Waliomsindikiza Mwalimu Nyerere safari ya kwanza UNO 1955

Waliomsindikiza Mwalimu Nyerere safari ya kwanza UNO 1955

Allama Mohamed Said usimshangae huyo Ndinani. Hapo kishaishiwa anatapatapa.
Maalim Faiza,
Kuna jambo mimi linanistaajabisha sana kwa hawa ndugu zangu.
Hivi hawaiamini hii historia niliyoandika au kitu gani?

Hivi kweli wao wanaona sawa kuwa hii historia yote hii iliyofutwa hivi wangependa kama isingekuwapo?

Kwa nini wana chuki na historia hii?

Hili mosi,
Pili kinachowaghadhabisha ni kitu gani?

Ni kwa kuwa historia hii ni historia ambayo inaeleza kuwepo kwa Waislam Tanganyika na kuwa walipigania uhuru wa Tanganyika au ni nini khasa kinawakereketa nafsi zao na ndiyo maana wakailia njama kuifuta?

Tatu tofauti na wasomi Ulaya na Marekani hawa historia hii imegutua fikra zao na kushangazwa kuwa iweje historia kama hii iwe watafiti wote na wasomi katika Idara ya Historia ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam iwapite wasiifahamu kwa miaka yote?

Sasa wao kwangu mimi wamekuwa ni kuniuliza maswali na kutaka kujua zaidi na kuomba ushahidi kwa baadhi ya mambo ambayo wao hawakuyaelewa.

Hawa sasa hivi wamekuwa msaada mkubwa sana hawa ndiyo walioniletea taarifa za ziri za Special Branch kutoka Uingereza kuhusu Abdul Sykes na harakati zake za siasa wakati wa anahanga kuunda TANU.

Baadhi ya nyaraza hizi nimeziweka hapa barzani na kila wakipata taarifa mpya basi watanitumia.

Ni hawa rafiki zangu walionitia hima nitafute picha ya Denis Phombeah (TANU Card No. 5) hadi nikaitia mkononi.

Nimeweka picha mbili za Denis Phombeah hapa Majlis na nimeandika historia yake naamini wengi mmemsoma.

Historia hizi zinawachoma nini?

Hakuna hata mmoja katika wasomi hawa wa Ulaya na Marekani kanikabili kwa vitisho, kejeli au matusi.

Zaidi wamenipa mialiko kuzungumza kwenye vyuo vyao.
Ni hapa nyumbani tu ndipo historia hii inapandisha ghadhabu kupelekea matusi na kejeli.

Ajabu ya Rahman.
 
Maalim Faiza,
Kuna jambo mimi linanistaajabisha sana kwa hawa ndugu zangu.
Hivi hawaiamini hii historia niliyoandika au kitu gani?

Hivi kweli wao wanaona sawa kuwa hii historia yote hii iliyofutwa hivi wangependa kama isingekuwapo?

Kwa nini wana chuki na historia hii?

Hili mosi,
Pili kinachowaghadhabisha ni kitu gani?

Ni kwa kuwa historia hii ni historia ambayo inaeleza kuwepo kwa Waislam Tanganyika na kuwa walipigania uhuru wa Tanganyika au ni nini khasa kinawakereketa nafsi zao na ndiyo maana wakailia njama kuifuta?

Tatu tofauti na wasomi Ulaya na Marekani hawa historia hii imegutua fikra zao na kushangazwa kuwa iweje historia kama hii iwe watafiti wote na wasomi katika Idara ya Historia ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam iwapite wasiifahamu kwa miaka yote?

Sasa wao kwangu mimi wamekuwa ni kuniuliza maswali na kutaka kujua zaidi na kuomba ushahidi kwa baadhi ya mambo ambayo wao hawakuyaelewa.

Hawa sasa hivi wamekuwa msaada mkubwa sana hawa ndiyo walioniletea taarifa za ziri za Special Branch kutoka Uingereza kuhusu Abdul Sykes na harakati zake za siasa wakati wa anahanga kuunda TANU.

Baadhi ya nyaraza hizi nimeziweka hapa barzani na kila wakipata taarifa mpya basi watanitumia.

