changamoto za utaratibu mpya,lakini tuwape "benefit of doubt " waanze utekelezaji wakikwama watarekebisha utaratibu.
Si vema kuhukumu kuwa huko halmashauri za wilaya rushwa na upendeleo umetamalaki,kiasi kwamba watendaji wote wilayani wataleta ndugu zao au watapokea rushwa kuleta watu wao.
Kwa uelewa wangu, wilayani Kuna Takukuru na Usalama wa Taifa ambao wako Kyle kuhakikisha kuwa haki inatendeka na taifa linakuwa salama.

Ushauri wangu
1). Maombi yatumwe kwenye hizo tume za Walimu za wilaya kupitia mfumo wa ki Electronics.
2). wakati wa kupanga ajira ,hizi tume zishirikishe tukukuru na TISS.
3).Tamisemi iwe inatoa vigezo na miongozo ya uendeshaji wa zoezi zima.
4).Tume itakayobainika kukosa maadili ya kazi zao iwajibike Mara moja.

Manufaa ya utaratibu mpya
1).Walimu wengi watapangiwa kazi maeneo waliyoombea kazi
2).Tume ya Walimu ya Wilaya husika itakuwa inafahamu mahitaji halisi ya Walimu kwa kila shule wilayani
3). Utaratibu wa kuajiri Walimu kutoka Makao Makuu Tamisemi,mara ya mwisho,ulisababisha Mwalimu mmoja jina lake kujirudia mara 196,(unapokuwa na idadi kubwa ya Waombaji na watalaam wa IT wasio na weledi).
4). wilaya za pembezoni,nazo zitapata Walimu waliokubaliana na mazingira ya eneo hilo (itaondosha walimu wengi kutoripoti vituo vya kazi au kuomba uhamisho ndani ya muda mfupi)
Huu utaratibu sio kwamba ni mpya uliwahi kuwepo miaka ya nyuma japo kwa kipindi hicho ulisimamiwa na wakurugenzi wa halmashauri. Rushwa ikawa inatembea balaa na ukitaka kupangiwa mjini unatoa hela kazi inakwisha na hii ndio ilichangia shule za mjini kuwa na walimu wengi kuliko za vijijini. Baada ya kuliona hilo serikali ikafuta huo utaratibu wa ajira ukarudishwa kuwa chini ya wizara. Kwahiyo kusema wapewe muda ni kubariki uhuni uliofanyika miaka ya nyuma kuendelea kuwatafuna watanzania. Hili halikubaliki
 
Rushwa ipo siku nyingi huko TAMISEMI
Ni kweli ipo lakini mfumo wa kielektroniki unaotumika sasa umesaidia kupunguzwa rushwa na kujuana kwenye ajira kwa kiwango kikubwa huwezi kufananisha na rushwa itakayotembea endapo utaratibu utakuwa chini ya TSC
 
Waziri wa nchi, ofisi ya Rais-Tamisemi ameiagiza tume ya utumishi wa walimu 'TSC' kuandaa utaratibu wa kuanza kuajiri walimu kupitia halmashauri kwa niaba ya wizara ya ofisi ya Rais-Tamisemi.

Japo utaratibu wa kuomba hizo ajira bado haujafahamika lakini nadhani maombi yatakuwa yanatumwa moja kwa moja kwenye ofisi za tume ya utumishi wa walimu(TSC) zilizopo kwenye kila wilaya.

Baada ya utaratibu huu kuanza kutumika tutarajie rushwa kuwa moja ya kigezo kwenye upatikanaji wa ajira. Maana yake kama unatokea familia duni sasa sahau kupata ajira ya ualimu.

Najua kwa sasa naweza nisieleweke lakini ukweli ndio huo kwa sababu watumishi wa TSC nao ni binadamu wana ndugu zao. Je, unadhani wataacha kuchomeka ndugu zao wakupe ajira wewe mtu baki?

