Waliomsindikiza Mwalimu Nyerere safari ya kwanza UNO 1955

Waliomsindikiza Mwalimu Nyerere safari ya kwanza UNO 1955

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
1571429456771.png

Sahihisho picha ya akina mama walimsindikiza Mwalimu.
Kulia ni Bi. Tatu bint Mzee na kushoto ni Bi. Chiku bint Said Kisusa
Daisy Sykes akiwa msichana wa miaka 8 anamkumbuka marehemu baba yake wakati wa kujenga TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hapo chini anaeleza jinsi alivyoshuhudia nyumbani kwao jinsi baba yake alivyowaingiza akina mama katika harakati za TANU:


''Ilikuwa katika kipindi hiki cha mimi kuanza kupata akili katika kukua kwangu ndipo nilipokutana na wanawake wazalendo waliokuwa wanaochipukia katika uongozi wa Tanganyika, wanawake kama Bi. Lucy Lameck kutoka Moshi, Mary Ibrahim na akina mama wa Kiislam kama Bi. Titi Mohamed, Bi. Tatu bint Mzee, Bi. Hawa bint Maftah, hawa kutoka Dar es Salaam, wote hawa kwangu mimi walikuwa bibi zangu.

Kitu cha kufurahisha ni kuwa hawa akina mama wote walivutwa katika siasa na Bibi Chiku bint Said Kisusa, maarufu akijulikana kama Mama Sakina.

Soma pia: Bi. Chiku Kisusa (Mama Sakina)

Alikuwa Mama Sakina ndiye aliyewapa hawa wanawake niliowataja hapo juu utambulisho na wakaja kuwa watu maarufu.

DAISY POTRAIT.jpg


Baba yeye ndiye alikuwa kiongozi wa mikakati hii yote kwa sababu bila yeye kuwatia hima kwa kutumia ushawishi wake ingekuwa vigumu kuweza kuwatia hawa wanawake katika kuwahamasisha wanawake wenzao wa Kiislam na wao watoke majumbani kuja mstari wa mbele katika mikutano wakiimba na kutoa vibwagizo vya kuunga mkono TANU na kudai uhuru.

Hili jambo lilikuwa jipya, jambo ambalo katika utamaduni wetu kwa wakati ule halikutarajiwa na ni kinyume katika utamaduni wetu kwa wanawake wa Kiislam kulifanya katika siku zile.

Nimesikia mazungumzo mengi wakati baba na wenzake walipokuwa wakijadili majina na shughuli ambazo hawa akina mama walikuwa wahusishwe ili kuleta mvuto wa kisiasa katika mikutano yao ya TANU.

Nakumbuka vizuri sana jinsi baba alivyokuwa karibu sana na Mwalimu Sakina na ndugu yake Mwalimu Fatna (wote hawa watoto wa Mama Sakina), na jinsi alivyowaleta ndugu hawa karibu na Mama Maria na hawa wakamjulisha Mama Maria Nyerere kwa mama yao na mashoga zake Bi Hawa Maftaha, Bibi Titi Mohamed na Bi Tatu binti Mzee.

Hawa wanawake ndiyo waliomsaidia Mama Maria kufungua duka lake dogo pale Mtaa wa Livingstone kona na Mchikichi, mahali ambako Mama Maria alishinda kutwa nzima akiuuza duka lake.

Nikiwa mtoto nakumbuka kwenda kwenye duka lile kila siku mchana kupeleka chakula kwa Mama Maria, ambako hapakuwa mbali kutoka nyumbani kwetu.

Kwa kuwa baba alikuwa anataka ratiba hii yake ya chakula ifuatwe sawasawa kwa wakati wake, wakati mwingine hii ilikuwa changamoto kubwa sana.''


 
Jana nilikuwa nangalia documentary moja inazungumzia jinsi kijana Mmarekani mweusi, Berry Gordy, alivyoanzisha kampuni ya muziki ya Motown na kupata mafanikio makubwa sana kuwatambulisha wanamuziki wengi sana waliochipukia miaka ya sitini, sabini, mpaka themanini mwanzoni kutoka kampuni ya Motown. Kuanzia kina Smokie Robinson, Stevie Wonder, Marvin Gaye,Michael Jackson, The Temptations, The Supremes na wengine wengi sana.

