Waliosoma Jitegemee Secondary School hebu ingieni hapa Tusalimiane

nakumbuka vizuri maisha ya JITE, siwezi kuwasahau Masemele, Madilu mzee wa tai za vitobo, Babu Mafunguo, Mrimi Mnandi, Afande Ismaili, Afande Bruno, Afande Tall, mpiga picha P.DIDI, bila kusahau Mkisi Program

Mkuu Mrimi Mnandi alitangulia mbele za haki Huyu jamaa alikuwa bingwa wa kuandaa Study Tour
 
Member wa Jitegemee kuanzia 1993 mpaka 1996
Mkisi kaanzia siku nyingi kufundisha civics na misifa yake
Wakati tunasoma pale Bwenge alikuwa na binti yake anasoma palepale
Mkuu tumesoma wote, ila nilikuwa mchepuo wa Sayansi.....
Nilikuwa maarufu sana hapo shuleni maana nikiamua kutoroka natorokea getini na sijawahi kukamatwa. Walioniiga walikuwa wanaishia kupata alama za kudumu.


Nakumbuka tuliifunga Tambaza that day ndo balaa likaanza. Kwa wasiofahamu ni kwamba Vurugu ile ndo ilipelekea Tambaza kubadilisha mchepuo kutoka Olevel to Alevel. Nilikuwepo ktk wanafunzi waliokwenda Tambaza kuwatambua vinara wa vurugu.

Mrimi ameshatangulia mbele ya haki mkuu. Bruno tumbo mzee wa beetle!! Hahahaa...lafudhi ya huyu jamaa ni vituko aise.
Alikuwa Mwalimu wangu wa Darasa. Alikuwa ananimaind sana maana nilikuwa natengua maamuzi yake mengi sana (nilikuwa Kiranja) ya kionevu. Alipenda totoz hivyo wakimzingua darasa zima mnakuwa msambweni.

Mnamkumbuka Castory Ponella? Alimaliza 1996 Olevel (nilimaliza naye) alikuja kupata kesi ya mauaji ya yule msanii wa Bongo Fleva katika ugomvi, amekaa jela tangu miaka hiyo na ametoka last year mwezi wa tisa.


Mkuu Mrimi Mnandi alitangulia mbele za haki Huyu jamaa alikuwa bingwa wa kuandaa Study Tour
Kuna safari moja tulikwenda Manyara kisha Ngorongoro same trip. Tuliongozana naye na Wajadi kama wakuu wa msafara, kuna dogo mmoja (siku hizi ras maarufu ana kiwanda cha kutengeneza vikoi) alikamatwa na puli kumi za bangi pale Mto wa Mbu. Alizichukua Wajadi kama kidhibiti ila hazikufika Dar, jamaa alizipuliza zote....

Naikumbuka JITEUTE ya Massawe ilikuwa full vipaji na taaluma. Mnawakumbuka GWM? Wale mapacha akina Makalla. Tulianza nao njuka hadi form four.... Siku hizi mmoja hajitambui kwa uteja

 
Mkuu Paw mbona na mimi nilikuwa mchepuo huo huo wa Science
Kweli mkuu Jiteute ilikuwa enzi za Massawe na akina Bwenge na yule mama wa Skauti nimemsahau jina na vipaji lukuki na nkumbuka matokeo yetu ya Form four 1996 ndo yalikuwa ya mwisho mazuri kwa upande wa Olevel na baada ya hapo na baada ya Massawe kuondoka shule ikaanza kuporomoka kutokana na utozi mwingi
Tufahamiane Mkuu Paw
 
Last edited by a moderator:
Hahahaha nimecheka hapo kwenye Bold mkuu. Inawezekana tunafahamiana ila bahati mbaya haya masecurity yetu JF hayavunji ukuta wa kujua who is who.

Yule mama anaitwa Anyitike. Nadhani unamkumbuka, pia nilikuja kupata taarifa kuwa afande Kihimbi alikuja kufariki ghafla baada ya kuanguka akikimbiza denti Smart Area. Kifua kilikuwa amekopesha kampuni ya sigara.

