Walimu Shule ya Msingi Chanika, acheni kuwafungia darasani watoto wasiotoa mchango wa chakula

Walimu Shule ya Msingi Chanika, acheni kuwafungia darasani watoto wasiotoa mchango wa chakula

Ninachojua shule hakuna chakula kizuri,kitamu,kibichi wala kilichoiva. Au kwasababu hyo shule ipo daslam?
 
Kwani maana ya kuchangia ni nini? Si ni pamoja na kununua kuni, chakula na mpishi?

Kinachozungumzwa hapa ni chakula kilichopikwa na mpishi kwa kutumia kuni kwa michango ya wanafunzi lakini ni chakula kibaya, kinachopekelekea watoto wasikipende na kuamua kwenda kununu chakula nje, kitendo ambacho kimewaudhi hao waandaji wa chakula na kuwafungia madarasani.
Sasa haya malalamiko yako ya watoto kula chakula kibichi, si ungeyapeleka huko shule ili hiyo kasoro irekebishwe?

Au unataka tukufahamu ya kuwa una uwezo wa kumpa mtoto wako hela ya kununulia chakula tofauti na hicho kinachopikwa shule?
 
Katika hali isiyotarajiwa wanafunzi wameanza kupata shida mashuleni.

Iko hivi, baada ya Serikali kutoa mwongozo kwa ajili ya watoto wetu kula chakula mashuleni hali imekuwa tofauti kabisa.

Watoto wanalalamika kuwa chukula wanachopewa ni kibaya, wameenda mbali na kusema wakati mwingine kinakuwa kibichi. Kutokana na hali hiyo watoto wengi hawatoi pesa ya mchango wa chakula wanyopewa na wazazi wao na kuamua kununua kile wanachokitaka.

Sasa hili la kutotoa hela ya chukula na kuamua kununua chakula nje ya shule, wanafunzi wa shule ya Msingi CHANIKA kufungiwa darasani kwa wale wasiotoa hela ya chakula muda wa mapumziko na kuambiwa kwa lugha kali kuwa endapo watakuwa hawatoi pesa hata shule watafukuzwa.

Je, huu ndio mwongozo wa serikali uliyotolewa?
Aisee
 
Ninachojua shule hakuna chakula kizuri,kitamu,kibichi wala kilichoiva. Au kwasababu hyo shule ipo daslam?
Yani mkuu wazazi wa kipindi hiki wanamalezi mabovu kweli kwel sisi tumesoma boarding huko tumekula vibichi matumbo yakauma na tumepona tuko hapa leo
 
Lipa hio pesa acha usumbufu, bila ubandidu kama huo watu hamtatoa michango. Nawapongeza walimu, washikilie hapo hapo, mana mlikubaliana wenyewe kwenye vikao vya wazazi hio michango.

Kama hutaki wanao wale hicho chakula, toa mchango kisha uwe unawapa pesa ya kula chakula chao.
Kwakuwa hela zinaokotwa ....
 
Uko sahihi.wasio kuelewa ni wale wasiojali.Wenzetu ngozi nyeupe zinajali sana malezi ya vizazi vyao ndio maana wengi wao wanajielewa nakujisimamia.uku kwetu mtu anaambiwa changamoto inayomgusa mtoto anaona sawa tu.Ikitokea wamezurika tunakua wa kwanza kulaani.Lakini pia kama kweli hao wanafunzi wanafungiwa sio sahihi.Wahusika wafwatilie.Tujifunze kupenda nakuthamini vinavyotuhusu.
 
Back
Top Bottom