Wamiliki wa lodge kuweni serious

Wamiliki wa lodge kuweni serious

Kama ungekuwa wewe ungeweza kutoa Geisha kwa kila mteja anapokodi chumba ?

Sabuni hizo zinapunguza cost kwa sababu inatumika once kesho inatakiwa zipatikane zingine hata hivyo ikiisha unaweza kuomba nyingine

Family inauzwa 500/= hizo geisha ni buku..!
Umelipa 50k mwenye lodge anapata hasara gani akitoa hizo? Vile visabuni kwanza vina harufu mbaya na kinyaa!
Binafsi mimi nikiwa safari inayonilazimu kulala lodge nakuwa na imperial ama dettol zangu!
 
Family inauzwa 500/= hizo geisha ni buku..!
Umelipa 50k mwenye lodge anapata hasara gani akitoa hizo? Vile visabuni kwanza vina harufu mbaya na kinyaa!
Binafsi mimi nikiwa safari inayonilazimu kulala lodge nakuwa na imperial ama dettol zangu!
Lodge ina vyumba 10, utoe 1000 kununua sabuni kila siku kwa mwaka utakuwa umetumia karibia milioni tatu kwa sabuni tu bado za kufulia, umeme na kodi hiyo Lodge italipa kweli ???
 
Family inauzwa 500/= hizo geisha ni buku..!
Umelipa 50k mwenye lodge anapata hasara gani akitoa hizo? Vile visabuni kwanza vina harufu mbaya na kinyaa!
Binafsi mimi nikiwa safari inayonilazimu kulala lodge nakuwa na imperial ama dettol zangu!
Kubeba sabuni yako haukatazwi ile ni biashara lazima mtu atoe inayompa faida.

Pale siyo home kwamba upewe home services.
 
Nshakutana na mavi mabichi bafuni ,nikajiuliza inamaana huyu muhudumu alinitandikia hajaona hayo mavi au ni yeye kanya na ilikua haihitaji DNA kujua ni yupi mzazi wa Lile kimba yaani Lile kimba lilikua ni yule muhudumu copyright ,nikaamua kuachana nao nikaenda kulala msikitini tu
 
Siku moja 2020 nilienda Ifakara nikafikia Lodge fulani mpya ipo karibu na Stand ya Mabasi ni lodge kali sana na huduma ziko sawa sawa.

Ila changamoto iliyonikuta nililala vizuri asubuhi nimeamka na mvi shuka inatoa nyuzi hatari kila nguo ukigusisha kwenye shuka la kitanda unaokota nyuzi za shuka.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nshakutana na mavi mabichi bafuni ,nikajiuliza inamaana huyu muhudumu alinitandikia hajaona hayo mavi au ni yeye kanya na ilikua haihitaji DNA kujua ni yupi mzazi wa Lile kimba yaani Lile kimba lilikua ni yule muhudumu copyright ,nikaamua kuachana nao nikaenda kulala msikitini tu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Lodge ina vyumba 10, utoe 1000 kununua sabuni kila siku kwa mwaka utakuwa umetumia karibia milioni tatu kwa sabuni tu bado za kufulia, umeme na kodi hiyo Lodge italipa kweli ???

Wewe kweli ni hewa tu! Unakuja na hesabu za kiduwanzi!
Kwa hivyo vyumba 10, kwa malipo ya 50k kwa siku, mapato ni zaidi million180, ikitumika hiyo million 3 kuna hasara gani, wakati running cost haifiki hata million80?
Wewe utakuww mhudumu wa guest house siyo bure!!
 
Siku moja Moshi mjini mitaa ya Majengo nilichukua room kwenye lodge moja, 20k. Nilipoingia tu nikafunga mlango wa room kwa funguo, nikavua nguo direct kuoga bafuni. Huko bafuni nililazimika kurudishia mlango maana bafu ni dogo sana. Ile nafunga mlango nikasikia kitu kinaanguka upande wa pili wa mlango (upande wa chumbani). Sikujali nikaendelea kuoga.

Nimemaliza kuoga nafungua mlango haufunguki. Kumbe handle ya kitasa upande wa nje na kile kijichuma kinaunganisha handles na kitasa ndio vinedondoka.

Niliita wahudumu kwa nguvu sana ila wasisikie mpaka koo likauma na matusi yote hapo nimeshamaliza, na hakuna hata mteja mwingine room jirani anisikie awaambie. Wamekuja baada ya nusu saa hivi ila hawawezi kuingia chumbani kwangu kwani nimefunga. Funguo za akiba hawana anazo boss mwenye guest house. Boss amepigiwa yupo mbali, shambani. Alikuja baada ya kama 3hrs hivi. Muda wote huo nipo chooni tu.

Walipofungua nikatoka. Jicho nililowakata wakaelewa namaanisha nini. Wakanirudishia hela yangu bila kusema chochote nikaondoka kutafuta lodge nyingine.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Aiseee..
 
Kupata muda wa kutosha wa kuandaa chumba kwa ajili ya wageni wengine, na wakati mwingine unakuta chumba kilishakuwa booked.
kuwa booked na mimi niko ndani less than 24hrs?
By the way mimi nikiwa nakaa hotel like 3 days huwa nakataa hizo mambo za kuingia kufanya usafi na kubadil mashuka na kufanya usafi mpaka siku naondoka
 
Sometimes mtu anasafiri analazimika kuchukua chumba lodge Kwa sababu mbalimbali ikiwemo ukaribu wa anapokwenda mfano kikazi mtu atachukua lodge karibu na ofisi, au ukumbi wa mikutano na kadhalika. Sometimes kwa sababu ya lodge zingine kuwa zimejaa n.k..

Lakini sasa unaona lodge nzuri Kwa nje na hata ndani Kwa macho unaona iko Sawa, unalipia ulale unashangaa na unayo kutana nayo.

1. Feni inapiga kelele.
2. Bomba bovu maji yanatiririka bafuni.
3. Vitasa vibovu.
4. Mlango wa bafuni haufungi.
5. Taa bafuni haiwaki
6. Kitanda kinatoa milio
7. Mto ngumu Sana au mlaini Sana..
8. Feni haipungui wala kuongezeka Ama uwashe au uzime.
9. AC inapiga kelele
10. Tiles bafuni zina kutu.
11. Wahudumu Wana makelele.

Mradi matatizo ni mengi ambayo mtu anaejali biashara yake ni rahisi kabisa kutatua.

Nashauri kama mtu unamiliki lodge au kuendesha uweke utaratibu wa kulala wewe mwenyewe kila chumba Kwa mda Fulani ukague ujirishishe na huduma unazotoa.

Kuna lodge chumba kimoja kina joto kuliko chumba kingine Nakadhalika.

Kuweni serious, lodge ni sehemu ya mteja kulala comfortable sio kuwaza wateja wote wanaenda kwa ngono tu na kuondoka.
Hiyo ndio shida ya kulala sehemu ya Tsh 10k mpaka 15k. Ukilala sehemu ya at least 40-60k hutoona kadhia hizo.
 
30. Neti imetoboka na imefungwangwa mafundo ya matundu au imeshonwa na ni chafu ukiigusa tu lazma upige chafya na upate mafua.
31. Shuka zina madoadoa, godoro lina madoadoa ya kutisha (nashauri epuka kufunua funua shuka kuona hali ya godoro, maana usingiz utatoweka) na limebonyea mno katikati hadi mbavu au mgongo unagusa chaga.
32. Taulo zina uvundo
33. Kandambili rangi tofauti
34. Kandambili imekatwa kwa mbele
 
Back
Top Bottom