Waliomsindikiza Mwalimu Nyerere safari ya kwanza UNO 1955

Waliomsindikiza Mwalimu Nyerere safari ya kwanza UNO 1955

Nime

Nimeuliza wewe wapi? Maana umewataja "wa Msikitini" kama viile ni kitu kigeni sana kwako au cha ajabu. Kwa kejeli.

Hivi kukejeli mtu ambae hana imani kama yako kunakusaidia nini? Ndiyo imani yako ilikifunza hivyo au ni kibri tu?
Ilikifunza = Ilikufunza

Hivi huko madrassat ulienda kusomea upumbavu?
 
Yaani huyu Mzee atatapatapa sana mpaka mwisho ila hawezi kuibadili Historia kwa walioisoma tayari.

Nyerere is still an Icon.
 
Sasa nijibu na yale ya "history journal" na "anthropology" uliyoyaleta, si unakumbuka

Wewe ulitaka mimi niandike historia ya Mzee John nikakwambia huna haja ya kusubiri kwani imeishaandikwa bila bias yeyote ya udini na nikakupa reference sasa unataka nini zaidi sheikh!!!
 
Yaani huyu Mzee atatapatapa sana mpaka mwisho ila hawezi kuibadili Historia kwa walioisoma tayari.

Nyerere is still an Icon.
Azarel,
Sikuandika kitabu kuteremsha hadhi na mchango wa Mwalimu katika historia ya TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Ningekuwa mjinga wa kiasi hicho ningekiua kitabu changu na kisingekuwa hai hadi hii leo tukawa tunakijadili hapa na tunatoa matoleo.

Nilichokifanya mimi ni kusahihisha historia ya TANU kwa kuandika ule ukweli ambao wengi wenu hamkuwa mnaujua.

Kwa ajili hii basi hakuna swali la kutapatapa labda mwenye kuhangaika ni wewe ambae hujajiuliza hadi leo kuwa ilikuwaje historia ya TANU ikaandikwa hata isielezwe michango muhimu ya hawa wazalendo ambao sasa unawasoma hapa.

Angalia hapo chini matoleo tofauti ya kitabu hiki kwa Kiingereza na Kiswahili toka kitabu cha kwanza hicho cheupe kichwapwe London mwaka wa 1998.

Nadhani umepata picha ya heshima na hadhi ya kitabu hiki kwa wasomaji.

Moyo wako umejaa chuki hii imejitokeza namna unavyoniita kwa kejeli, "Huyu mzee..."

Ukishamtambua mtu kuwa ni mzee basi tambua anastahili kuheshimiwa kwa kile cheo chake cha uzee si kutukanwa.

Na kwa lipi nililokukosea?

Kwa kukueleza historia ya Abdul Sykes na Nyerere na kukufungulia nyaraka za kihistoria zilizosheheni historia ya TANU?
 

Attachments

  • SYKES BOOK ALL EDITIONS.jpg
    SYKES BOOK ALL EDITIONS.jpg
    54.1 KB · Views: 1
Wewe ulitaka mimi niandike historia ya Mzee John nikakwambia huna haja ya kusubiri kwani imeishaandikwa bila bias yeyote ya udini na nikakupa reference sasa unataka nini zaidi sheikh!!!
Hukuweka reference wala hukunukuu kilichoandikwa.

Ona ulichoandika...

"...ukienda kwenye Journal of history and Anthropology..."

Hiyo ndiyo "reference" au kututoa njiani?

Nikakuuliza kuna kipi katika hizo "references" zako kilichopingana na alichoandika Mohamed Said?

Ukawa huna la kujibu, mpaka dakika hii unapiga piga chenga tu. Njoo na historia "solid" si kubabaisha babaisha useme ndiyo historia.

Kwani Allama Mohamed Said hujamsoma anachokisema siku zote? Kuwa kaisoma historia iliyopo akakuta mapungufu au kwa lugha yako akakuta "bias" na yeye akaona aandike anayoyajuwa, aliyoyaishi, anaowajuwa kuweka sawa historia iliyopotosha ikapindisha ukweli au iliyowaacha wazalendo waliokuwa mstari wa mbele kuutafuta uhuru kabla hata ya Nyerere kuja Dar.

