Waliojenga mwaka 2021 tunaomba uzoefu wenu

Waliojenga mwaka 2021 tunaomba uzoefu wenu

Shukrani mkuu kwa ushauri wako, mimi pia nina project yangu japo imesimama kidogo, kwa ushauri huu nimepata nguvu na hamasa ya kujivuta taratibu.

Narudia tena, usikate tamaa wala kuona unachelewa.

Hizo picha zisikutishe, mambo hayakwenda haraka kama zinavyoonekana.

Baada ya kufunga mkanda wa chini, nilikaa mda mrefu tu inakaribia miezi nane.

Nilipoinua boma kufunga linter na ile mistari mitatu ya juu napo nikapitea hapo ni miaka 2. Nikaja kurudi kwa kasi hadi kuhamia sasa.

Usivunjike moyo kabisa.
 
Narudia tena, usikate tamaa wala kuona unachelewa.

Hizo picha zisikutishe, mambo hayakwenda haraka kama zinavyoonekana.

Baada ya kufunga mkanda wa chini, nilikaa mda mrefu tu inakaribia miezi nane.

Nilipoinua boma kufunga linter na ile mistari mitatu ya juu napo nikapitea hapo ni miaka 2. Nikaja kurudi kwa kasi hadi kuhamia sasa.

Usivunjike moyo kabisa.
Am sure mpaka kufika July nitakuwa nafanya finishing. Tuombe uzima
 
IMG_4853.jpg

Teknolojia mpya hii ya ujenzi wandugu..wenye experience tafadhali..naona hawatumii tofali
 
Hongera mkuu kwa hatua hii. Daaah najiwazie mie wa buku 7 daily ntaweza kujenga kweli kama msingi tu unakula tofari buku 2!
 
Hongera mkuu kwa hatua hii. Daaah najiwazie mie wa buku 7 daily ntaweza kujenga kweli kama msingi tu unakula tofari buku 2!

Tofali zinaweza kuongezeka au kupungua kulingana na eneo. Ikiwa kiwanja chako kipo kwenye tambarare, msingi hauli tofali nyingi.

Usikate tamaa wala usife moyo mkuu.
 
Kujenga ni technique..nilipigwa nyumba ya kwanza lakini sasa nimejifunza, kifupi jiweke kidalali sio kiboss..
1. Msingi nawauzia vibarua, tunakubaliana, alafu fundi anasimamia
2. Tofali namuuzia fundi sh 300 japo za juu wengine wanadai nyongeza kidogo
3. Kokoto, nanunua kifusi cha kokoto alafu nachambua..hapo napata kifusi na kokoto
4. Tofali nanunua 950
5. Nondo naenda scrap yard napima zilizopo alafu zile pande ndefu nanunua..
6. Grill nachukua nondo hapo hapo scrap yard nanunua bomba za pembeni tu
7. Mbao za kuezekea nachukua buguruni, ukitaka kuwaweza madalali..nenda na mwanao tu alafu mfanye yy ndio boss, waite pemben waambie nimemleta boss, watakupa bei halisi
8.Bati mara nyingi hazina shortcut
9. Tiles kama unahitaji box chache..mafundi wanazo tena konk sana
10. Wire, mafundi wanazo nzuri tu sema earth rod kanunue copper inakuwa na bei kidogo kwenye 45k kwenda juu..chini ya hapo kafukue chuma hicho
11.Nenda mwenyewe dukani
NB: Nyumba inahitaji usimamizi wako, sio ndugu au rafiki, utalaumu watu bure
Kuwa mkali sana kwenye mali zako, simamia kila eneo..

Watakushukuru baadae...
 
Back
Top Bottom