Wamachinga wamkumbuka Magufuli na Antony Mtaka kwenye Ugawaji wa Maeneo Soko jipya la Machinga Dodoma kwa kuwekwa wasiokuwepo na wao kukosa

Wamachinga wamkumbuka Magufuli na Antony Mtaka kwenye Ugawaji wa Maeneo Soko jipya la Machinga Dodoma kwa kuwekwa wasiokuwepo na wao kukosa

ryan riz

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
423
Reaction score
683
Ikiwa zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya soko jipya la machinga linaendelea, ila limegubikwa na sintofahamu tokana na zoezi hili

Kipindi cha awali wamachinga wanaofanya biashara soko la jioni Nyerere square waliandikishwa kwa usimamizi madhubuti wa aliyekuwa mkuu wa mkoa Antony mtaka kuhakikisha hakuna upendeleo kwa wote wanaofanya biashara maeneo hayo.

Kipindi yupo majina yalitoka na watu waliona majina yao.waliitwa kwenye kikao cha ugawaji wa maeneo na kupewa namba ya vibanda vyao.

Kikao hicho alikuwepo waziri wa fedha MWIGULU NCHEMBA alikuwepo kushuhudia zoezi hilo na pia alitoa AHADI kuwa mama SAMIA ametoa bilioni 2 kumalizia soko lote likamilike.

Sasa kizungumkuti kimetokea baada tu ya mkuu wa mkoa kuondoka,majina ya wale waliopewa vibanda awali yameandikwa VERIFIED lakini hawajapiga picha ya vitambulisho vya soko lile na kuambiwa waondoke watapigiwa simu. Huku wale waliondikwa kwenye majina yao ACTIVE wakipiga picha na kupatiwa vitambulisho vya soko hilo wakati wote wanafanya biashara eneo hilo miaka na miaka toka zamani.

Sintofahamu hiyo inakuja kwanini huyu wa active apewa na huyu wa verified asipewe na wote awali walipewa maeneo kabla hata ya soko halijakamilika vizuri ila baada ya kukamilika wanatemwa?
 
Hili jambo la kuwapora maeneo yao ndo linasababishaga masoko YACHOMWE MOTO. ili likijengwa upya lilete utata kama huu wamachinga warudi barabarani kukimbizwa na mgambo.
 
Serikali kwa hili ni dhuluma na litaleta vurugu huko mbeleni,watu wananunua nafasi za watu..wahusika halisi ambao ni machinga wameambiwa wa
 
Hili jambo la kuwapora maeneo yao ndo linasababishaga masoko YACHOMWE MOTO. ili likijengwa upya lilete utata kama huu wamachinga warudi barabarani kukimbizwa na mgambo.
Moto utawaka..we subiri tu
 
Tuache kulalamika!! Waliowekwa ni wanyaruanda!?
 
Serikali ndiyo ilisababisha haya yote kwa kuendekeza Siasa

Haikutakuwa mtu afanyie biashara barabarani
 
Serikali ndiyo ilisababisha haya yote kwa kuendekeza Siasa

Haikutakuwa mtu afanyie biashara barabarani
Sawa,ila km serikali imefanya juhudi ya kuwajengea maeneo ya biashara na imechukua list ya majina yao KWANINI SASA WAHUSIKA WANAOWAPANGA MAENEO HAYO YA BIASHARA KUCHUKUA RUSHWA NA KUINGIZA WASIOKUWEMO..(
 
Back
Top Bottom