Wamanyema ndio kabila pekee lenye watu majasiri, shupavu, na wajanja hapa nchini

Wamanyema ndio kabila pekee lenye watu majasiri, shupavu, na wajanja hapa nchini

Lakini pia hao watu wanasifika kwa kupenda kamserereko mpaka kujihusisha na mambo yanayotweza utu wao mfano huyo dimpozi pozi kwa pozi
Kuna jambo huwa ni mila, utamaduni na desturi ya kabila fulani. Na kuna jambo huwa ni tabia na mwenendo wa mtu fulani. Kwahiyo kama kuna jambo ambalo amefanya dimpoz basi amelifanya kutokana na tabia na mwenendo wake, ila sio kwa mila, utamaduni na desturi ya kabila lake. Nafikiri umenielewa bruh.
 
Natoa salamu kwenu marafiki na ndugu zangu. Kwa wale wasiolifahamu hili kabila. Wamanyema ni kabila linalopatikana katika mkoa wa Kigoma, hasa hasa maeneo ya mjini kama vile Kigoma mjini, Ujiji, Mwanga, Gungu na baadhi ya maeneo ya Kasulu mjini.

Yani toka enzi za ukoloni mpaka leo hii, mtoto wa mjini pale Kigoma ni mmanyema, japo miaka hii kuna waha wachache waliojisogeza sogeza na kufoji uenyeji wa mjini kwa kuiga mienendo na tamaduni za kimanyema nk.

Pia kabila hili la Wamanyema linapatikana katika baadhi ya maeneo ya mkoa wa Tabora, na huko Ufipa mkoani Rukwa.

Wamanyema ni kabila la pili kwa ukubwa mkoani Kigoma, kabila la kwanza kwa ukubwa mkoani humo ni Waha ambao wengi wanaishi vijijini, pamoja na makabila mengine madogo madogo.

Wamanyema ni kati ya makabila ya mwanzo mwanzo kabisa kufika katika mkoa wa Dar es salaam enzi hizo ikiitwa mzizima, kabla hata Tanganyika haijawaza au hata kufikiria kuwa kuna siku itapata uhuru.

Pia Wamanyema ndio lilikuwa kabila la kwanza la wageni kumiliki maeneo yote muhimu ambayo sasa ndio mjini kama vile Kariakoo, Ilala na Tabata.

Kwa watu wanaoishi au waliowahi kufika Dar es salaam nafikiri mnaufahamu msikiti wa Manyema uliopo katika katika ya mjini yani kariakoo, ule msikiti ulijengwa kabla ya uhuru na hakuna mkoloni yeyote aliethubutu kuugusa kwa vile hata wakoloni walilifahamu vizuri hili kabila, kwamba sio la kulifanyia mzaha hata kidogo.

Kabla mambo ya utandawazi hayajaeneo na kupelekea waha kuvamia miji kwa fujo hasa kwa mkoa wa Dar es salaam, watu wengi walikuwa wanajua kuwa Wamanyema ndio kabila pekee katika mkoa wa Kigoma.

Ila miaka inavyokwenda ndo na mambo yanavyozidi kujiweka wazi yenyewe, na kupelekea watu kujua makabila mengine ya mkoa wa Kigoma.

Wamanyema ni kati ya Makabila yaliopigania uhuru kwa kupambana na wakoloni, huku wakishirikiana na wenyeji wao wa Dar es salaam kama vile Wazaramo, Wandengereko na makabila mengine ya mkoa wa Pwani.

Tabia za wamanyema wake kwa waume ni 1] usafi 2] umaridadi 3]unadhifu. Wamanyema wengi ni maridadi sana kuanzia kwenye swala la mavazi, usafi wa mwili ndani na nje, pia huwa hawajinyimi kula.

Ni vigumu sana kumkuta mmanyema anatembeza mayai, sijui vikapu vya mafuta uzuri na biashara nyingine ndogo ndogo za kuzurula juani, hizi biashara kwa watu wanaotokea Kigoma iwe kwa mkoa wa Kigoma wenyewe, Dar au kwengineko huwa zinafanywa na waha.

Kwa mtu ambae ashawahi kuishi na wamanyema iwe jirani au nyumba moja nafikiri atakuwa amenielewa. Kama una mkeo au mumeo akinaswa na mmanyema tu basi andaa talaka, au kama mwanamke andaa kutalikiwa kabisa, maana mkeo au mumeo ndo umeshamkosa tayari.

Sifa nyingine 4]ubishi 5]kujiamini kupita kiasi. Mmanyema anaweza kutoa hela yake mfukoni akaununua ugomvi wa rafiki yake, na kuanza kupambana kwa niaba yake.

