Waliondamana Dar es Salaam kupinga mkataba wa bandari wakamatwa na polisi. Mratibu wa maandamano na wenzake 10 wanahojiwa na Polisi

Waliondamana Dar es Salaam kupinga mkataba wa bandari wakamatwa na polisi. Mratibu wa maandamano na wenzake 10 wanahojiwa na Polisi

Ni raha sana kutawala Taifa ambalo wengi wa wananchi hawana uelewa( wajinga wengi_, mtu atakwambia kwani hiyo Bandari ntaila? inanihusu nn ? mie napigania ugali wa wanangu bwana, nikaandamane afu wanivunje miguu nani atanitibia na kuwalisha wanangu nikiwa rumbande ama jela 😀 😀

Sasa hata mimi nginekuwa Rais hapo nachekelea tu, siku zinasonga mbele.
 
Ni raha sana kutawala Taifa ambalo wengi wa wananchi hawana uelewa( wajinga wengi_, mtu atakwambia kwani hiyo Bandari ntaila? inanihusu nn ? mie napigania ugali wa wanangu bwana, nikaandamane afu wanivunje miguu nani atanitibia na kuwalisha wanangu nikiwa rumbande ama jela 😀 😀

Sasa hata mimi nginekuwa Rais hapo nachekelea tu, siku zinasonga mbele.
Umenena kweli sn mkuu
 
Halafu wananchi wenyewe wanashangaa hata hawaelewi kinachoendelea, ukute wengine walijua movie inaigizwa🤣🤣🤣

Sema nini, wabongo tunavimba sana nyuma ya keyboard, location mambo tofauti sana🤣🤣🤣
Mimi Leo kila nnae muuliza kuhusu maandamano ananiuliza Mimi .. maandamano kuhusu nini??

Watu hawataki kabisa kusumbuana na serikali.....kila mtu anawaza kuiba upande wake .🤣🤣🤣🤣
 
Vijana waandamana jijini Dar es Salaam Tanzania kupinga mkataba wa bandari kati ya serikali na Dubai Ports World pamoja na muswada wa marekebisho ya sheria ya Usalama wa Taifa.

Vijana walioandamana jijini Dar es Salaam kupinga mkataba wa Bandari wamekamatwa eneo la Mnazi Moja.


========

WALIOANDAMANA WAISHIA MIKONONI MWA POLISI

Taarifa za awali zinaeleza kuwa vijana waliokuwa wameandamana kupinga Mkataba wa Bandari eneo la Mnazi Mmoja kuelekea Ikulu ya Magogoni Dar es salaam wamekamatwa na Jeshi la PolisiTaarifa zaidi zitawajia endelea kutufatilia.


MRATIBU WA MAANDAMANO AINGIA MITINI

Jeshi la Polisi limewakamata baadhi ya vijana waliojitokeza kuandamana kupinga mkataba wa ushirikiano wa uendeshaji wa bandari kati ya Kampuni ya DP World na Tanzania.

Hata hivyo, a mratibu wa maandamano hayo, Deus Sokkatika hali ya kutofahamika, hajatokea kwenye maandamano hayo yaliyopangwa kuanzia Temeke na kuishia Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Mwananchi Digital ilipomtafuta kwa simu zake zote za kiganjani, hakupatikana na katika majina ya waliokamatwa na polisi pia jina lake halikuwepo.

Juni 15 mwaka huu Deus Soka ambaye aligombea udiwani katika Uchaguzi Mkuu wa 2020, alitangaza kuitisha maandamano kupinga mkataba wa ushirikiano wa uendeshaji wa bandari kati ya Kampuni ya DP World na Tanzania.

Hata hivyo Juni 17 Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam likipiga marufuku maandamano hayo na kueleza kuwa, mtu aliyeandaa maaandamano hayo ameshajibiwa kwa barua akielezwa ni marufuku kufanyika maandamano yoyote.

Juni 10, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha azimio kuhusu pendekezo la kuridhiwa kwa mkataba baina ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai kwa lengo la kuanzisha ushirikiano katika uendelezaji wa maeneo ya bandari nchini.

Pendekezo hilo liliwasilishwa bungeni Juni 10, na kupitishwa na Bunge baada ya wabunge kupata fursa ya kuchangia na kuishauri Serikali kuhusu mkataba huo.


Mwananchi

PIA, SOMA:
- Vijana kufanya Maandamano kupinga Mkataba wa Bandari kati ya Tanzania na kampuni ya DP World ya Dubai
- Polisi yapiga marufuku maandamano ya kwenda Ikulu ya Magogoni, Dar es Salaam, Jumatatu Juni 19, 2023
Dada jasiri kabisa. Jina lake? tuomtoe Rumande.

Polisi Tanzania muwe wazalendo, mwachiane dada na wote mliowakamata. Wanaopigania maslahi yenu na familia zenu kwa miaka 100 inayokuja.
 
Back
Top Bottom