Ni hawa rafiki zangu walionitia hima nitafute picha ya Denis Phombeah (TANU Card No. 5) hadi nikaitia mkononi.

Nimeweka picha mbili za Denis Phombeah hapa Majlis na nimeandika historia yake naamini wengi mmemsoma.

Historia hizi zinawachoma nini?

Hakuna hata mmoja katika wasomi hawa wa Ulaya na Marekani kanikabili kwa vitisho, kejeli au matusi.

Zaidi wamenipa mialiko kuzungumza kwenye vyuo vyao.
Ni hapa nyumbani tu ndipo historia hii inapandisha ghadhabu kupelekea matusi na kejeli.

Ajabu ya Rahman.
Allama Mohamed Said kwa upande wangu naona jibu ni jepesi sana, inawachoma kwa kuwa wengi wao walikuwa upande wa pili wa shillingi na hawana cha maana cha kuhadithia.

Umeongelea Marekani, kuna mada niliileta ya huko huko Marekani, nayo naona imekuwa mwiba kwao. Lakini kwa wenzetu huko, wengi sana wanaipokea kama historia kwa roho nyeupe kabisa kwa kuwa ni ukweli. Hii hapa...


Maalim wewe shusha vitu tu, tupo wengi tunaoithamini hii historia. Hawa wachache wasiofahamu maana ya historia wasikushughulishe sana, wape nondo tu kama kawaida yako.

Ma shaa Allah.
 
Wakina mama wa kimanyema nao walijitahidi kujenga vibanda vingi hapo CARRY AND GO kutokana na biashara ya vitumbua;; nyie wajukuu zao mmeviuza kwa Wapemba ili mkatangaze ufalme bar!!!
Ndinani,
Umenikumbusha bibi yangu mkubwa.
Tukizoea kumwita Biti Farijallah Mkubwa.

Bibi yangu huyu nyumba yake iilikuwa hapa Mtaa wa Mafia na Msimbazi inapopita barabara ya Msimbazi.

Nyumba yake ilivunjwa kupisha upanuzi wa Barabara ya Msimbazi.
Fidia aliyolipwa na serikali akanunua nyumba mbili Temeke.

Bibi yangu huyu nathubutu kusema kuwa ndiye mwanamama wa Kiswahili ambae kwa Kariakoo ile ya 1960s alikuwa na gari yake mwenyewe na dereva wa kumuendesha yeye na mumewe, babu yangu Mzee Kassim,

Ulipotaja mwanamke wa Kimanyema umenikumbusha bibi yangu huyu huge, tall and very elegant mikono yake yote miwili kaeneza dhahabu kama vile namuona kwenye Peugeot yake kakaa nyuma.

Kila alipokuwa akiona sura yangu alikuwa ananipa shilingi moja hadi alipofariki.

Nakuwekea picha ya Bibi yangu Mkuu Bi. Safia bint Numbi, maarufu kwa jina Bibi Popo huyu ni mama ya bibi zangu yeye katokea Belgian Congo mwishoni mwa miaka ya 1880s.

Picha hii nimempiga mimi Tabora 1965 nikiwa na umri wa miaka 13 kwa kamera aliyonipa baba yangu aina ya Kodak.

Hapo alikuwa mtu mzima sana mwangalie kasimama 6 ft ingawa kapinda kidogo kwa uzee.
Baba yangu ndiye aliyenitia mimi katika kupenda photography.

Miaka ile ilikuwa ''expensive hobby,'' maana ilibidi anipe fedha za kusafisha picha wakiita, ''developing,'' na hakuchoka kunipa fedha hizo,
 

Attachments

  • SAFIA BINT FARJALA.jpg
    SAFIA BINT FARJALA.jpg
    15.7 KB · Views: 1
Ndinani,


Nakuwekea picha ya Bibi yangu Mkuu Bi. Safia bint Numbi, maarufu kwa jina Bibi Popo huyu ni mama ya bibi zangu yeye katokea Belgian Congo mwishoni mwa miaka ya 1880s.

Picha hii nimempiga mimi Tabora 1965 nikiwa na umri wa miaka 13 kwa kamera aliyonipa baba yangu aina ya Kodak.

