Walinzi wa getini ofisi ya Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam punguzeni njaa, msijifiche kwenye kichaka cha barakoa

Wee ni mlinzi au
 
Sisi watanzania tushukuru Mungu sana vile Covid haijatupiga barabara...

La sivyo sasa hivi tungekuwa na nyuzi za kuhimizana tuvae barakoa hata kama wengine wanakaidi...

Hao walinzi naamini wanatekeleza maagizo tu, ukienda sehemu kama hizo kuepusha shari uwe unavaa, ukitoka hapo unavua unaendelea na maisha yako, ya nini kuanza kupoteza muda kubishana kwa kitu kidogo tu kama hicho
 
Hakika mkuu,,tena mtu anafanya upuuzi waziwazi na kuhalalisha haramu.
 
Hata pia ukienda ofisi ya tra mkoa wa Pwani nao ni hivyo hivyo bila barakoa huingii ndani na cha ajabu pia barakoa hizo wanauza wenyewe walinzi wa Suma JKT na ukiingia ndani hakuna mfanyakazi hata mmoja aliye vaa barakoa
Dah,,hili kumbe ni janga la taifa..
 
Kuvaa barakoa sio tatizo,
Lakini je?
Mbona wao hawavai?
Na kwanini wakwambiye nunuwa pale.

Na baada ya manunuzi hata usipovaa wao haiwahusu wala hawajali kama umevaa au umeweka mfukoni.
Na ukifika humo ndani Kati ya watu 100 amevaa mmoja tu kwa ufasaha.
Lakini wengine wote wameweka barakoa shingoni au mkononi.huku wao wenyewe watumishi wa umma hawana barakoa kabisa.
Huu ni uonevu kama sio njaa.

Sasa tujiulize kwamba hivi barakoa tunazolazimishwa kununuwa hapo getini ni biashara au ni kwa ajili ya afya na usalama wa wanainchi ktk janga hili la Corona?
 
Mambo mangine kujitakia shari na watu kisa buku tu.We nunua barakoa yako kafanye shughuli zako halafu pita hivi sasa uanze kupigishana makelele na watu kisa kitambaa cha puwa.Funika kombe mwanaharamu apite.Sisi marasta tunaamini hivo.
 
Daaaahhh. Jamaa wanaabudu sana barakoa. Ni biashara yao tangu zamani.
Korona haupo duniani bali kuna uhuni tu
Ni biashara zao mkuu,,hili halina ubishi.
Nimejiridhisha pasi na Shaka.
 
Nina barakoa yangu ya kitambaa nilinunua BUKU pale kibo complex roho iliniuma sana nilinunua tangu mwezi wa Saba mpaka leo ninayo IPO kwenye beg nikienda sehemu za mizinguo ndo naivaa.
Kutoa BUKU bila sababu inauma[emoji16][emoji16]
 
Sio ofisi zote za umma.
Mimi ni mtumishi wa umma, ofisini kwetu hakuna mtumishi wala mgeni anayevaa barakoa.
Barakoa katika ofisi za umma zinaletwa na walinzi njaa au wasiojitambua
 
Sio ofisi zote za umma.
Mimi ni mtumishi wa umma, ofisini kwetu hakuna mtumishi wala mgeni anayevaa barakoa.
Barakoa katika ofisi za umma zinaletwa na walinzi njaa au wasiojitambua
Ila hawa wa kwa mkuu wa mkoa daresalam njaa yao imezidi.

Wapo tayari kukuweka chini ya ulinzi kisa unahoji uhalali wa wao kulazimisha watu kununuwa barakoa getini na kuvaa,
Wakati wao wenyewe na watumishi wote humo ndani hawana..

Inashangaza kuona aliyeshika barakoa mkononi anaruhusiwa kupita bila usumbufu,
lakini wewe ambaye huna ndy unalazimishwa ununuwe kwa nguvu kupitia kwa mtu wao waliyemuweka pale getini,
 
Kama wanyama
 

Wao kutokuvaa ni tatizo na bora umewalipua na umewachana live...

Wao kulazimisha watu kununua barakoa za hapo getini hata kama mtu anayo ya kwake hilo nalo ni tatizo...

Mwisho wa siku kwenye ishu kama covid, ni kama ilivyo ngoma tu, ni suala la kujikinga binafsi
 
Barakoa kwa wanainchi wakawaida tu si ndy?
Mkuu kumbe wewe ni juha?
Nafahamu kwamba wewe ni mmoja wa walinzi,,umeamua kujitokeza hadharani na kutetea upupu.

Hivi Corona kumbe inachaguwa wa kumpata?
Mtumishi wa umma hastahili kuvaa barakoa?

Na haya Mambo ya kanunuwe pale yanatoka wapi kama sio biashara zenu?
Eti unasema wapunguze njaa kwa barakoa.
Watu wanaoingia humo kwa siku ni zaidi ya 300.
Sasa 300*1000 =ni sh ngpi kwa siku unapata?
 
Kweli kabisa mkuu.
Sasa waamue kusuka au kunyoa hilo ni jukumu lao.,

Ila wanapaswa watambuwe kuwa wasitufanye Sisi wanainchi wa kawaida hatujui umuhimu wa kuvaa barakoa..
Barakoa ni kwa wote na sio kwa wanaoingia pekee humo maofisini..

Na mambo ya kanunuwe pale yakomeshwe..

Wanapaswa wajikite kwenye uvaaji wa barakoa kwa ufasaha na sio kuishika mkononi au kuivaa shingoni.
Mbona hawalazimishi watu kunawa maji tiririka na senitezer ?
Kama ni kweli wapo kwa ajili ya kupambana na COVID na sio njaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…