Na naam, historia aliyotuletea ni adhyim na adim na ndiyo kila akiingia humu mijadala yake hujaza watu wenye shauku za kila namna.

Huelewi hayo?

Wewe badala ya kuja na historia inayomuweka sawa alipopindisha au alipopaacha unakuja na porojo unatuambia kasomeni huko.

Tukasome badala ya kuonesha hii hapa umeandika kuhusu John Rupia ipo "biased" ukaweka "citation" ya ulichokisoma kuwa hakipo sawa. Huna. Nini huko ulichokiona ambacho kipya hata utupe kazi ya kupatafuta?

Kama wewe huna ulijualo si weka "citation" za huko ulipopaita "reference" yako ambayo siyo "bias", japo ya sentensi mbili tatu ili utukinaishe?

Tunasubiri. Nnauhakika tutasubiri sana kama njlivyokueleza juu huko. Wenzako miaka inakatika bado tunawasubiri sijuwi "wameingia mitini"? Bado wewe.

Tunasubiri.
 
Yeye hamfahamu kama wewe unamfahamu si useme ni nani. Pia si una wazee wako wanaweza mfahamu si uwaulize?

Mnataka kulazimisha kitu ambacho mtu hakielewi?

Mbona kaandika kuwa Daisy kwenyenkitabu chake ameandika kuhusu mama yake Nyerere kuwa alikuwa na duka la mafuta ya taa mtaa wa Livingston na Mchikichi kwani huyo bibi alikuwa akivaa baibui?
Labda ulimsoma ukiwa na kilevi kichwani. Mohamed hajawahi kuandika kuwa mama yake Nyerere alikuwa na duka mtaa huo. Aliyekuwa na duka ni mke wa Nyerere.
 
Labda ulimsoma ukiwa na kilevi kichwani. Mohamed hajawahi kuandika kuwa mama yake Nyerere alikuwa na duka mtaa huo. Aliyekuwa na duka ni mke wa Nyerere.
Ni kweli kabisa. Ni mimi ndiye nimechanganya mambo, Daisy kumwita mke wa Nyerere "mama" Maria Nyerere, kidole changu kikakataa kumwandika mke wa mtu "mama". tatizo si pombe au "kilevi" tatizo kuna mambo Kiswahili kinatuchanganya sana vichwa vyetu kukubali hususan sisi ambao haya mambo ya mke wa mtu kumuita "mama" fulani ni mwiko. Aah ni kinyume kabisa na "vocabulary" iliyopo kichwani mwangu. Nimerekebisha sentensi huko juu, isitupe shida. Toa neno "yake" weka Maria. Simpo.
 
Ni kweli kabisa. Ni mimi ndiye nimechanganya DAISY kumwita mke wa Nyerere "mama" Maria Nyerere) tatizo si pombe tatizo kuna mambo Kiswahili kinatuchanganya sana vichwa vyetu kukubali hususan sisi ambao haya mambo ya mke wa mtu kumuita "mama" fulani ni mwiko. Aah ni kinyume kabisa na "vocabulary" yangu iliyopo kichwani mwangu. Nitarekebisha sentensi huko juu, isitupe shida. Toa neno "yake" weka Maria. Simpo.
Sijui kwanini mnapenda sana majina ya kikristo nyie mabinti wa kiislam! Daisy, jina la kikristo japo yeye Islam. Wewe, jina lako la kikristo. Mliishiwa majina ya kiislam?!
 
Sijui kwanini mnapenda sana majina ya kikristo nyie mabinti wa kiislam! Daisy, jina la kikristo japo yeye Islam. Wewe, jina lako la kikristo. Mliishiwa majina ya kiislam?!
Daisy ni jamii ya maua ambayo hayana msimu wala muda wa kuchanua, utayakuta wakati wote yamechanua tu. Sasa kama mmea nao upo usio wa Kiislam hilo sijasikia. Mimi naamini mimea yoye ni ya Kiislam.

Hapo sasa.
 