Sasa, kuna sehemu katika ile documentary, marafiki wawili wa muda mrefu, Berry Gordy na Smokie Robinson, ambao wote walikuwapo wakati Motown inaanza, wakawa wanabishana kuhusu nani alikuwa wa kwanza kuimba wimbo fulani kati ya Marvin Gaye na mwanamuziki mwingine. Wakawa hawakubaliani. Ikabidi Wamarekani kama kawaida yao, wafanye "bet" ya USD 100. Haya mambo mengine naona hata Google inawezekana haijui, au wao hawakutaka ku Google, wakampigia simu rafiki yao mwingine. Wakamuuliza swali, aliyeanza kuimba wimbo huu ni nani? Ikatokea Berry Gordy akawa kapatia, Smokie Robinson akafungua wallet pale pale akatoa dola 100 kama mchezo.

Nikajifunza kitu kimoja hapo, ingekuwa ameulizwa Smokie Robinson peke yake, angeweza kutoa jibu lisilo sawa, akakubalika, kwa sababu yeye ni "authority" na alikuwapo wakati Motown inaanzishwa.

Ila, nikaona kwamba, hata "authority" naye, mara nyingine anaghafilika, kwa sababu miaka mingi ikipita kukumbuka mambo si rahisi.

Hii ni sababu muhimu ya kufanya uchunguzi, kuandika mambo, kurejea maandiko, kupambanisha authority na authority (wasomi wanaita "peer review").

Smokie Robinson aliweza kukosolewa kwa sababu kulikuwa na peer review ilifanyika kwa Berry Gordy na mtu mwingine waliyempigia simu.

JF pia tunahitaji peer review ya kisomi.

 
Jana nilikuwa nangalia documentary moja inazungumzia jinsi kijana Mmarekani mweusi, Berry Gordy, alivyoanzisha kampuni ya muziki ya Motown na kupata mafanikio makubwa sana kuwatambulisha wanamuziki wengi sana waliochipukia miaka ya sitini, sabini, mpaka themanini mwanzoni kutoka kampuni ya Motown. Kuanzia kina Smokie Robinson, Stevie Wonder, Marvin Gaye,Michael Jackson, The Temptations, The Supremes na wengine wengi sana.

Sasa, kuna sehemu katika ile documentary, marafiki wawili wa muda mrefu, Berry Gordy na Smokie Robinson, ambao wote walikuwapo wakati Motown inaanza, wakawa wanabishana kuhusu nani alikuwa wa kwanza kuimba wimbo fulani kati ya Marvin Gaye na mwanamuziki mwingine. Wakawa hawakubaliani. Ikabidi Wamarekani kama kawaida yao, wafanye "bet" ya USD 100. Haya mambo mengine naona hata Google inawezekana haijui, au wao hawakutaka ku Google, wakampigia simu rafiki yao mwingine. Wakamuuliza swali, aliyeanza kuimba wimbo huu ni nani? Ikatokea Berry Gordy akawa kapatia, Smokie Robinson akafungua wallet pale pale akatoa dola 100 kama mchezo.

Nikajifunza kitu kimoja hapo, ingekuwa ameulizwa Smokie Robinson peke yake, angeweza kutoa jibu lisilo sawa, akakubalika, kwa sababu yeye ni "authority" na alikuwapo wakati Motown inaanzishwa.

Ila, nikaona kwamba, hata "authority" naye, mara nyingine anaghafilika, kwa sababu miaka mingi ikipita kukumbuka mambo si rahisi.

Hii ni sababu muhimu ya kufanya uchunguzi, kuandika mambo, kurejea maandiko, kupambanisha authority na authority (wasomi wanaita "peer review").

Smokie Robinson aliweza kukosolewa kwa sababu kulikuwa na peer review ilifanyika kwa Berry Gordy na mtu mwingine waliyempigia simu.

JF pia tunahitaji peer review ya kisomi.


Kiranga,
Umesema kweli kabisa makosa mengi hufanyika na ni vizuri kusikia na mwengine analijua vipi.

Miaka mingi ikipita kumbukumbu hupotea kirahisi sana.

Umenikumbusha mbali sana kaka.

Collection yangu ya ngoma hizo ilikuwa kali sana.

Siku nilipofika Apollo Theatre New York nikakumbuka wakati nina miaka 16 hivi nakua Dar es Salaam mimi na wenzangu tukiziimba nyimbo za Tamla Motown.

