Walimu kuajiriwa na TSC badala ya Wizara kunaenda kutengeneza rushwa, undugu na kujuana kwenye ajira. Rais litazame hili linaenda kukuharibia

Walimu kuajiriwa na TSC badala ya Wizara kunaenda kutengeneza rushwa, undugu na kujuana kwenye ajira. Rais litazame hili linaenda kukuharibia

Ni sababu ipi iliyofanya OTEAS iondolewe....?? ..hili swali ni la kujiuliza mno!
Hakuna sababu maalum ila naona wameamua kubuni njia mpya ya kuchomeka ndugu zao kwenye ajira na watatumia mlango wa kujitolea ili kufanikisha adhima hiyo. Kama huamini subiri muda ufike utanambia
 
Kwani nani kasema njia ya kietronic haiwezi kutumika na TSC?
Bado haimeki sense kwa sababu tamisemi kama wizara wana facilities toshelevu na uwezo wa kusimamia hili zoezi kwa ufanisi mkubwa kuliko hicho kiidara kilichojaa wala rushwa
 
Huyu mama ummy mwalimu anapoekekea sio pazuri
Wakati anaingia alianza kufanya vizuri kwa kurekebisha makosa yaliyofanywa awamu iliyopita hasa kwa kuanza kuajiri kwa kufuata series ya miaka lakini ghafla anataka kuharibu utaratibu huu aturudishe kule kule tulikotoka
 
Rushwa na kujuana nchi hii hakuwezi kuisha. Kila nikiwaza Utumishi wanavyofanya kwa nafasi kubwa nachoka kabisa, wapuuzi wamekuja na mbinu mpya anzia mwaka jana. Nafasi zote zile nzuri na kubwa zinatangazwa ila kwenye interview hazitangazwi, watu wanaitwa kimya kimya ili waweze kuchomeka watu wao.
Mnafanya interview vizuri kabisa ila nafasi anakuja kupewa mtu ambae hakuwepo kabisa kwenye intvw. Nafasi wanatuachia tupasuane kiukweli ni za chini tu. Sasa huko kwenye walimu tunaenda kuuana tena
 
Mimi nalitazama hill swala kwa pande mbili, upande was chanya ; njia hii ikitumika itasaidia mwajiliwa kuchagua halimashauli anayopenda kufanyia kazi kuliko hivi sasa ambapo wengi hupelekwa halimashauli wasizotaka hivyo kuanza kuomba uhamisho.
Pili njia hii itasaidia kutatua tatizo la uhaba wa walimu vijijini kwa kuwa kila halimashauli itapeleka walimu sehemu yenye uhitaji mkubwa

Kwa upande wa hasi; swala la rushwa litatamalaki sana.kwakuwa hofu kubwa ni rushwa kutamalaki basi selikari ifanye yafatayo; iandae vigezo vitakavyotumiwa na tume kuajili walimu na vigezo hivyo visima miwe na selikari ,kama nikigezocha umri basi iwe hivyo isitokee mhitimu wa hivi karibuni ameajiliwa wakati wazamani wapo
 
Mimi nalitazama hill swala kwa pande mbili, upande was chanya ; njia hii ikitumika itasaidia mwajiliwa kuchagua halimashauli anayopenda kufanyia kazi kuliko hivi sasa ambapo wengi hupelekwa halimashauli wasizotaka hivyo kuanza kuomba uhamisho.
Pili njia hii itasaidia kutatua tatizo la uhaba wa walimu vijijini kwa kuwa kila halimashauli itapeleka walimu sehemu yenye uhitaji mkubwa

Kwa upande wa hasi; swala la rushwa litatamalaki sana.kwakuwa hofu kubwa ni rushwa kutamalaki basi selikari ifanye yafatayo; iandae vigezo vitakavyotumiwa na tume kuajili walimu na vigezo hivyo visima miwe na selikari ,kama nikigezocha umri basi iwe hivyo isitokee mhitimu wa hivi karibuni ameajiliwa wakati wazamani wapo
Mimi naona wizara ndio iajiri lakini kazi ya kusambaza walimu kwenye vituo vya kazi ndio ifanywe na Tsc! Unless siungi mkono ajira kusimamiwa na wala rushwa Tsc!
 
Ninadhani wahusika wamesikia changamoto za utaratibu mpya,lakini tuwape "benefit of doubt " waanze utekelezaji wakikwama watarekebisha utaratibu.
Si vema kuhukumu kuwa huko halmashauri za wilaya rushwa na upendeleo umetamalaki,kiasi kwamba watendaji wote wilayani wataleta ndugu zao au watapokea rushwa kuleta watu wao.
Kwa uelewa wangu, wilayani Kuna Takukuru na Usalama wa Taifa ambao wako Kyle kuhakikisha kuwa haki inatendeka na taifa linakuwa salama.

Ushauri wangu
1). Maombi yatumwe kwenye hizo tume za Walimu za wilaya kupitia mfumo wa ki Electronics.
2). wakati wa kupanga ajira ,hizi tume zishirikishe tukukuru na TISS.
3).Tamisemi iwe inatoa vigezo na miongozo ya uendeshaji wa zoezi zima.
4).Tume itakayobainika kukosa maadili ya kazi zao iwajibike Mara moja.

Manufaa ya utaratibu mpya
1).Walimu wengi watapangiwa kazi maeneo waliyoombea kazi
2).Tume ya Walimu ya Wilaya husika itakuwa inafahamu mahitaji halisi ya Walimu kwa kila shule wilayani
3). Utaratibu wa kuajiri Walimu kutoka Makao Makuu Tamisemi,mara ya mwisho,ulisababisha Mwalimu mmoja jina lake kujirudia mara 196,(unapokuwa na idadi kubwa ya Waombaji na watalaam wa IT wasio na weledi).
4). wilaya za pembezoni,nazo zitapata Walimu waliokubaliana na mazingira ya eneo hilo (itaondosha walimu wengi kutoripoti vituo vya kazi au kuomba uhamisho ndani ya muda mfupi)
Tume ya walimu ujinga huu
 
Kati ya tume za hovyo zinazopaswa kufumuliwa ni tume ya walimu...!

Tume imejaa vibibi vina roho mbaya kichizi halafu vinajifanya vina maadili kumbe vipiga madili vikubwa..nyambafu kabisa..
 
Back
Top Bottom