Tukumbuke kuwa ofisi za TSC zipo kila wilaya kwenye majengo ya halmashauri ambako kuna watendaji na maafisa wa idara mbali mbali na hawa watu wana fanya kazi kwa ukaribu sana. Sasa tuchukulie baada ya ajira kutangazwa, mkurugenzi wa halmashauri achomeke watu wake, DC achomeke watu wake, afisa mipango achomeke watu wake, afisa utumishi achomeke mtu wake, afisa elimu achomeke mtu wake, afisa ardhi achomeke mtu wake, afisa tehama naye achomeke wakwake katika mgawanyo kama huu ajira zitaishia kuwa za watu wa halmashauri na wenye ukaribu na watumishi wa TSC kwahiyo mtoto wa mkulima hatakuwa na nafasi ya kupata ajira tena.

Pia tukumbuke baada ya ajira kurudishwa TSC kuna vigezo vipya vitaibuka moja wapo kitakuwa kigezo cha kujitolea, ufaulu, chuo ulichosoma, umri, jinsia nakadhalika. Kimsingi vigezo hivi vitawekwa kimkakati ili kutengeneza mianya ya rushwa ili kwa yoyote atakayeshindwa kuvitimiza atoe pesa ili apatiwe ajira.

Sasa kwakuwa hili ni jambo la kitaifa na linagusa maslahi ya wananchi naomba kushauri mambo yafuatayo,

1. Namuomba waziri wa Tamisemi, ummy mwalimu asitishe mchakato huu kwani unaenda kutengeneza undugu, kujuana na rushwa kwenye ajira.

2. Nashauri utaratibu unaotumika sasa kuajiri walimu uendelee kama kawaida kwani kwa kiasi fulani umesaidia kupunguza kama sio kuondosha kabisa urasimu kwenye ajira. Na katika hili napendekeza pia utaratibu uliotumika kwenye ajira zilizopita wa kutumia kigezo cha mwaka wa kuhitimu chuo ndio uendelee kwani kuna vijana wamemaliza chuo muda mrefu na wameanza kukata tamaa hata kukosa matumaini kwa serikali yao.

3. Namuomba mheshimiwa Rais mama yetu Samia aliangalie hili kwa uzito wake kwani linaenda kumchonganisha yeye binafsi na serikali anayoiongoza kwa wananchi wake.

4. Namuomba mheshimiwa Rais atafakari upya na kurudisha usimamizi wa masula ya elimu kwenye wizara husika(wizara ya elimu) kwani mapendekezo haya ya waziri ni dalili kwamba TAMISEMI imeanza kuelemewa kutokana na mzigo wa kimajukumu iliyonayo ya kuhudumia sekta nyingi kwa wakati mmoja.

5. Kwakuwa waziri wa Tamisemi, ummy mwalimu alianza vizuri na hapa kati kati ameanza kulega nilikuwa nashauri amwombe mheshimiwa Rais ambadilishie wizara kabla mambo hayajaharibika kwa sababu huku anakotaka kwenda siko.

Mwisho kabisa natoa Rai kwa ndugu wazazi na vijana mnaotarajia kuomba ajira ya ualimu kukataa utaratibu huu kwani unaenda kuwaumiza zaidi badala ya kuwaponya. Hata mimi binafsi naupinga kwa nguvu zote kwani umewahi kutumika miaka ya nyuma na rushwa ilikuwa inatembea sana ndipo serikali ikabadili utaratibu wa kuajiri sasa nashangaa leo serikali inataka kuturudisha kulekule. Katika hili tuseme HAPANA kwa sauti kubwa
Viongozi wa ccm huwa wanatumia kila namna kutengeneza mazingira ya rushwa ili wanufaike nayo binafsi.
 