Nilisimama kwa muda Broadway nikakumbuka mwimbo wa Wilson Pickett ''Funky Broadway,'' na ikasadifu kuwa barabara nikiipita Manhattan katika shughuli zangu.

Wengi wa hawa ''stars'' walianza ''carrier'' zao hapo Apollo Theatre na tukikuona mbali sana...

Kaka Kiranga Temptations wakaja Paris kufungua Disneyland mimi niko upande wa pili wa English Channel katika kimji kidogo Wales wako mubashara...wazimu kaka sasa tumekuwa watu wazima miaka imekwenda wapi?

Nadhani Temptations aliye hai ni mmoja tu.

MOHAMED APOLLO THEATRE.JPG
 
Kiranga,
Umesema kweli kabisa makosa mengi hufanyika na ni vizuri kusikia na mwengine analijua vipi.

Miaka mingi ikipita kumbukumbu hupotea kirahisi sana.

Umenikumbusha mbali sana kaka.
Collection yangu ya ngoma hizo ilikuwa kali sana.

Siku nilipofika Apollo Theatre New York nikakumbuka wakati nina miaka 16 hivi nakua Dar es Salaam mimi na wenzangu tukiziimba nyimbo za Tamla Motown.

Nilisimama kwa muda Broadway nikakumbuka mwimbo wa Wilson Pickett ''Funky Broadway,'' na ikasadifu kuwa barabara nikiipita Manhattan katika shughuli zangu.

Wengi wa hawa ''stars'' walianza ''carrier'' zao hapo Apollo Theatre na tukikuona mbali sana...

Kaka Kiranga Temptations wakaja Paris kufungua Disneyland mimi niko upande wa pili wa English Channel katika kimji kidogo Wales wako mubashara...wazimu kaka sasa tumekuwa watu wazima miaka imekwenda wapi?

Nadhani Temptations aliye hai ni mmoja tu.


Hili halisemwi kwamba Kuna mtu hakutaka historia ya mchakato wa ukombozi wa nchi yetu iwe bayana kwa nia ya "monopolising his prestige"

Mwalimu was classmate of my father in Tabora, of course, Mwalimu has indeed done good things for this country but one of his attitude at the school as my father narrated makes me nervous, it was the underlying attitude which made some of the independence struggle history be hidden.
 
Daisy Sykes akiwa msichana wa miaka 8 anamkumbuka marehemu baba yake wakati wa kujenga TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hapo chini anaeleza jinsi alivyoshuhudia nyumbani kwao jinsi baba yake alivyowaingiza akina mama katika harakati za TANU:


''Ilikuwa katika kipindi hiki cha mimi kuanza kupata akili katika kukua kwangu ndipo nilipokutana na wanawake wazalendo waliokuwa wanaochipukia katika uongozi wa Tanganyika, wanawake kama Bi. Lucy Lameck kutoka Moshi, Mary Ibrahim na akina mama wa Kiislam kama Bi. Titi Mohamed, Bi. Tatu bint Mzee, Bi. Hawa bint Maftah, hawa kutoka Dar es Salaam, wote hawa kwangu mimi walikuwa bibi zangu.

Kitu cha kufurahisha ni kuwa hawa akina mama wote walivutwa katika siasa na Bibi Chiku bint Said Kisusa, maarufu akijulikana kama Mama Sakina.

Alikuwa Mama Sakina ndiye aliyewapa hawa wanawake niliowataja hapo juu utambulisho na wakaja kuwa watu maarufu.

Baba yeye ndiye alikuwa kiongozi wa mikakati hii yote kwa sababu bila yeye kuwatia hima kwa kutumia ushawishi wake ingekuwa vigumu kuweza kuwatia hawa wanawake katika kuwahamasisha wanawake wenzao wa Kiislam na wao watoke majumbani kuja mstari wa mbele katika mikutano wakiimba na kutoa vibwagizo vya kuunga mkono TANU na kudai uhuru.

Hili jambo lilikuwa jipya, jambo ambalo katika utamaduni wetu kwa wakati ule halikutarajiwa na ni kinyume katika utamaduni wetu kwa wanawake wa Kiislam kulifanya katika siku zile.

Nimesikia mazungumzo mengi wakati baba na wenzake walipokuwa wakijadili majina na shughuli ambazo hawa akina mama walikuwa wahusishwe ili kuleta mvuto wa kisiasa katika mikutano yao ya TANU.