Watu maarufu kutoka katika kabila la Wamanyema ni 1]Sheikh Yahya Husein (aliekuwa mtabiri afrika mashariki) 2] Iddi Faiz Mafongo (aliekuwa mwekahazina wa chama cha TANU) 3] Iddi Tosiri 4] Iddi Simba (huyu mama alikuwa mmanyema, huku baba ni mdengereko) 5] Amri Abedi Karuta (meya wa kwanza jijini Dar) 6] Amani Kabouru (aliekuwa mbunge wa kwanza Kigoma mjini CDM) 7] Diamond 8] Ally Kiba 9] Ommy Dimpoz 10] mh Zitto Kabwe kiongozi wa ACT wazalendo (mbunge mstaafu) 11] Katibu mkuu kiongozi mh balozi Huseein A.
Katanga na wengine wengi serikalini, siasani, kwenye michezo, mziki na fani mbali mbali.

Tatizo kubwa la Wamanyema wa enzi hizo (yani mababu) ilikuwa ni ushirikina. Jambo lililosababisha wamanyema wengi kusambaa katika mikoa mingine hasa Dar es salaam na kujenga huko ili kuwaepuka vigagula hao.

Pia wamanyema hawana ushirikiano kivile katika mambo yanayohusu maisha. Iwe kazini, katika biashara na mambo mengi ya kimaendeleo huwa hawabebani kama yanavyobebana makabila mengine, yani kwa wamanyema kila mtu hubeba msalaba wake mwenyewe.

Kwa kukosa kushirikiano huo ndio maana mababu ambao ndio waliwahi kuwa wamiliki wa maeneo ya Kariakoo, Ilala, Tabata nk walipofariki, wale waliorithishwa maeneo hayo waliyauza yote kwa wahindi (K'koo) waarabu (Ilala) pia maeneo mengi ya Tabata waliorithishwa waliyauza kwa watu mbali mbali.
Pamoja na mbwembwe zote hizi lakini ndio kabila pekee ambalo halina lugha yake ya asili yani kilugha chake kama ilivyo wasambaa-kisambaa,wagogo-kigogo etc
 
Suala la ujasiri ni sifa ya Wakurya (kanda maalum) na mahasimu wetu wamasai pekee. Nyie wengine mnaongopa kujipa sifa ya ujasiri!
 
Wabwali, wakusu, wamasanze na wabembe hao wote ni jamii ya wamanyema bruh. Kama wewe ndo haujui uulize.
Hujui kitu wamanyema wanatokea Kasongo DRC wakati wabwari wanatokea Burundi
 
Pamoja na mbwembwe zote hizi lakini ndio kabila pekee ambalo halina lugha yake ya asili yani kilugha chake kama ilivyo wasambaa-kisambaa,wagogo-kigogo etc
Lugha ya asili ipo, hakuna kabila la kiafrika ambalo halina lugha ya asili, isipokuwa kiswahili ndio kimeimeza lugha yao. Leo hii hata vijana wa kizaramo wengi ukiwauliza hata salam ya kizaramo hawajui sababu, na wao babu zao waliendeleza sana kiswahili na kukifanya ndio lugha yao ya nyumbani.
 
bebi bebi bebi ndagushima chane ommy dimpo kaimba kiha hapo na sio kizaire aka kicongo
 
Yah..kn mzee mmj yuko tmk
Sahv anauza spare za machine(jina kapuni)utajiri wake ulitokea kwenye uwizi kwenye treni na pembe za ndovu

Ova
 
Tanzania ukitoa wahzabe na wagogo, makabila yaliobakia yote yalitoka sehemu mbali mbali za afrika. So kama wewe sio mmoja wa makabila hayo niliyoyataja hapa, basi hoja yako haina mashiko mkuu.
wahadzabe wana asili ya nchi za kusini,hata lugha zinafanana ,wanafanana hata na makhirikhiri
 
wahadzabe wana asili ya nchi za kusini,hata lugha zinafanana ,wanafanana hata na makhirikhiri
Afrika imeanzia juu (kaskazini + magharibi) kushuka chini (mashariki + kusini) kwahiyo hao wa kusini walianzia tanganyika (wahadzabe) wakateremka hadi kusini. Kumbuka historia inasema mifupa na hata nyayo za binadam wa kale kabisa zilipatikana ("Tanga", Tanganyika) Kwahiyo usishangae pengine hao wa kusini na sehem zingine za afrika wanaweza kuwa ni wahadzabe ambao walitoka Tanganyika zaman sana na kusambaa sehem zingine za Afrika ikiwepo hiyo kusini kutafuta chakula nk. Ndio maana hayati Magufuli kwa kutambua uchakachuaji wa historia yetu, alitakaa wataalam wake tena chini na kuiandika upya. Haiwezekani Tanzania tu ndio iwe nchi pekee ambayo kila kabila eti limetoka nchi nyingine.
 
