Waliosoma shule za Ufundi (Technical schools) Tukutane hapa

Waliosoma shule za Ufundi (Technical schools) Tukutane hapa

Kwa uzoefu wangu watu waliosoma vyuo vya ufundi diploma ukimuweka na PCM aliyeiva na kuzoea kukata nyanga huyu ndugu wa ufundi hawezi furukuta kwenye theory ,ni wazuri kwa practical ila ni wachovu sana kwenye hesabu,ila wanaweza sana kazi za maabara ,bahati mbaya elimu yetu ya juu module nyingi ni kumeza meza
I was luck enough to get both,unapigwa theory then unapewa zana za vita mpk ucku wa manane huondoki mpk practical ifanye kazi trust me imenisaidia sn kimaisha
 
Mimi ni miongoni mwa mazao ya shule za Ufundi... nilipigaga Iyunga miaka kadhaa nyuma hapo...

Nazikubali sana hizi shule...
Nilijifunza mambo mengi sana...

Na kwa sasa mimi Ni Engineer katika Taasisi fulani napiga kazi...

Big up sana kwa Technical Schools..

Hususani Iyunga Boys Technical Secondary School.. wenyewe tulikuwa tunaiita Eunger Large Complex Camp....🤝🤝
 
Partical ya Moshi Technical nipo hapa from KARUME 33.

Moto " KUTII, KUWAJIBUKA NA KUZIBUNI MBINU ZA KAZI"

Nimesoma Plumbing (CIVIL).
Engineering science ilinifanya niione Mechanics ya Advance ni nyepesi sana wakati wenzangu wanalia.
Dah...sikuwahi kuishi wala kuipenda Karume labda ni kwa sababu iko karibu na Zanzibar😂😂😂
Nimeishi Mkwawa 19 kisha Azimio 10 halafu Lumumba 14 na 202

Namkumbuka Malale, Koba, Mpande na wengineo😂😂😂
 
hongera nahisi utakua the best sababu ya Technical drawing kuijua toka mdogo hivyo kuwatia vibao jamaa wa special na Private huko chuo (Engineering school)

Si kweli. Mimi nilisoma umeme wakati nipo O-Level. Kulikuwa na vipindi vya practical na tuliingia workshop ambapo mnauda circuits tofauti kwenye meza zilizo na mbao maalumu Kwa ajili ya kugunga vifaa vya umeme.

Pia Mwl. Urban Nguli alikuwa anapewa kazi mtaani na alikuwa akituchukua kufanya kazi hizo Kwa mikono yetu kisha anakuja kukagua.

Mfano Kuna wakati Fulani alipata kazi ya kufanya marekebisho ya mfumo wa umeme pale Chuo Cha Ualimu. Alituita na tukaenda kupiga show kama kawaida.

Hii ilinifanya niwe napiga hela hata nikiwa likizo nyumbani. Huyu Mwalimu alituhimiza pia kuwa tufanye Ile mitihani ya Trade Test ya VETA. Yaani nilikuwa Certified Electrician hata kabla sijamaliza Secondary School.
Hao ndio walimu sasa. Sio hawa tunaoshinda nao bar kila siku
 
Naliona bweni langu la Jamhuri pale. Niliishi Cell D. Huo uwanja wa basketball upo karibu na town way pale Kwa Mbunge Kanjibai njia ya kuelekea Coast.

Miaka hiyo ilikuwa usafiri wa uhakika kwenda Mtwara ni meli tu. Barabara haikupitika kirahisi.

Mwalimu Mnelamwana alishawahi kunipa adhabu ya kung'oa visiki kule forest kama unaenda chuo Cha ualimu ufundi. Alifanya kurusha jiwe na kusema mwisho wa adhabu yako ni pale na ukimaliza adhabu uje kuripoti. Sikwenda kuripoti maana ilikuwa ni mtego wake kwani ukienda kuripoti huwa anakuja kukagua na kurusha Tena jiwe huku akisema mwisho wa adhabu yako sio hapa bali ni pale (anarusha jiwe upya).

All in all, hapa nilijifunza discipline kwenye maisha. Kwa sasa Mimi ni Civil Engineer.
Mje muitembelee shule shule yenu sasa
Sasa hivi madogo wanakula practical za kutosha.
 
IYUNGA TECHNICAL SECONDARY SCHOOL
 
Mnatumia vitabu vimetungwa enzi za mjerumani kina mambo mengi balaa.

mashine ticha kaificha tu inapigwa na vumbi tu ofisini, hamtumii.

Kuna ticha anaitwa mwakasege pale iyunga wa welding, yule wanafunzi wake alikuwa anawafundisha mpaka practical. Naamini wale jamaa wakitoka pale wanaweza kujiajili.
Mwakasege a.k.a Kyege.
 
Mnatumia vitabu vimetungwa enzi za mjerumani kina mambo mengi balaa.

mashine ticha kaificha tu inapigwa na vumbi tu ofisini, hamtumii.

Kuna ticha anaitwa mwakasege pale iyunga wa welding, yule wanafunzi wake alikuwa anawafundisha mpaka practical. Naamini wale jamaa wakitoka pale wanaweza kujiajili.
Hakika... Mwakasege alikuwa mwalimu mzuri sana wa somo la Welding & Metal Fabrication...
Na pia mtalaam kwelikweli wa mpira wa Kikapu... Iyunga was best kwenye kikapu...

Kuna jamaa zangu waliiva sana kwenye kikapu, mpaka timu za hapa Dar niliwahi kuwaona kipindi fulani wakikimbiza kikapu...
 
Musoma technical hiyo!.. Bweni urafiki na chemba ni lunduno!.. Kuna ticha alikua mkuda sana wakuitwa "kutiki" bila kumsahau "mnyeti"!.. Ukiwa na kosa kwa hao wakuda na ukifikishwa kwa kilonda ni UMEISHAAAA
 
Musoma technical hiyo!.. Bweni urafiki na chemba ni lunduno!.. Kuna ticha alikua mkuda sana wakuitwa "kutiki" bila kumsahau "mnyeti"!.. Ukiwa na kosa kwa hao wakuda na ukifikishwa kwa kilonda ni UMEISHAAAA
Hawakosagi hao kila shule wapo
 
Back
Top Bottom