Ni kweli kabisa. Ni mimi ndiye nimechanganya mambo, Daisy kumwita mke wa Nyerere "mama" Maria Nyerere, kidole changu kikakataa kumwandika mke wa mtu "mama". tatizo si pombe au "kilevi" tatizo kuna mambo Kiswahili kinatuchanganya sana vichwa vyetu kukubali hususan sisi ambao haya mambo ya mke wa mtu kumuita "mama" fulani ni mwiko. Aah ni kinyume kabisa na "vocabulary" iliyopo kichwani mwangu. Nimerekebisha sentensi huko juu, isitupe shida. Toa neno "yake" weka Maria. Simpo.
Isome sura Al-Mujaadila, imeruhusu.
 
Isome sura Al-Mujaadila, imeruhusu.
Hiyo isome wewe inatosha. Mimi siifahamu.

Hata mimi naruhusu ndiyo maana nikarekebisha.

Isipokuwa,kuna sura ya Qur'an, sura ya 58, inaitwa AL - MUJAADALAH

Kama ulimaanisha hiyo unaweza kuisoma na tafsiri yake hapa... Al Mujaadalah
 
Old tales
Azarel,
Sikuandika kitabu kuteremsha hadhi na mchango wa Mwalimu katika historia ya TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Ningekuwa mjinga wa kiasi hicho ningekiua kitabu changu na kisingekuwa hai hadi hii leo tukawa tunakijadili hapa na tunatoa matoleo.

Nilichokifanya mimi ni kusahihisha historia ya TANU kwa kuandika ule ukweli ambao wengi wenu hamkuwa mnaujua.

Kwa ajili hii basi hakuna swali la kutapatapa labda mwenye kuhangaika ni wewe ambae hujajiuliza hadi leo kuwa ilikuwaje historia ya TANU ikaandikwa hata isielezwe michango muhimu ya hawa wazalendo ambao sasa unawasoma hapa.

Angalia hapo chini matoleo tofauti ya kitabu hiki kwa Kiingereza na Kiswahili toka kitabu cha kwanza hicho cheupe kichwapwe London mwaka wa 1998.

Nadhani umepata picha ya heshima na hadhi ya kitabu hiki kwa wasomaji.

Moyo wako umejaa chuki hii imejitokeza namna unavyoniita kwa kejeli, "Huyu mzee..."

Ukishamtambua mtu kuwa ni mzee basi tambua anastahili kuheshimiwa kwa kile cheo chake cha uzee si kutukanwa.

Na kwa lipi nililokukosea?

Kwa kukueleza historia ya Abdul Sykes na Nyerere na kukufungulia nyaraka za kihistoria zilizosheheni historia ya TANU?
 
Old tales
Azarel,
Iwe iwavyo mimi nimepata faraja kuwaeleza yale niyajuayo kuhusu historia ya TANU.
Nashukuru kuwa nimeweza kuandika kitabu na kimependwa sana.

Lakini kubwa linalonifurahisha ni kuwa nimeweza kusimama kwa hoja na kila aliyejaribu kunipinga na mwisho wa siku wote nawaacha hawana kitu labda kukimbilia kunitukana na kunikejeli lakini hajatokea yeyote wa kuja na historia nyingine isiyo hii.

Abdul Sykes hamkuwa mkimjua nimekupeni kitabu kizima.
Leo mnamjua na mnajua kuwa nyumba yake ndiyo ilikuwa ngome ya mipango yote.

Hamkuwa mnajua vipi Nyerere aliingia katika uongozi wa TAA nimekupeni yote yaliyopitika Nansio na katika Ukumbi wa Arnautoglo nk. nk. nk.

Mwisho kwa kukosa hoja umejibu bandiko langu nilikuwekea historia ya matoleo ya kitabu hiki kwa Kiingereza na kwa Kiswahili kurekebisha historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika kwa maneno mawili, ''Old Tales.''

Kejeli za kitoto.

Indeed old tales.
You have all of you failed to steal my thunder.

1571945143376.png
 
Kwani Allama @Mohamed Said hujamsoma anachokiswma siku zote

Hapo ulipoandika " anachokiswma" ndio lugha gani, kimanyema?