Ninadhani wahusika wamesikia changamoto za utaratibu mpya,lakini tuwape "benefit of doubt " waanze utekelezaji wakikwama watarekebisha utaratibu.
Si vema kuhukumu kuwa huko halmashauri za wilaya rushwa na upendeleo umetamalaki,kiasi kwamba watendaji wote wilayani wataleta ndugu zao au watapokea rushwa kuleta watu wao.
Kwa uelewa wangu, wilayani Kuna Takukuru na Usalama wa Taifa ambao wako Kyle kuhakikisha kuwa haki inatendeka na taifa linakuwa salama.

Ushauri wangu
1). Maombi yatumwe kwenye hizo tume za Walimu za wilaya kupitia mfumo wa ki Electronics.
2). wakati wa kupanga ajira ,hizi tume zishirikishe tukukuru na TISS.
3).Tamisemi iwe inatoa vigezo na miongozo ya uendeshaji wa zoezi zima.
4).Tume itakayobainika kukosa maadili ya kazi zao iwajibike Mara moja.

Manufaa ya utaratibu mpya
1).Walimu wengi watapangiwa kazi maeneo waliyoombea kazi
2).Tume ya Walimu ya Wilaya husika itakuwa inafahamu mahitaji halisi ya Walimu kwa kila shule wilayani
3). Utaratibu wa kuajiri Walimu kutoka Makao Makuu Tamisemi,mara ya mwisho,ulisababisha Mwalimu mmoja jina lake kujirudia mara 196,(unapokuwa na idadi kubwa ya Waombaji na watalaam wa IT wasio na weledi).
4). wilaya za pembezoni,nazo zitapata Walimu waliokubaliana na mazingira ya eneo hilo (itaondosha walimu wengi kutoripoti vituo vya kazi au kuomba uhamisho ndani ya muda mfupi)
Wewe utakuwa ni mtumishi wa hiyo tume thus why unatetea ili upate nafasi ya kuchomeka ndugu zako kwenye ajira!
 
eti rais!

haya malamiko yenu yapelekeni kwa mkwe wake ndiyo yupo incharge.
 
Hata Sasa hivi bado inasemekana ajira zinatolewa Kwa kujuana...

Hakuna jipya pambana...
 
Ofisi za tsc zinanuka rushwa za kila aina.. ukiwa mwanaume pesa ndo pona yako na ukiwa mwanamke rushwa ya ngono itakuhusu. Makatibu wa TSc wilaya wamejitunuku Umungu mtu! Ummy aliekushauri amekupotosha!
 
Kwanini tuogope kabla... Wacha wajaribu kwanza.
Sio geni lilikuwepo na hali ilikuwa mbaya zaidi ndipo serikali ikarudisha utaratibu wa kuajiri wizarani. Sasa ukiona linataka kurudishwa tena ujue wapiga madili wamerudi kazini
 
Ofisi za tsc zinanuka rushwa za kila aina.. ukiwa mwanaume pesa ndo pona yako na ukiwa mwanamke rushwa ya ngono itakuhusu. Makatibu wa TSc wilaya wamejitunuku Umungu mtu! Ummy aliekushauri amekupotosha!
Huyu waziri kabla ya kufikia huu uamzi angefanya japo research kwa walimu kuona namna gani masuala yao ya kinadhamu yanavyoshughuliwa na hawa TSC. Ni rushwa tupu.

Tena hawa kisheria hawana mamlaka ya kuajiri ila kwakuwa ni wapiga dili ndio watakuwa wamemshauri waziri awapatie kibali cha kuajiri na waziri naye bila kufikiri akajaa mzima mzima
 
Nakubali rushwa haiwezi kuisha lakini angalau kutuma maombi kwa njia ya kielektroniki na maombi hayo kusimamiwa na wizara kulipunguza sana urasimu kwenye ajira tofauti na mfumo wanaotaka kuanzisha. Kuhusu uhitaji wa walimu kimasomo takwimu huwa zinatumwa TAMISEMI labda ni wao ndio huwa hawazifanyii kazi kwenye upangaji wa ajira
Kwani nani kasema njia ya kietronic haiwezi kutumika na TSC?
 
Back
Top Bottom