Waliocheka, Walionuna na Waliolia baada superpower kubadili muelekeo.

Waliocheka, Walionuna na Waliolia baada superpower kubadili muelekeo.

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Uchaguzi wa Marekani ndio mkubwa zaidi duniani, kila kona ya dunia wanaufuatilia, uwe unaipenda au unaichukia Marekani.
Kwa matokeo haya ya Trump kushinda

1.Democrats wamelia kilio cha maombolezo, ushindi uliokuwa ukitegemewa umeyuyuka, wameshindwa kwa kishindo.

2.NATO na Umoja wa Ulaya wamenuna, Trump huwa hataki pesa za US kutoka sana kwenda nje ya US na Trump ni rafiki wa Putin adui mkubwa wa EU.

3.Ukraine wamelia kilio cha maombolezo, watalazimishwa kukubaliana na mashariti ya Russia kumaliza vita, msaada wa Marekani kupambana na Russia hautegemewi kuendelea.

3. Putin, Orban, Netanyahu na MBS wamecheka sana, wao na Trump ni washikaji sana. Saudi Arabia itaongeza biashara yake na US, Russia wanaweza kuondolewa vikwazo. Viktor Orban hayuko mnyonge tena ndani ya NATO, boss mkubwa wa NATO na yeye ni mapacha.

4. Hamas, Iran na Korea Kaskazini watabaki kuwa nyutro, Trump hatakuwa na msaada au afadhali yoyote kwao.

5.China-kawaida tu,
Wachina wao walishajua tangu zamani ku deal na yeyote wa US huku maslahi yao yakizingatiwa zaidi(Wachina unavyokuja ndivyo wanavyokupokea), pia wana misuli ya uchumi ya kutiliwa maanani na yeyote dunia hii.

6. Africa- Sisi tupo tupo tu, Iwe Kamala au Trump hakuna athari zozote kubwa za maana upande huu wa dunia kutoka kwa yeyote.

7.Wanaharakati wa demokrasia duniani kote- nusu wamecheka, nusu wamelia.

8.Wahamiaji na wazamiaji US-Kilio cha maombolezo.

9.India- Kawaida tu, hawa mambo yao na Marekani ni constant, huwa hayabadiliki awe yeyote pale White House, nafikiri Wahindi ndio Immigrants wanao enjoy sana US.
 
Haikwepeki, lazima Urusi na Ukraine watakaa meza moja ya makubaliano; ingawa walishapoteza watu, lakini maisha lazima yaendelee.
Inawezekana wanatamani wajiondoe kwenye vita, lakini watajiondoaje? Kwa mazingira hayo, kwa huu uongozi mpya utakuwa umewarahisishia kama utafanya hivyo.​
 
1.Democrats wamelia kilio cha maombolezo, ushindi uliokuwa ukitegemewa umeyuyuka, wameshindwa kwa kishindo.
Na wanalia sana, sisi kazi yetu ni kuwapatia lesso na tissue kwa ajili ya kufutia makamasi
2.NATO na Umoja wa Ulaya wamenuna, Trump huwa hataki pesa za US kutoka sana kwenda nje ya US na Trump ni rafiki wa Putin adui yao.
Hakatai hela ya US kutoka, ila anachohitaji ni uwiani sawa kwa mujibu wa makubaliano sababu wengine hawa play parts zao
3.Ukraine wamelia kilio cha maombolezo, watalazimishwa kukubaliana na mashariti ya Russia kumaliza vita
Trump hawezi kuwaacha Ukraine kama wengi wanavyofikiri, kufanya vitu bila kuzingatia msimamo, hadhi na maslahi ya nchi ni kati ya vitu Trump anavipinga. Pia ameona madhara yake kule Afghanistan, aliweka utaratibu mzuri wa kuondoa majeshi ya US, lakini Demons wakayaondoa kwa kukurupuka
3. Putin, Orban, Netanyahu na MBS wamecheka sana, wao na Trump ni washikaji sana. Saudi Arabia itaongeza biashara yake na US, Russia wanaweza kuondolewa vikwazo.
Putin hana cha kufurahia, unadhani itakuwa rahisi kuambiwa ayaachie na aondoke maeneo yote ambayo hakuwe kabla ya uvamizi?
4. Hamas, Iran na Korea Kaskazini watabaki kuwa nyutro, Trump hatakuwa na msaada au afadhali yoyote kwao.
Hamas na Iran ni kilio, Korea ataachwa kama alivyo
5.China-kawaida tu,
Wachina wao walishajua tangu zamani ku deal na yeyote wa US huku maslahi yao yakizingatiwa zaidi(unavyokuja ndivyo wanavyokupokea), pia wana misuli ya uchumi ya kutiliwa maanani na yeyote.
China kichwa kinamuwaka, anakutana na yule wa weka ugoko nipige na nondo au jiwe. China alizoea kwa miaka mingi kudhibiti US products, like google, youtube n.k, for once akakutana na mtu aliyeamua kwenda naye jino kwa jino
6. Africa- Sisi tupo tupo tu, Iwe Kamala au Trump hakuna athari zozote kubwa za maana upande huu wa dunia kutoka kwa yeyote.
Afrika wana hata hiyo habari basi!? Ndiyo kwanza wana CCM wengi walimuunga mkono Kamala wakiona kumuunga mkono Mwanamke ni kumuunga Mkono Samia
7.Wanaharakati wa demokrasia duniani kote- nusu wamecheka, nusu wamelia.
democrasia ni mtambuka
8.Wahamiaji na wazamiaji US-Kilio cha maombolezo.
Hajawahi kuwa na shida na wahamiaji halali
 
Na wanslia sana, sisi kazi yetu ni kuwapatia lesso na tissue kwa ajili ya kufutia makamasi

Hakatai hela ya US kutoka, ila anachohitaji ni uwiana sawa kwa mujibu wa makubaliano sababu wengine hawa play parts zao

Trump hawezi kuwaacha Ukraine kama wengi wanavyofikiri, kufanya vitu bila kuzingatia msimamo, hadhi na maslahi ya nchi ni kati ya vitu Trump anavipinga. Pia ameona madhara yake kule Afghanistan, aliweka utaratibu mzuri wa kuondoa majeshi ya US, lakini Demons wakayaondoa kwa kukurupuka

Putin hana cha kufurahia, unadhani itakuwa rahisi kuambiwa ayaachie na aondoke maeneo yote ambayo hakuwe kabla ya uvamizi?

Hamas na Iran ni kilio, Korea ataachwa kama alivyo

China kichwa kinamuwaka, anakutana na yule wa weka ugoko nipige na nondo au jiwe. China alizoea kwa miaka mingi kudhibiti US products, like google, youtube n.k, for once akakutana na mtu aliyeamua kwenda naye jino kwa jino

Afrika wana hata hiyo habari basi!? Ndiyo kwanza wana CCM wengi walimuunga mkono Kamala wakiona kumuunga mkono Mwanamke ni kumuunga Mkono Damia

democrasia ni mtambuka

Hajawahi kuwa na shida na wahamiaji halali
Nashangaa sana ni kwanini CCM hasa machawa wameumizwa sana na ushindi wa Trump, yaani ukipita kwenye page zao huko ni captions za pole tu kwa Haris
 
Back
Top Bottom