Nakumbuka vizuri sana jinsi baba alikvyokuwa karibu sana na Mwalimu Sakina na ndugu yake Mwalimu Fatna (wote hawa watoto wa Mama Sakina), na jinsi alivyowaleta ndugu hawa karibu na Mama Maria na hawa wakamjulisha Mama Maria Nyerere kwa mama yao na mashoga zake Bi Hawa Maftaha, Bibi Titi Mohamed na Bi Tatu binti Mzee.

Hawa wanawake ndiyo waliomsaidia Mama Maria kufungua duka lake dogo pale Mtaa wa Livingstone kona na Mchikichi, mahali ambako Mama Maria alishinda kutwa nzima akiuuza duka lake.

Nikiwa mtoto nakumbuka kwenda kwenye dula lile kila siku mchana kupeleka chakula kwa Mama Maria, ambako hapakuwa mbali kutoka nyumbani kwetu.

Kwa kuwa baba alikuwa anataka ratiba hii yake ya chakula ifuatwe sawasawa kwa wakati wake, wakati mwingine hii ilikuwa changamoto kubwa sana.''


Hiyo picha ya kwanza juu ,umewataja majina hao wakina mama wengi waliovalia mabaibui lakini umemuacha huyo aliyevaa sketi humjui? Huyo mama ni Lucy Lameck!!!!
 
Hiyo picha ya kwanza juu ,umewataja majina hao wakina mama wengi waliovalia mabaibui lakini umemuacha huyo aliyevaa sketi humjui? Huyo mama ni Lucy Lameck!!!!
Ndinani,
Huyo si Lucy Lameck.

Nimejitahidi kutafuta majina ya hao wanawake wawili bado sijafanikiwa.
 
Nadhani hizi sentensi ndio zimebeba theme(s) za huu uzi.
Dutu,
Wala hujakosea.

Ilikuwa si rahisi kuwatoa uani wanawake wa Kiislam miaka ile ukawaleta Mnazi Mmoja hadharani kwenye mikutano ya TANU.
 
Nadhani hizi sentensi ndio zimebeba theme(s) za huu uzi.
Huyu mzee amejaa hila, na maandishi yake mimi nayaona kama ya hovyo tu kwakuwa yamejiegemeza ktk kubagua watu kidini kwa kujifunika na blanketi la kujifanya anaijua sana historia ya nchii!!
Hayo maneno hapo ni uthibitisho tosha!

Nimeona vitabu vyake vinauzwa misikitini kariakoo, nikacheka kimoyomoyo!
 
View attachment 1237639
Sahihisho picha ya akina mama walimsindikiza Mwalimu.
Kulia ni Bi. Tatu bint Mzee na kushoto ni Bi. Chiku bint Said Kisusa
Daisy Sykes akiwa msichana wa miaka 8 anamkumbuka marehemu baba yake wakati wa kujenga TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hapo chini anaeleza jinsi alivyoshuhudia nyumbani kwao jinsi baba yake alivyowaingiza akina mama katika harakati za TANU:


''Ilikuwa katika kipindi hiki cha mimi kuanza kupata akili katika kukua kwangu ndipo nilipokutana na wanawake wazalendo waliokuwa wanaochipukia katika uongozi wa Tanganyika, wanawake kama Bi. Lucy Lameck kutoka Moshi, Mary Ibrahim na akina mama wa Kiislam kama Bi. Titi Mohamed, Bi. Tatu bint Mzee, Bi. Hawa bint Maftah, hawa kutoka Dar es Salaam, wote hawa kwangu mimi walikuwa bibi zangu.

Kitu cha kufurahisha ni kuwa hawa akina mama wote walivutwa katika siasa na Bibi Chiku bint Said Kisusa, maarufu akijulikana kama Mama Sakina.

Alikuwa Mama Sakina ndiye aliyewapa hawa wanawake niliowataja hapo juu utambulisho na wakaja kuwa watu maarufu.

Baba yeye ndiye alikuwa kiongozi wa mikakati hii yote kwa sababu bila yeye kuwatia hima kwa kutumia ushawishi wake ingekuwa vigumu kuweza kuwatia hawa wanawake katika kuwahamasisha wanawake wenzao wa Kiislam na wao watoke majumbani kuja mstari wa mbele katika mikutano wakiimba na kutoa vibwagizo vya kuunga mkono TANU na kudai uhuru.

