DOKEZO Walimu Wasio na Ajira (NETO) wanaongea na waandishi wa habari kuondoa dukuduku lao

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Walalamikue ajira kuwa kidogo lakini ishu ya interview ni muhimu saana.huyu waziri apongezwe.walimu ,wauguzi na madaktari ni majangaa.unakuta hawajuhi kitu.unakuta nesi hajuhi ata kudunga sindano.Wanatakiwa kufanya mitihani 3 tupunguze vilaza.
Iko sawa kwa 100%
 
Gentleman,
kwasabb hujafanikiwa kupata nafasi ya ajira za ualimu ndio waziri ajiuzulu, kweli?

Relax bana, ajira nyingi sana za uhakika na za kutosha ziko shambani, ni kufanya maamuzi sahihi na kuthubutu tu unatoboa kiulaini kabisa maisha.

Hata hivyo,
usikate tamaa, ajira hizo zonatoka kwa awamu, huenda awamu nyingine ukafanikiwa 🐒
 
Shida ya Mkenda ni nini hasa ulitaka waalimu waajiriwe bila interview? Na wafanyakazi wengine nao pia waajiriwe bila interview?
 
Yule mrombo ni very arrogant, ana egoism, anajiona anajua kila kitu, ameharibu elimu kuanzia mitaala. Ananyanyasa walimu anavyojisika ndio maana analalamikia protokali ya ikulu. Halafu kwanini watu wasiseme huu ni Rais wa kuambiwa.
Fanyeni interview yaani mpate masifuli harafu mtake kufelisha watoto
 
Walimu walikua hawatoshi miaka yote ila sasa wamezidi nafasi, kada zingine zilijaa miaka mingi sana nyuma
Siyo kweli kuna ofisi kibao hazina wahaisibu na makeshia wanatumia masekletari kufanya kazi hizo.
Kuna ofisi hazina ma IT ndiyo maana mafoleni kibao kazi haziendi.
Kuna maofisi hazina maprocurement manunuzi hovyo hovyo tuu.
Kuna zahanati hakuna Dr wanatibiwa na manesi.
Sema nyie mmezoea kupangiwa vituo hamjawahi ona intavyuu moyo kuruka ruka. Kuna watu toka 2012 mpaka sasa hawana kazi na wanafeli intavyuu lakini hawalalamiki.
 
Bahati mbaya sana mie sio mwalimu na nishafanya mainterview ya kutosha hadi ikafika naitwa tu na kupewa ofa, Nimetoa mawazo yangu unaweza kuchukua au kuyaacha tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…