Waliosema Tanzania ni miongoni mwa ligi tano bora Afrika wajitafakari

Waliosema Tanzania ni miongoni mwa ligi tano bora Afrika wajitafakari

Kidagaa kimemwozea

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2018
Posts
3,680
Reaction score
6,554
1675569179475.jpeg


Mtandao uliotoa takwimu na kusema Tanzania inashika nafasi katika ligi tano Bora Afrika bila kujali Kigezo walichotumia huenda takwimu hizo zilisukumwa na aidha kutokuwa na taarifa sahihi kuhusu ligi za Afrika, au mitazamo na mihemko binafsi au labda alitumia Kigezo cha kuwa na mashabiki na followers wengi katika mitandao ya kijamii. Unapozungumzia ligi hauongelei timu moja au mbili Bali vilabu vyote vinavyoshiriki ligi kuu pengine na ligi nyinginezo za chini.

Nalubaliana na hoja kuwa tanzania inaweza kuwa na vilabu Bora kimoja au viwili lakini hatuna ligi Bora. Ligi yetu haijawahi kutoa wachezaji Bora Afrika Wala wachezaji wakutumainiwa Sana katika timu zao za Taifa (wanaoweza kufanya makubwa kwenye mashindano katika timu zao za Taifa)

Ligi yetu bado inahitaji uwekezaji mkubwa ili timu zote zimudu kuwa na wachezaji Bora kutoka kila pembe ya Dunia.

Tukiwa na ligi Bora hata timu yetu ya Taifa utapata ahueni. Hauwezi kuwa na ligi Bora then ukose timu ya Taifa Bora. Aidha linapokuja suala la ushindani ligi yetu bado Sana. Ushindani upo baina ya vilabu vikubwa viwili kwa miaka mingi huo ubora uko wapi? Je, manufaa ya ubora huo yako wapi?

Ikiwa hata timu yetu ya Taifa ambayo inawachezaji wengi wanaocheza ligi ya tano Bora Afrika wanashindwa kufuzu Chan?

Chanzo masshele.com
 
Waingereza walituachia umbea na ligi timu la taifa bovu.. 😂 😂

Kwanza napinga kuwa namba 5',
Ligi za misri, morroco, algeria, tunisia, South Africa, angola, sudan zinapaswa kuwa juu yetu.

Pili ligi yetu inang'arishwa na wachezaji wa kigeni, hilo ndilo tatizo.
Wazawa hatuna jambo.. Na hata hao wazawa wanaofanya vizuri, ukiwaweka pamoja wanavyocheza utacheka. 😂
 
View attachment 2506865
Mtandao uliotoa takwimu na kusema Tanzania inashika nafasi katika ligi tano Bora Afrika bila kujali Kigezo walichotumia huenda takwimu hizo zilisukumwa na eidha kutokuwa na taarifa sahihi kuhusu ligi za Africa, au mitazamo na mihemko Taifa ambayo inawachezaji wengi wanaocheza ligi ya tano Bora Afrika wanashindwa kufuzu Chan?
Chanzo masshele.com
Umeandika andiko losilo na mashiko hata kidogo.
 
Waingereza walituachia umbea na ligi timu la taifa bovu.. [emoji23] [emoji23]

Kwanza napinga kuwa namba 5',
Ligi za misri, morroco, algeria, tunisia, South Africa, angola, sudan kusini zinapaswa kuwa juu yetu.

Pili ligi yetu inang'arishwa na wachezaji wa kigeni, hilo ndilo tatizo.
Wazawa hatuna jambo.. Na hata hao wazawa wanaofanya vizuri, ukiwaweka pamoja wanavyocheza utacheka. [emoji23]
Sudan kusini? Mkuu upo serious kweli? Yani ligi ya kina fc zalan iwe juu yetu
 
Uje na matokeo ya utafiti wako..sio kulabdia.
 
Waingereza walituachia umbea na ligi timu la taifa bovu.. [emoji23] [emoji23]

Kwanza napinga kuwa namba 5',
Ligi za misri, morroco, algeria, tunisia, South Africa, angola, sudan zinapaswa kuwa juu yetu.

Pili ligi yetu inang'arishwa na wachezaji wa kigeni, hilo ndilo tatizo.
Wazawa hatuna jambo.. Na hata hao wazawa wanaofanya vizuri, ukiwaweka pamoja wanavyocheza utacheka. [emoji23]
Unajua kwamba ligi ya Sudan imesimama muda mrefu?
 
Ujinga tupu... Ko ulitaka usikie ni ya 54 kwa ubora ili uje uponde hapa??.
Unatakiwa ufanye mambo kisomi. Ukiletewa utafiti nawe unatakiwa uipitie na ujidhihirishe kama kweli ni sahihi.
Kiufupi huo utafiti siyo sahihi
 
Back
Top Bottom