Mmezoea kutafuniwa sasa nimekwambia nenda huko kwenye " JOURNAL OF HISTORY AND ANTHROPOLOGY" utakuta unachotaka niandike ! Kama unajua kutafuta taarifa kwenye maandiko hiyo taarifa ni tosha kabisa kukuwezesha kupata ukitafutacho.

Mzee John ameacha jumba la ghorofa pale Msimbazi kama ukumbusho na mali nyingine nyingi.
 
Hapo ulipoandika " anachokiswma" ndio lugha gani, kimanyema?

Mmezoea kutafuniwa sasa nimekwambia nenda huko kwenye " JOURNAL OF HISTORY AND ANTHROPOLOGY" utakuta unachotaka niandike ! Kama unajua kutafuta taarifa kwenye maandiko hiyo taarifa ni tosha kabisa kukuwezesha kupata ukitafutacho.

Mzee John ameacha jumba la ghorofa pale Msimbazi kama ukumbusho na mali nyingine nyingi.
Ndinani,
Ungeboresha hiyo rejea kama unayo ili iwe rahisi kuipata.

John Rupia gorofa lake ni maarufu Mtaa wa Kitchwele na Msimbazi.

Lakini lipo pia Gorofa la Sheikh Said Chaurembo Mtaa wa Msimbazi na Congo nalo pia linafahamika mji mzima kwa kituo chake cha mabasi toka enzi za DMT watu wakikitambua kama Kwa Chaurembo na hili jina limebakia hadi leo.

Sheikh Chaurembo alikuwa mwaka wa 1950 katika TAA Political Subcommittee pamoja na Sheikh Hassan bin Ameir, John Rupia na vijana Abdul Sykes, Hamza Mwapachu, Dr. Vedasto Kyaruzi na Steven Mhando.

Picha hiyo hapo chini ni Sheikh Said Chaurembo na Liwali Ahmed Saleh.
 

Attachments

  • SHEIKH SAID CHAUREMBO.jpg
    SHEIKH SAID CHAUREMBO.jpg
    43.5 KB · Views: 2
Ndinani,
Ungeboresha hiyo rejea kama unayo ili iwe rahisi kuipata.

John Rupia gorofa lake ni maarufu Mtaa wa Kitchwele na Msimbazi.

Lakini lipo pia Gorofa la Sheikh Said Chaurembo Mtaa wa Msimbazi na Congo.

Wakina mama wa kimanyema nao walijitahidi kujenga vibanda vingi hapo CARRY AND GO kutokana na biashara ya vitumbua;; nyie wajukuu zao mmeviuza kwa Wapemba ili mkatangaze ufalme bar!!!
 
Wakina mama wa kimanyema nao walijitahidi kujenga vibanda vingi hapo CARRY AND GO kutokana na biashara ya vitumbua;; nyie wajukuu zao mmeviuza kwa Wapemba ili mkatangaze ufalme bar!!!
Ndinani,
Mimi huwa siwezi mjadala wa hii namna yako.
 
Hapo ulipoandika " anachokiswma" ndio lugha gani, kimanyema?

Mmezoea kutafuniwa sasa nimekwambia nenda huko kwenye " JOURNAL OF HISTORY AND ANTHROPOLOGY" utakuta unachotaka niandike ! Kama unajua kutafuta taarifa kwenye maandiko hiyo taarifa ni tosha kabisa kukuwezesha kupata ukitafutacho.

Mzee John ameacha jumba la ghorofa pale Msimbazi kama ukumbusho na mali nyingine nyingi.
Hapo pasikutishe. Tazama keyboard yako ilipo e na w utaelewa kuwa hiyo ni "typo" tu. Na hata hivyo ahsante kwa kunitanabahisha, nimerekebisha.

Historia hiyo unayoisema kama vile inapingana na aliyoileta Allama Mohamed Said haipo. Kama ipo iweke hapa. Mbona Mohamed Said anaweka vitu hapa hapa na kila mtu anajisomea? Kinakushinda nini?

Uliahidi tusubiri bado tunasubiri.

Kama huna sema tu huna. Acha porojo.
 
Back
Top Bottom