Hili jambo lilikuwa jipya, jambo ambalo katika utamaduni wetu kwa wakati ule halikutarajiwa na ni kinyume katika utamaduni wetu kwa wanawake wa Kiislam kulifanya katika siku zile.

Nimesikia mazungumzo mengi wakati baba na wenzake walipokuwa wakijadili majina na shughuli ambazo hawa akina mama walikuwa wahusishwe ili kuleta mvuto wa kisiasa katika mikutano yao ya TANU.

Nakumbuka vizuri sana jinsi baba alikvyokuwa karibu sana na Mwalimu Sakina na ndugu yake Mwalimu Fatna (wote hawa watoto wa Mama Sakina), na jinsi alivyowaleta ndugu hawa karibu na Mama Maria na hawa wakamjulisha Mama Maria Nyerere kwa mama yao na mashoga zake Bi Hawa Maftaha, Bibi Titi Mohamed na Bi Tatu binti Mzee.

Hawa wanawake ndiyo waliomsaidia Mama Maria kufungua duka lake dogo pale Mtaa wa Livingstone kona na Mchikichi, mahali ambako Mama Maria alishinda kutwa nzima akiuuza duka lake.

Nikiwa mtoto nakumbuka kwenda kwenye dula lile kila siku mchana kupeleka chakula kwa Mama Maria, ambako hapakuwa mbali kutoka nyumbani kwetu.

Kwa kuwa baba alikuwa anataka ratiba hii yake ya chakula ifuatwe sawasawa kwa wakati wake, wakati mwingine hii ilikuwa changamoto kubwa sana.''


Kweli familia ya Sykes unaitukuza. Hivi unajua kuwa Nyerere Aliipoanza kazi Tabora nani alimpokea akaa kwake hadi akamuoa Mama Maria nyumbani kwake? Hizi simulizi zako zimeegemea upande mmoja. Tungependa simulizi neutral
 
Nyerere ndiye alianzisha kudai uhuru. Nyerere ndiye alianzisha ofisi za kudai uhuru Tanganyika. Nyerere ndiye alianzisha TANU. Nyerere ndiye alibuni jina la TANU.

Hao wote hapo kwenye picha walikuwa wanajipendekeza tu kwa Nyerere.

Historia ya kudai uhuru wa Tanganyika inaanzia na kuishia kwa Nyerere.

Nyerere kaja Dar kakuta watu hawajui kusoma wala kuandika. Kakuta watu wajinga wajinga tu hata uhuru hawaujui ni nini.

Sio hayo yanayompa utakatifu? Au kuna mengine yanayompa utakatifu ambayo hatuyajui?
 
Kweli familia ya Sykes unaitukuza. Hivi unajua kuwa Nyerere Aliipoanza kazi Tabora nani alimpokea akaa kwake hadi akamuoa Mama Maria nyumbani kwake? Hizi simulizi zako zimeegemea upande mmoja. Tungependa simulizi neutral
Si hadithia na wewe simulizi zako, mbona na mimi nimeweka simulizi yangu hapo juu.

Hauelewi kuwa hili ni jukwaa huru?
 
Abdi...
Historia hii nimeiandika ni kitabu hivi sasa kipo huu mwaka wa 21 na kiandikwacho hakipotei mradi wako wasomaji.
Wanao soma vitabu n wachache Sana siku hz na zile Baraza za masimuliz hazipo siku hz story nying za viongoz wetu waliopita hazipo Tena kitaaa kuwa na vitabu s tatizo,tatizo Ni wasimuliz wanaongeza chumv na kukupa ushawishi wa kutafuta kitabu husika
 
Wanao soma vitabu n wachache Sana siku hz na zile Baraza za masimuliz hazipo siku hz story nying za viongoz wetu waliopita hazipo Tena kitaaa kuwa na vitabu s tatizo,tatizo Ni wasimuliz wanaongeza chumv na kukupa ushawishi wa kutafuta kitabu husika
Siku hizi kuna hizi media za kielektroniki tunasoma sana tu. Si hata wewe umekisoma kisa hiki cha waliomsindikiza Nyerere hapo hapo kiganjani mwako?
 
Back
Top Bottom