Hapo alikuwa mtu mzima sana mwangalie kasimama 6 ft ingawa kapinda kidogo kwa uzee.
Tabora maeneo yepi Maalim! kama namfahamu huyu bibi.
 
Ulipotaja mwanamke wa Kimanyema umenikumbusha bibi yangu huyu huge, tall and very elegant mikono yake yote miwili kaeneza dhahabu kama vile namuona kwenye Peugeot yake kakaa nyuma.

Wakina mama wa Kimanyema walikuwa wajasiliamali sana ukiwafananisha na waume zao. Nawakumbuka wakina mama wawili wa Kimanyema; Binti Matola wa kule Mbeya ambaye ndiye alikuwa kinara wa TANU enzi hizo nae alikuwa mjasiliamali mzuri aliyejenga nyumba yake sambamba na hilo soko hapo Mbeya mjini lililopewa jina lake, mwingine alikuwa akiitwa Binti Mausi huyu alikuwa Dodoma pamoja na wakina Mzee Alli Ponda naye alikuwa mjasiliamali akijishuhulisha zaidi na upikaji wa Pombe za kienyeji!! Nao pia walikuwa na tabia hiyo ya kuwapa watoto wadogo pesa!!!!
 
Wakina mama wa Kimanyema walikuwa wajasiliamali sana ukiwafananisha na waume zao. Nawakumbuka wakina mama wawili wa Kimanyema; Binti Matola wa kule Mbeya ambaye ndiye alikuwa kinara wa TANU enzi hizo nae alikuwa mjasiliamali mzuri aliyejenga nyumba yake sambamba na hilo soko hapo Mbeya mjini lililopewa jina lake, mwingine alikuwa akiitwa Binti Mausi huyu alikuwa Dodoma pamoja na wakina Mzee Alli Ponda naye alikuwa mjasiliamali akijishuhulisha zaidi na upikaji wa Pombe za kienyeji!! Nao pia walikuwa na tabia hiyo ya kuwapa watoto wadogo pesa!!!!
Ndinani,
Sikujua kama Bi. Fatima bint Matola alikuwa Muislam.

Ahsante kwa taarifa hii.
 
Allama Mohamed Said kwa upande wangu naona jibu ni jepesi sana, inawachoma kwa kuwa wengi wao walikuwa upande wa pili wa shillingi na hawana cha maana cha kuhadithia.

Umeongelea Marekani, kuna mada niliileta ya huko huko Marekani, nayo naona imekuwa mwiba kwao. Lakini kwa wenzetu huko, wengi sana wanaipokea kama historia kwa roho nyeupe kabisa kwa kuwa ni ukweli. Hii hapa...


Maalim wewe shusha vitu tu, tupo wengi tunaoithamini hii historia. Hawa wachache wasiofahamu maana ya historia wasikushughulishe sana, wape nondo tu kama kawaida yako.

Ma shaa Allah.
Haswaaa maana hata sisi tulichelewa kuzaliwa tunasoma katika kumbukumbu walizotutunzia wazee wetu kama kitabu kile cha WAISLAM AMKENI cha khalifa Khamisi na maisha ya Almarhum shekh kassim bin Jumaa lakini hatujatosheka,Mzee Mohamed ashushe nondo tu
 
Wakina mama wa Kimanyema walikuwa wajasiliamali sana ukiwafananisha na waume zao. Nawakumbuka wakina mama wawili wa Kimanyema; Binti Matola wa kule Mbeya ambaye ndiye alikuwa kinara wa TANU enzi hizo nae alikuwa mjasiliamali mzuri aliyejenga nyumba yake sambamba na hilo soko hapo Mbeya mjini lililopewa jina lake, mwingine alikuwa akiitwa Binti Mausi huyu alikuwa Dodoma pamoja na wakina Mzee Alli Ponda naye alikuwa mjasiliamali akijishuhulisha zaidi na upikaji wa Pombe za kienyeji!! Nao pia walikuwa na tabia hiyo ya kuwapa watoto wadogo pesa!!!!

= mjasiriamali
 
Back
Top Bottom