Unakumbuka zile bakora zilizokuwa zinaletwa na fuso? Dah ile shule ilitupatia nidhamu za maisha kweli kweli
 


Year uko right mkuu ni Mama Anyitike na wanasema yule mama hakuwahi kuwa na mtoto ndo maana alikuwa mkali vibaya sana nanasikia pia Mama Lyimo alishafariki pia mkuu
Unamkumbuka yule mwalimu wa Biology alikuwa akija darasani hashiki chaki kwa ajili ya kuogopa kuchafuka achana na Mama Mnzava aliyekuwa bingwa wa Bios sanapale Jiteute
halafu unakumbuka Form Four moja ya biashara nafikiri ni D1 wakati huo sisi tukiwa Form IV C1 ilikuwa ya matoz wakiingia darasani wana perfume na vitana na brush wakitoka ile mchana huwezi jua ndo wanaingia au wanatoka maana ni wasafi mbaya na walimu walikuwa washajua darasa lile ni la matoz so wakiingia kufundisha waelewe wasielewe hakuna anayejali
Nimekutajia na darasa mkuu unaweza pata picha
Nakuja PM mkuu Paw
 
Last edited by a moderator:
Yule mwalimu bishoo alikuwa anaitwa Mpeta (nadhani ni chemistry)..... Mama Mnzava ndiye alinifundisha Biology. Nakumbuka Ktk Reproduction nusu ya mabinti walitega shule siku hiyo....

Kumbuka darasa ambalo lilishawahi kumtoa baruti afande Tall (Form Four)
 


Mkuu achana na Mpeta kuna mama pia wa Bios alikuwa bishoo mbaya yaani hashiki chaki na hataki kuchafuka na hamalizi hata muda wake wa kipindi

Sisi tulikuwa tukiingia mchana tukijua siku hiyo kuna Bios tunawahi asubuhi vipindi vya mama Mnzava tunakula shule ya uhakika na huyo mama bishoo akiingia tunasikiliza tuu hakuna hata kuandika lolote
Nimekumbuka sana Mkuu nyie mlikuwa balaa
Ila tumekula sanastick aise za Jiteute dah ile shule ilinifundisha mengi sana
 
Yeah namkumbuka yule mama. Alikuwa mnataji sana aisee. Jinale limenitoka maana hakuwahi kutufundisha sisi. Mabada unamkumbuka? Mzee wa Fizikia.

Darasa letu tangu january hadi desemba halikuwahi kuwa na wanafunzi wote kufika kwa pamoja, ajabu tulifanya vizuri sana kwenye papers. Namkumbuka JINIAZ Jeremiah alitutesa kwenye sayansi kinoma ila National alipata namba isiyo njema kuitaja hadharani. Nilikutana naye yupo AIRTEL sijui kama bado anapiga kazi pale

 


C1 walikuwa wanoko ni lazima kila siku darasa lijae na tulikuwa hivyo toka form three na tulikuwa kwenye final examstunapishana point aise jamaa walikuwa na usongo wasomaji kwa kwenda mbele hawakosi kipindi namuda wote wanajisomea
Wengi walienda Alevel japo wengine Maths ilikataa tukajikuta tunaenda Arts na sio Science
Mabada kweli wewe una kumbukumbu nawatu wengi
Wengine tulikuwa tunakutana nao baada ya pale Jiteute hata salam kukupa ni issue ikawa kama sijui ni sisi tulifanya matokeo yao yasiwe mazuri
Namtafuta sanarafiki yangu mmoja Fortunatus Boniface alikuwa D2 yaani toka tumalize Jiteute sijawahi msikia wala kumuonana somebody Victor Hitler alikuwa C1 pia
 

Hahahahaaa....na adhabu kali kali kama push up uwanja wa damu pale...vipi siku hizi, mwanao shule anasoma utakubali atiwe stick kama za Wajadi au Ndyamukama?!
 
Nikukumbushe
utukutu sie wengine tulianza nao tangu kidato cha kwanza. Unakumbuka issue ya Francis Rweyemamu? jamaa alikuwa mnoko kweli tukaweka mpango na kumkamatisha na kesi ya kubaka kule Interchick? Unakumbuka Francis Tall aliyerith nafasi yake hakudumu hata miezi miwili? Unakumbuka Mwal. Mwakasege aliyekuwa ananyanyasa wanafunzi alipokuwa Discpline Master?