Mhhhh. Wabwari wanatokea Burundi
Katiba ya burundi inatambua makabila matatu tu, yani watusi, wahutu na watwa. Hao wengine unawatambua wewe tu, lakini warundi wenyewe hawawatambui. Na hii sio kwa Burundi tu hata nje ya Burundi kwa mfano uki google kuhusu makabila ya Burundi, google itakuonesha makabila matatu tu niliyoyataja mimi hapo juu. Hao wabwari, wabembe nk ni migrants tu walioingia Burundi kipindi cha utumwa na ukoloni. Ila hawana asili na wala hawana uhusiano wowote na warundi. Wewe unaongea kwa hisia zako, mimi naongea kupitia fact za warundi wenyewe kwenye google, na pia wabeleji wenyewe ambao walitawala nchi zote mbili za Burundi na Congo. Hapo chini imeandikwa kwa kifaransa na wazungu wenyewe waliotawala nchi zote mbili, kwahiyo ukiachilia mbali warundi hawawatambui wabwari kama unavyosema ww lkn pia na wakoloni wanatambua kuwa ubwari walipotokea wabwari ipo Congo.
 

Attachments

  • Screenshot_20220610-112130.jpg
    Screenshot_20220610-112130.jpg
    47.8 KB · Views: 26
  • Screenshot_20220610-113223.jpg
    Screenshot_20220610-113223.jpg
    44.9 KB · Views: 21
Yah..kn mzee mmj yuko tmk
Sahv anauza spare za machine(jina kapuni)utajiri wake ulitokea kwenye uwizi kwenye treni na pembe za ndovu

Ova
Dah.. kwahiyo mkuu makabila mengine hayana wezi?
 
Haya unayoongea ni ya miaka hii, ila kuanzia 2000 kushuka chini maeneo mengi ya nchi, hakuna watu waliokuwa wanafahamu kabila linaloitwa waha.
Kwa taarifa yako utambulisho wa kabila ni lugha. Wamanyema wanaongea lugha gani?
 
Pamoja na mbwembwe zote hizi lakini ndio kabila pekee ambalo halina lugha yake ya asili yani kilugha chake kama ilivyo wasambaa-kisambaa,wagogo-kigogo etc
Ndo maana hawana sifa ya kuwa kabila.
 
Kama msikiti wa manyema ulijengwa kabla ya wakoloni na wakoloni( Waarabu ) ndio wenye dini yao sasa hao wamanyema uislam waliujulia wap???
 
Pamoja na mbwembwe zote hizi lakini ndio kabila pekee ambalo halina lugha yake ya asili yani kilugha chake kama ilivyo wasambaa-kisambaa,wagogo-kigogo etc
Kama unamaanisha lugha moja ni kweli Wamanyema hatuna lugha moja ya asili kama ilivyo kwa Wachaga ila tofauti na Wachaga sisi tunayo lugha unganishi "lingua franca" Kiswahili cha lahaja ya kiungwana, pia kwa mfanano na Wachaga tunazo lugha zaidi ya moja kufuatana na kabila dogo la ndani la kimanyema, mf. Mimi ni Mgoma na huzungumza Lugha ya Kigoma ambayo pia kiisimu hutambuliwa kama lahaja ya Lugha ya Kizyoba kama ilivyo Kibwari(Kabwari) na Kimasanze(Kisanze).
 
Hujui kitu wamanyema wanatokea Kasongo DRC wakati wabwari wanatokea Burundi
Hata wewe pia hujui kitu, siyo tu Kasongo bali Congo nzima hakuna kabila la Wamanyema, bali kuna jimbo linaitwa Maniema, Utambulisho wa jamii ya Wamanyema ni Tanzania pekee, na zaidi zaidi Ujiji tumezoeleka kama Waswahili, majina ya jamii nyingi hutolewa kwa dhana tofauti tofauti ila Wanaanthropolojia huhesabu watu fulani kuwa jamii tengefu kwa utangamano na mfanano wao mf. Wamanyema tuna utambulisho mmoja mkuu ambao ni utamaduni wetu wa kiungwana "Tanganyika-arabian" na kutokeza kama jamii moja, kuhusu utofauti wa asili za baadhi ya makabila hilo lipo kwa jamii karibu zote, mf. Waluguru wana koo km. wabena, wamwenda, wahafigwa na wachuma na zote zina asili tofauti zikakutana uluguru na kutengeneza utambulisho mmoja. Hivyo tofautisha Umanyema wa kikabila na Umanyema wa nasibu anaoweza itwa mtu wa Kasongo kwa vile ni jimboni Maniema, pia fahamu kabla hilo jimbo halijagawiwa mpaka Kivu(walikotokea Wabwari) ilikuwa ni moja na iliitwa yote Kivu-Manyema na jina Manyema ndo la asili siyo Kivu maana makabila karibu yote ya Wamanyema yana chimbuko la eneo lenyewe la Manyema hata kabla ya kusogea Kivu na hatimae Kigoma
 
Mhhhh. Wabwari wanatokea Burundi
Wabwari wenyeji wa Burundi wapo ila kiasili wanatokea Zoni ya Fizi katika Himaya ya kijadi ya nusu kisiwa ya Ubwari, ili jibu lako liwe sahihi inategemea unajibu kwa mtazamo gani.
 
Back
Top Bottom