Daah nakumbuka hiyo michongo tuliifanya kisomi kweli kuondoa kiwingu cha kufukuzisha watu shule. Sikwambii tulifanyanye ila tulifanikisha mambo kimya kimya...

Shule ile sitaisahau ilinifundisha mengi. Unapigishwa kwata hadi unachafuka chapachapa lakini kesho lazima uje unang'ara...
 
Hahahahaaa....na adhabu kali kali kama push up uwanja wa damu pale...vipi siku hizi, mwanao shule anasoma utakubali atiwe stick kama za Wajadi au Ndyamukama?!
Kulya hapana aise zile zilikuwa sio adhabu bali mauaji
Kuna jamaa walitoroka kipindi cha dini bana wakakimbilia uwanja wa taifa kule wakakamatwa walivuliwa mashati saa sita za mchana wakalazwa vifua wazi pale uwanjani mpaka kipindi cha dini kikaisha
Wengine walikamatwa wakalowekwa kwenye mitaro ya maji machafu
Akina Bwenge na Wajadi ni balaa aise
 
Last edited by a moderator:
Paw wengine hatukuwa watukutu ila stick za akina Bwenge na Wajadi hatukuziepuka
Adhabu za wale maafande wa pale getini nazo hatukuepuka maana unafanya makosa darasani mwalimu anakuja kukukabidhi kwa maafande wa pale getini unapewa adhabu mbaya kabisa yaani hata kupanda gari kurudi home ni issue na kesho yake unatakiwa kuwa smart na uko darasani
Kiranja Mbise alivyokuwa mnoko na kunyang'anya watu sox na vitambaa na mabag na sweta ambazo sio za shule zikienda staff mwisho wa mwaka wanagawana
 
Last edited by a moderator:

kumbe unawakumbuka wale madogo.....halafu ktk kundi lao kulikuwa na dogo mwingine mtukukutu sana kwa jina la abuu,alikuwa anaishi kinondoni.kuna siku moja 2001 nilipiga feni home na kwenda kuliuza kkoo pale round about kwa wauza redio na vifaa vya umeme vilivyo tumika.lengo hasa ilikuwa ni kusaka mshiko wa kuingia ktk show ya manduli mobb kule ktk ukumbi wa jkt unaotumika kufanyia sherehe mbalimbali za kijamii.na ktk show hiyo walitangaza uwepo wa juma nature na duly sykes.basi nikaawachia wale jamaa wa kkoo ile feni yangu kwa ahadi kwamba after two days nipite kuchukua changu kama elfu 30 hivi.kila nikitoka shule jioni napita kkoo kuulizia mshiko wangu,jamaa wakawa wananizungusha tuu.baada ya wiki moja nikakata shauri.nikampa mchongo mzima abuu.abuu akaniambia mbona hiyo issue ndogo tuu.aka-organize watukutu wenzie kama watano hivi ili tukafanye ambush kkoo.ile jioni tunatoka tu jite,tukajikusanya na kudandia daladala hao kkoo kufata haki yangu.kilicho tokea dont miss part II.
 
zile stiki zilikua ni noma zinatoka maporini kule yani siwezi kumsahau wajadi nilikula stiki siku hiyo aliyonikamata getini siku tatu nilikua siwezi kukaa kwenye kitu kigumu!nikamwambia mshua mi ile shule tena basi !washua wetu wakitambo kile siunawaelewa tena akaniambia utasoma hapo hapo vaa uende shule,ila ndiyamukama alikua hatari sana nasikia wale waliitangulia kumaliza walimvunja mguu lakini bado balaa lake tuliliona!1998 na kuendelea
 
namkumbuka sana marehemu mbonabucha yule mlemavu wa mguu alikua mtaalam sana!wapi kaboka mchizi jina lake halisi limenitoka kidogo yule ticha wa civics
 

Mkuu hiyo Part II itakuwa lini?
 

mkuu Part II bado tu Haijatoka?
 

mkiso sasa ni mkuu wa Jkt mafinga bro!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…